KERO Ajira Mpya TAMISEMI Sumbawanga tunalia njaa, tusaidiwe fedha zitoke, tukihoji HR anakuwa mkali

KERO Ajira Mpya TAMISEMI Sumbawanga tunalia njaa, tusaidiwe fedha zitoke, tukihoji HR anakuwa mkali

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Ninaomba mtusaidie kupaza sauti kuhusu suala la kupata pesa za kujikimu sisi ajira mpya upande wa TAMISEMI Sumbawanga Municipal Council.

Nimepata ajira yangu huku lakini ninayoyasikia na kuyaona yanaumiza sana.

Kinachumiza zaidi ni kwamba HR wa Manispaa ni mkali kama pilipili alituambia siku tunafika kwamba, ole wetu tuanze kulalamika kuhusu hela ya kujikimu tutamjua.

Hata kwenye group huko WhatsApp watu baadhi walipojaribu kugusia suala la PESA ZA KUJIKIMU, huyo HR aligeuka kuwa mbogo.
 
Ukiwa huna kazi shida, ukipata kazi shida, kila kitu ni shida, hii shida itaisha lini mpaka siku ya mwisho..Huyo HR hajitambui hapaswi kuwa mkali anatakiwa awaelekeze lini watapata stahiki yao ni kipi kinakwamisha mpaka sasa na hatua zinazochukuliwa hili kutatua....Hili nalo mkalitazame.
 
Waajiriwa wengi wa nchii ambao hawapo kwenye kilo ya uwizi ndo wanaongoza Kwa kulia njaa kuliko hata majobless, lakn wao ndo mtaji wa uongozi kwenye kazi za hovyo na kununulika Kwa pesa ndogo sana.
 
Kwani huyo HR hana mkubwa wake mkamreport mbona kama hela anatoa mfukoni kwake kama kuna shida yoyote si anapaswa kuwapa majibu ya faraja
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom