Nimekuwa nikisoma gageti la Al-Huda lakini naona baadhi ya habari zake ni za uongo - hasa kama zinahusu Ukristo au Kanisa Katoliki. Huwa najiuliza kwa nini mtu mwenye akili timamu akae chini na aanze kuandika kitu anachoamini siyo kweli na ni kwa maslahi ya nani?
Katika toleo Na. 281 (Alhamisi Mei 28-Juni 3, 2009) ukurasa wa mbele gazeti hili limeandika:
KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2010...
Kanisa Katoliki laanza mchakato kuweka utawala mpya Tanzania
. Lapita nyumba kwa nyumba kuhamasisha
. Ladai kutoa mwongozo kwa waamini wake
Ukisoma habari hii, utaona ni mwendelezo wa upotoshaji ulioanzishwa na gazeti la The Sunday Citizen la Mei 3 mwaka huu. Katika ukurasa wa mbele wa The Sunday Citizen lilichachapisha 'story' kuhusu Kanisa Katoliki na kuipa kichwa cha habari ambacho ni 'twisted'.
Kilisema hivi: 'Catholic church pushes for choice of next president' na kueleza: 'The Catholic Church in Tanzania has launched a comprehensive project whose aim is to influence the 2010 electorate process, and ensure that the country gets a leader of the Churchs choice.'
Ukisoma kijitabu kinachozungumzwa na kile ambacho gazeti hilo lilitaka kieleweke kwa wasomaji na pia kile ambacho gazeti la Al-Huda linapigia debe ni vitu tofauti kabisa na nia na maelezo ya kijitabu/vijitabu vyenyewe au Kanisa lenyewe. For how long are we going to continue doing this?
Kwa nini mwandishi/mhariri wa Al-Huda asisome hicho kijitabu au vijitabu kwanza kuliko kuendeleza uongo au kuna maslahi katika uongo? Pamoja na mambo mengine, moja ya uongo ulisomemwa na gazeti hili unaonekana katika 'quotation' iliyotumiwa na gazeti hilo na inaenda hivi:
"In the last two years Council of Elders thrice met the President of Tanzania to press issues of common interest." Haya ni maneno gazeti la Al-Huda linasema limeyatoa kwenye tovuti ya Kanisa Katoliki na limeyatafsiri hivi: 'Katika kipindi cha miaka miwili iliyopita Baraza la Wazee lilikutana na Rais wa Tanzania mara tatu kushinikiza masuala yenye maslahi kwa Kanisa.'
Sasa, tafsiri ya 'issues of common interest' ni kweli 'masuala ya maslahi kwa Kanisa'?
Nia ya chombo chochote cha habari ni kuielemisha jamii juu ya mambo yanayowahusu na kutafuta njia za kuyatatua (kama ni matatizo), kuyakabili (kama ni changamoto) na kuyandeleza (kama yanajenga) na siyo kusema uongo dhidi ya dhehebu au dini fulani.
Watanzania lazima tubadilike. Dini maana yake ni chombo kinachoendeleza 'spiritual values' ili waumini wake wawe na imani na kutenda mema. Dini siyo chombo cha malumbano na tukitumia imani zetu kupotosha umma hatufanyi hivyo kwa sababu ya dini zetu bali ubinafsi wetu. Kuendelea kiimani au kijamii ni kupiga hatua katika ukweli, uwajibikaji, haki, kuunganisha watu na siyo kuwafanya wawe maadui.
Katika toleo Na. 281 (Alhamisi Mei 28-Juni 3, 2009) ukurasa wa mbele gazeti hili limeandika:
KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2010...
Kanisa Katoliki laanza mchakato kuweka utawala mpya Tanzania
. Lapita nyumba kwa nyumba kuhamasisha
. Ladai kutoa mwongozo kwa waamini wake
Ukisoma habari hii, utaona ni mwendelezo wa upotoshaji ulioanzishwa na gazeti la The Sunday Citizen la Mei 3 mwaka huu. Katika ukurasa wa mbele wa The Sunday Citizen lilichachapisha 'story' kuhusu Kanisa Katoliki na kuipa kichwa cha habari ambacho ni 'twisted'.
Kilisema hivi: 'Catholic church pushes for choice of next president' na kueleza: 'The Catholic Church in Tanzania has launched a comprehensive project whose aim is to influence the 2010 electorate process, and ensure that the country gets a leader of the Churchs choice.'
Ukisoma kijitabu kinachozungumzwa na kile ambacho gazeti hilo lilitaka kieleweke kwa wasomaji na pia kile ambacho gazeti la Al-Huda linapigia debe ni vitu tofauti kabisa na nia na maelezo ya kijitabu/vijitabu vyenyewe au Kanisa lenyewe. For how long are we going to continue doing this?
Kwa nini mwandishi/mhariri wa Al-Huda asisome hicho kijitabu au vijitabu kwanza kuliko kuendeleza uongo au kuna maslahi katika uongo? Pamoja na mambo mengine, moja ya uongo ulisomemwa na gazeti hili unaonekana katika 'quotation' iliyotumiwa na gazeti hilo na inaenda hivi:
"In the last two years Council of Elders thrice met the President of Tanzania to press issues of common interest." Haya ni maneno gazeti la Al-Huda linasema limeyatoa kwenye tovuti ya Kanisa Katoliki na limeyatafsiri hivi: 'Katika kipindi cha miaka miwili iliyopita Baraza la Wazee lilikutana na Rais wa Tanzania mara tatu kushinikiza masuala yenye maslahi kwa Kanisa.'
Sasa, tafsiri ya 'issues of common interest' ni kweli 'masuala ya maslahi kwa Kanisa'?
Nia ya chombo chochote cha habari ni kuielemisha jamii juu ya mambo yanayowahusu na kutafuta njia za kuyatatua (kama ni matatizo), kuyakabili (kama ni changamoto) na kuyandeleza (kama yanajenga) na siyo kusema uongo dhidi ya dhehebu au dini fulani.
Watanzania lazima tubadilike. Dini maana yake ni chombo kinachoendeleza 'spiritual values' ili waumini wake wawe na imani na kutenda mema. Dini siyo chombo cha malumbano na tukitumia imani zetu kupotosha umma hatufanyi hivyo kwa sababu ya dini zetu bali ubinafsi wetu. Kuendelea kiimani au kijamii ni kupiga hatua katika ukweli, uwajibikaji, haki, kuunganisha watu na siyo kuwafanya wawe maadui.