Lori lagongana na Coaster uso kwa uso, watu tisa wafariki dunia

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,634
697,867
Kuna taarifa ya ajali barabara ya Msata-Bagamoyo daladala Coaster imegongana na lori imeua watu wote. Tungoje taarifa zaidi.

Mwenyezi Mungu azilaze roho za marehemu panapostahili.

======

Watu tisa wamefariki dunia na wengine watatu kujeruhiwa katika ajali ya barabarani baada ya basi dogo la abiria aina ya coster lililokuwa likitokea Dar es Salaam kuelekwa Bagamoyo, kugongana uso kwa uso na lori lililokuwa limebeba mawe, eneo la Kiromo Bagamoyo.

Kamanda wa Polisi mkoani Pwani, Pius Lutumo amesema ajali hiyo imetokea Machi 10, 2024 majira ya saa 11 jioni na kwamba chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa dereva wa lori, aliyekuwa akiyapita magari mengine eneo ambalo haliruhusiwi kufanya hivyo.

Ameongeza kuwa miili ya waliofariki katika ajali hiyo imehifadhiwa kwenye Hospitali ya Wilaya ya Bagamoyo.


View: https://youtu.be/kU4ClnU4epI?si=rH9gWLwo1odNIwH8
 
shuhuda
I was there , Coaster imebakiza majeruhi wawili tu, ambao pamoja na marehemu wamefikishwa hospitali ya wilaya...Lori pia hakuna alietoka...Inatisha sana iyo ajali, miili mingine imefanywa kuokotwa vipande vipande yaani inatisha kuangalia...Eeeh Allah 🤲
 
Kuna taarifa ya ajali barabara ya Msata-Bagamoyo daladala Coaster imegongana na lori imeua watu wote. Tungoje taarifa zaidi.

Mwenyezi Mungu azilaze roho za marehemu panapostahili.


View: https://youtu.be/kU4ClnU4epI?si=rH9gWLwo1odNIwH8

Daaah inauma sana mtu anapoteza maisha angali ana umri wa kukamilisha hapa duniani. Hii ni kazi ya shetani. Mungu akiweka ahadi yake huwa anaitimiza. Tunaishi miaka 70 kinyume na hapo ni ubatili.

Poleni kwa familia zote waliopoteza ndugu na jamaa kwenye ajali hiii.

Mafisadi dhambi hii mtaibeba maisha yenu yote. Mnapokwapua fedha za umma tunakosa hela za kufanya miradi ya barabara za njia 4 nchi nzima. Ajali hii ingeepukika endapo tungelikuwa wote wasafi, wakweli na wenye hofu ya Mungu
 
Back
Top Bottom