BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,376
- 8,117
Watu watatu wamefariki dunia kwenye ajali iliyohusisha Lori lililobeba wafanyabiashara waliokuwa safarini kwenda Handeni mkoani Tanga kwa ajili ya mnada.
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Handeni, Dr. Hudi Shehdadi amethibitisha kupokea miili ya watu watatu na majeruhi 36 huku akieleza majeruhi 11 hali zao sio nzuri kutokana na majeraha waliyopata.
Kwa mujibu wa Rajabu Juma ambaye ni mmoja wa majeruhi, ajali imetokea eneo la Kwamagome baada ya Lori hilo kushindwa kukata kona.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Sofia Jongo hakupatikana kuzungumzia ajali hiyo, msaidizi wake ameeleza kuwa kamanda yupo kwenye msafara wa kumpokea Rais Samia Suluhu Hassan ambaye ameanza ziara mkoani Tanga.