Wanyakyusa Wajanja sana kwa kusaka hela na hasa vibabu. Ila wote tunajua General Mboma ndiyo alikomba za kutosha na kwenda kuzificha Kyela. Yaani haka kawilaya kadogo ila kameshatoa Wakuu wawili wa JWTZ, Msemaji wa Polisi, Mkuu wa Upepelezi Tanzania, Mbunge aliyesababisha Waziri Mkuu ajiuzulu, Mwanakijiji, Mtanzania, Babu wa Loliondo .......
Sasa hebu Mtanzania atupe habari zaidi, kwa nini Babu kaanzia kwenye Radio yake ya Kyela FM? Au wewe kijana na wewe umeanza Ujasilimali wa Babu wa Loliondo? Hahahaaaaaa, Wanyakyusa mpo juu sana. Kuna haja ya sisi jirani zenu wa Sikonge tujifunze mengi sana kutoka huko kwenu.
Kweli tutafika ?
Kama mtu anafika Studio ya Redio na kukaribishwa na kuuanza kumwaga pumba kama hizi alafu mtangazaji naye anaruhusu Ujinga kama huu sijui huko mbele ya safari Mungu atuongoze!
hili lichama linaamini sana mambo ya ushirikina na endapo wataidandia hii theory ya huyu mzee majibu yako wazi, akimfufua wanashinda akishindwa kumfufua vis-vesa
Sim'bishii huyo babu anasema kweli kabisa, hivi hamjui kwamba hii nchi inaongozwa na mizimu? 75% ya viongoz wa CCM na serikali yao wote ni mizimu tu, wenyewe walishakufa muda mrefu sana na hii iliyopo sasa ni mizimu yao!