kwanza tutake radhi mama zako ebho!! hivi kwa akili zako wewe ukigundua mkeo na serengeti boy mtaani utafurahi?ndio maana nasemaga wanawake tujitahidi kutafuta kipato na sio kunyoosha mkono kila uchao, unadiriki kusema kuwa sasa wanaangaliana usoni so ulitaka akae kimya kwa sababu hana mbele wala nyuma ili waendelee kupata huo mlo wa kila siku na bwana yake aliendelee na uzinzi wake? tatizo sio kwamwambia siri za office tatizo ni dharua alofanya huyo bwana ya kuwa na mwanamke tena hapo hapo mtaani kwao, akaanza kuleta dharau kwa mkewe. kesi kama hizo ni nyingi sana hata ninapofanya kazi mie kila mara wanawake wanakuja getini kulalamika kuwa wametelekezwa na waume zao hata wanapopata off hawaendi nyumbani huishia hoteli na sehemu mbali mbali za starehe bila kujali kuwa ana familia inamtegemea, kinachofuata ni mwanamke kuulizia roster ya mume wake kwa marafiki zake nao bila hiana humwambia ( shemeji mbona mumeo yupo off hii week ya pili?) anachukua hatua ya kutinga kazini kwa mumuwe, je mwanaume kama huyo akifukuzwa kazi lawama kwa mkewe, wanaume jiangalieni sio kupata vijisenti ya kubadilisha raba ukamsahau mkeo mliesota nae mkikaanga maandazi leo hii unaendesha mchuma wako huku mkeo akiangalia watoto wako unamwona hajui haendi na wakati loh.........nawakilisha.