Ajali ya Dr. Mwakyembe na yatokanayo

Wote mnakosea! habari za uhakika kabisa ni kuwa Dr Mwakyembe karogwa na kundi la mafisadi RA, EL, nk
 
Mtanzania huyu ni mkuu Mwakalelei,Mkuu Mwanjelwa kapotea kiaina.
Mkuu Jmushi1,

Asante mkuu kwa masahihisho, unajua haya majina ya mwa yamejaa kichwani mpaka mtu unachanganya. Asante na nimerekebisha ile post yangu.
 
Mr Mwakyembe explained that a lorry was overtaking his car and suddenly a minibus appeared on the opposite direction.

“That is when my driver decided to accelerate so that he could allow the lorry to go back. But the lorry kept on accelerating as well and knocked my car from the back causing it to lose direction before knocking a tree and overturned,” he said.

Gari ya Mh Mwakyembe ilikuwa katika mwendo wa kasi.
Dereva wa mwakyembe hakufanya maamuzi sahihi, kitendo chake cha kuongeza mwendo kingeweza kusababisha lorry kugongana na basi la abiria.
Kwa mantiki hiyo basi, inawezekana dereva wa lorry alipoona kuwa gari la Mwakyembe linaongeza mwendo njia sahihi ya kuepusha ajali na basi ni kuilazimisha land cruiser isalimu amri.
Huo uamuzi una hasara na faida zake, kwa hiyo tunaweza kuangalia ni zipi hasara na je zipi ni faida.
Bottom line kama lorry tayari lilikuwa limeruhusiwa kuipita gari ya mheshimiwa basi hakukuwa na sababu za dereva wa mheshimiwa kuongeza mwendo.
Mh alisema lorry lilikua mbele yake na driver akawaruhusu ku overtake lakini wakati wamepita trailer ya nyuma yule driver wa lorry aka swing kichwa kutaka kuwagonga. Driver wa Mh akaongeza mwendo kukwepa lakini driver wa lorry akawagonga kidogo nyuma kumfanya driver wa Mh akose mwelekeo na ku overturn. Coaster lilikua linakuja kwambali mbele.
 
Mtanzania,
Hakika hatuwezi kusingizia barabara kuwa sababu ya ajali zetu ikiwa sisi wenyewe ndio wajenzi wa hizi barabara..Ni miaka mingapi sasa hivi toka nisikie barabara ya Mbeya - Dar inawaondoa watu kila siku kwa ajali!. Zamani ilikuwa barabara ya kati na hasa pale Sekenke. Huwezi kuamini watu tulikuwa tukiomba Mungu pindi bus linapokaribia eneo hilo..Why? kuyaweka maisha yake mikononi mwa Mungu mahala ambapo sisi wenyewe ndio jukumu letu kuhakikisha usalama. Mbali na yote haya ya Usalama barabara ni kiungo kikubwa sana cha Uchumi wa nchi. Tunasahau kwamba barabara ile Ya Dar Mbeya ilipotengenezwa misafara yote ya magari ya mizigo kwenda Zambia, Zimbabwe na Zaire (Kongo) yaliitumia barabara hiyo na kulikuwepo na ongezeko kubwa sana ktk uchumi wetu enzi hizo..
Tofauti na wenzetu Ulaya, nchi za Kiafrika bado zinashindwa kuelewa mfumo mzima wa Ubepari na hasa ktk ukupanga vipaumbele. Sisi tunajenga miundombinu kwa sababu tofauti kabisa, yaani barabara ya Iringa itajengwa au kuimarishwa kwa sababu ya vifo au ajali zinazotokea na hasara kubwa kwetu ni kupoteza maisha ya watu. Wakati hawa wenzetu Miundombinu hutazama kwanza Uchumi wa nchi na uzalishaji wake, safety ni kipengele kinachoingia ktk ujenzi sii sababu ya Ujenzi wa Muundombinu. Ndio maana siku zote tuko nyuma kaatika mambo mengi kwa sababu hadi mtu afe au malalamiko ya watu ndipo tunapoanza kufikiria ulazima wa kuboresha Miundombinu ili kukuza uchumi na kuboresha maisha ya wananchi wake. Uchumi unafuatia mahitaji ya watu.. sii kutangulia mahitaji hayo.
Barabara nzuri moja kwa moja hupunguza ajali na kinachotisha zaidi ni kwamba bado tuna tumia elimu ya Kijamaa ktk mambo mengi sana..Tunafikiria Kuboresha maisha ya mananchi pasipo kuboresha Uchumi, yaani ujenzi wa miundombinu itazame kwanza safety na ubora wa vitu hivyo ktk matumizi ya wananchi wake badala ya kutazama vitu hivyo ktk kuboresha Uchumi wa nchi. Ni mara zote nchi zenye Uchumi bora, xenye Miundombinu bora, maisha ya wananchi wake kuboreka zaidi!..Hata hizo kero za wananchi mara nyingi zinahusu huduma na mahitaji yao wao binafsi na sii mahitaji ya vianzio vya kukuza uchumi na kuongoeza ajira ktk mazingira yao.
 
Ni Mungu tu amenisaidia -Dk Mwakyembe
broken-heart.jpg
Na Patricia Kimelemeta

MBUNGE wa jimbo la Kyela, Harrison Mwakyembe amesema kuwa dereva wa lori alionekana amepania kuwaingiza kwenye ajali mbaya ya gari juzi na kwamba kunusurika kwake kumetokana na rehema za Mungu.

Mbunge huyo machachari katika vita ya ufisadi alisita kuhusisha moja kwa moja ajali hiyo na jaribio la wapinzani wake kutaka kummaliza, lakini akasema kama ajali hiyo ilitokana na njama hizo au haikutokana na njama, msimamo wake ni ule ule: kuendeleza vita dhidi ya ufisadi.

Dk Mwakyembe, aliyeongoza kamati teule ya Bunge ambayo ripoti yake ilifichua kashfa nzito dhidi ya kampuni ya Richmond Development (LLC), jana alionekana mwenye ahueni baada ya kuumia kwenye ajali ya gari wakati akisafiri kutoka Mbeya kuja Dar es salaam na akasimulia jinsi ajali hiyo ilivyotokea.

Alisema ajali hiyo ilitokana na gari la mizigo aina ya Scania kuwagonga kwa ubavuni na kusababisha gari yake kuacha njia na kupinduka mara tatu.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana katika hospitali ya Taasisi ya Mifupa (MOI), Mwakyembe alisema wakati wanafika eneo la Ihemi walikutana na lori ambalo lilikuwa mbele yao.

Alisema walijaribu kuomba njia ili waweze kupita, lakini dereva wa lori hilo alikataa, ndipo walipoamua kulipita.

"Nilimwambia devera amwashie dereva wa lori taa kumuarifu kuwa tunapita, na yeye akaturuhusu na ndipo tulipoanza kummpita," alisema Mwakyembe.

"Kabla ya kumalizika kulipita, dereva wa lori hilo aliongeza mwendo na baadaye kufungua kioo kabla ya kukifunga na kutugonga upande wa kushoto wa nyuma wa gari letu na kusababisha tuanguke.

"Yule dereva tulimuomba njia zaidi ya mara tatu, lakini alikataa tukawasha indiketa za kumuonyesha kuwa tunataka kupita, lakini alituruhusu kupita kabla ya kumaliza bodi ya gari lake ndipo alipotupa 'bodi' kwa nyuma."

Aliongeza baada ya kutokea kwa ajali hiyo dereva wa lori hilo aliongeza mwendo na kutokomea, jambo ambalo liliwafanya washindwe kusoma namba.

"Kama ajali niliyoipata imepangwa na Mungu, namuomba anisaidie ili niweze kuona, lakini kama imepangwa na binadamu katika kuzima mikakati yangu ya kupambana na ufisadi, nitaendelea na msimamo wangu hadi mwisho," alisema Dk Mwakyembe.

"Ajali iliyonitokea haitokani na kupambana na ufisadi. Ni ajali ya kawaida japokuwa ilikuwa mbaya na ambayo ingeweza kuhatarisha maisha yangu. Lakini mkakati wangu wa kupambana na ufisadi utabaki pale pale, hivyo namuomba Mungu anisaidie."

Dereva wa gari ya Mwakyembe, Joseph Msuya alisema kuwa dereva wa lori hilo alionekana kudhamiria kuwaua kwa sababu walishaomba njia zaidi ya mara tatu, lakini alishindwa kuwajibu.

"Niliomba njia zaidi ya mara tatu, lakini hakunijibu chochote. Nikaamua kupita kwa lazima ndipo na yeye aliponiwekea bodi ya gari lake kwa nyuma na kutuangusha,"alisema Msuya.

Hata hivyo mganga mkuu anayemshughulikia Mwakyembe, Profesa Joseph Kahamba alisema kuwa, mgonjwa huyo anayendelea vizuri baada ya kupata matibabu.

"Tulidhani amevunjika taya tulipoona uvimbe, lakini tumempima na kubaini kuwa hakuna kiungo chochote kilichoathirika zaidi ya maumivu ya ajali. Ikiwa tutabaini matatizo mengine tutatoa taarifa,"alisema Profesa Kahamba.

Aliongeza kuwa mpaka sasa mgonjwa wake anaendelea na matibabu kama kawaida, jambo ambalo limemsaidia kupunguza maumivu anayoyasikia.

Jana watu wengi walikuwa wakifurika Muhimbili kwenda kumpa pole mwakilishi huyo wa wananchi wa Kyela.

Baadhi ya viongozi wa chama na Serikali waliofika kumpa pole hospitalini hapo ni pamoja na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Wiliam Lukuvi.

Wengine ni pamoja na mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Davis Mwamunyange, kamanda wa polisi wa kanda ya Dar es salaam, Suleyman Kova na jaji mstaafu, Joseph Sinde Warioba.
uma maoni kwa Mhariri
 
Kuna kijana mmoja wa nyumbani ambaye yuko polisi hapo Iringa (ni officer))na alikuwa katika watu waliomsaidia Dr. Mwakyembe baada ya kupata ajali na kushughulikia suala zima. Anasema dereva wa lori alipatikana na alishahojiwa na polisi. Mimi sina uhakika mlioko huko mnaweza ku confirm na polisi. Hii habari ninayotoa hapa ni kusaidia wengine muweze kupata ukweli zaidi.

Anasema kwa ataarifa alizo nazo yeye anaweza kusema kwa asilimia 100 kwamba makosa yalikuwa ya dereva wa Dr. Mwakyembe na sababu kubwa ni mwendo wa kasi na kutaka ku overtake sehemu ambayo haitakiwi kufanya hivyo.

Anasema kulingana na dereva wa lori ni kweli hakumruhusu dereva wa Dr apite kwasababu yeye analijua hilo eneo kwamba ni hatari na hivyo hakumpa nafasi ya ku overtake lakini dereva wa dr akalazimisha na kutaka ku overtake kisha ghafla akaona gari lingine linakuja na hivyo kulazimisha kurudi kwenye upande wake. Kwa kusoma hapa JF mimi nilipata mawazo kwamba dereva wa lori hajapatikana.

Pia ni kama polisi wana wasiwasi na wao kuingizwa kwenye siasa kwenye hili suala.

kama nilivyoandika mwanzoni, nimeongea na kijana mmoja tu na sina njia ya kuthibitisha hiyo habari kwa kutumia sources zingine. Ila ninamwamini huyo kijana na ninafikiri anasema kweli.
 
Mtanzania,
Hakika hatuwezi kusingizia barabara kuwa sababu ya ajali zetu ikiwa sisi wenyewe ndio wajenzi wa hizi barabara..Ni miaka mingapi sasa hivi toka nisikie barabara ya Mbeya - Dar inawaondoa watu kila siku kwa ajali!. Zamani ilikuwa barabara ya kati na hasa pale Sekenke. Huwezi kuamini watu tulikuwa tukiomba Mungu pindi bus linapokaribia eneo hilo..Why? kuyaweka maisha yake mikononi mwa Mungu mahala ambapo sisi wenyewe ndio jukumu letu kuhakikisha usalama. Mbali na yote haya ya Usalama barabara ni kiungo kikubwa sana cha Uchumi wa nchi. Tunasahau kwamba barabara ile Ya Dar Mbeya ilipotengenezwa misafara yote ya magari ya mizigo kwenda Zambia, Zimbabwe na Zaire (Kongo) yaliitumia barabara hiyo na kulikuwepo na ongezeko kubwa sana ktk uchumi wetu enzi hizo..
Tofauti na wenzetu Ulaya, nchi za Kiafrika bado zinashindwa kuelewa mfumo mzima wa Ubepari na hasa ktk ukupanga vipaumbele. Sisi tunajenga miundombinu kwa sababu tofauti kabisa, yaani barabara ya Iringa itajengwa au kuimarishwa kwa sababu ya vifo au ajali zinazotokea na hasara kubwa kwetu ni kupoteza maisha ya watu. Wakati hawa wenzetu Miundombinu hutazama kwanza Uchumi wa nchi na uzalishaji wake, safety ni kipengele kinachoingia ktk ujenzi sii sababu ya Ujenzi wa Muundombinu. Ndio maana siku zote tuko nyuma kaatika mambo mengi kwa sababu hadi mtu afe au malalamiko ya watu ndipo tunapoanza kufikiria ulazima wa kuboresha Miundombinu ili kukuza uchumi na kuboresha maisha ya wananchi wake. Uchumi unafuatia mahitaji ya watu.. sii kutangulia mahitaji hayo.
Barabara nzuri moja kwa moja hupunguza ajali na kinachotisha zaidi ni kwamba bado tuna tumia elimu ya Kijamaa ktk mambo mengi sana..Tunafikiria Kuboresha maisha ya mananchi pasipo kuboresha Uchumi, yaani ujenzi wa miundombinu itazame kwanza safety na ubora wa vitu hivyo ktk matumizi ya wananchi wake badala ya kutazama vitu hivyo ktk kuboresha Uchumi wa nchi. Ni mara zote nchi zenye Uchumi bora, xenye Miundombinu bora, maisha ya wananchi wake kuboreka zaidi!..Hata hizo kero za wananchi mara nyingi zinahusu huduma na mahitaji yao wao binafsi na sii mahitaji ya vianzio vya kukuza uchumi na kuongoeza ajira ktk mazingira yao.

Bob,

Kitu cha kwanza kabisa katika design ya miundombinu yeyote ile cha kuzingatia ni SAFETY......hiyo ndio itahakikisha kuwa
1.Hatupotezi vijana wetu wasomi kama rafiki yake Mtanzania aliyetokea Japan na PhD yake.

2.Freight/Cargo/Mazao yetu kuwa + kufika salama huko yaendako

3.Uhakika wa mawasiliano

Design Mbovu/Mbaya both in cost/benefit ni ile isiyo SAFE

Ukiangalia trend za ajali Tanzania utaona kuwa inapanda, sababu ni nyingi.

Zamani ajali zilikuwa chache labda kw akuw amagari yalikuwa machache lakini umakini ulikuwa Mkubwa....na hii ilitokana na kuwa suala la usafiri lilikuwa defined and controlled.......tulikuwa tukisafiri na warrant zetu enzi zile, ikifika katikati ya safari gari hubadilishwa na dereva pia, barabara zetu zilikuwa nyembamba zaidi but we managed....comparatively ukiangalia data za zetu za ajali kipindi hicho na nchi jirani we were better (im sorry sijaweza kukuwekea data hapa kutokana na matatizo ya kiufundi kwenye uploading), ma-area engineers wakati ule pamoja na landrover zao + bedfords na vile viji-force account walivyokuwa navyo kwa kweli walijitahidi sana kwenye suala la maintenance

siku hizi magari ni mengi, leseni hutolewa hovyo hovyo (nakumbuka zamani zile leseni ilitosha kabisa kuwa kama kitambulisho chako), siku hizi mtu mmoja anaendesha toka Dar mpaka Arusha/Mbeya/Singida.....you name it bila hata msaidizi/kupumzika (wengine huchukulia eti kusimama na kula njiani ndio mapumziko yenyewe......duuhh (ndio UCHOVU wenyewe), Siku hizi maintenance be it kwenye magari tunayotembelea or ktk barabara zetu.....yaani we just take things for granted....i.e. a lot of MAYBEs and POSTPONEs to our maintenance activities, mtu ukiambiwa badilisha tyres/shockups/rod ends unadharau, Driving Schools ndio Balaa, watu barabarani hawaheshimiani Kila mtu mbabe........

Kama maelezo ya Engineer kuhusu timings za safari ya Mheshimiwa ni sahihi basi UCHOVU itakuwa ni a definite factor, ukiwa mchovu hata akili ya kufikiri kuwa wapi ni sahihi ku-overtake....INAPOTEA trust me.....
 
Mkuu Mwakaleli,

Nimependa hii ya consultancy services vijijini. Kama unaweza naomba niandikie zaidi kidogo hata kupitia PM yangu juu ya zina include vitu gani? Huenda kuna mambo ambayo unafanya ambayo na wengine tunaweza kujifunza/kufaidika au kusaidiana. Kuna mambo mengi sana huko vijijini yakifanywa inavyotakiwa, kuna weza kuwa na impact kubwa kwa wananchi wa kawaida.

Kazi njema.
Mtanzania usijali mkuu nitakushirikisha vingi katika hii shughuli ya consultancy services ni mambo ya technical evaluation za mambo ya barabara na madaraja, design za water supply, design and supervision of civil works( barabara, madaraja na maji) pamoja na design and supervision of building works abazo zinahusika zaidi na majengo, mambo ya test za udongo( geotechnical investigation) na masuala mengine yanayohusiana na mambo ya consultancy katika mambo ya ujenzi(preparation of contract document and tender document). Ndugu yangu nitakuhabarisha zaidi nikirudi tz mwanzoni mwa mwezi ujao.
 
...Hiyo barabara ya Iringa Mbeya kidogo mimi iniweke chini. Kuna dereva ambaye siku zote namtumia, alikuwa na tender nzuri zaidi, akaona kuiachia kwa safari za wiki mbili haitakuwa vizuri. Nikamwelewa na akanitafutia dereva mwingine; njiani nikawa namwambia hii barabara mbaya punguza mwendo. Akawa anapunguza kisha anarudi pale pale, ilifika mahali nikachoka na kumwacha. Ghafla mwendesha...

Mtanzania,
Utachokaje kumsihi dereva wako awe mwangalifu? Maisha yako unayaacha mikononi mwa reckless driver umechoka? Kumbe ndio maana wenzetu walishaona kila mtu ajiendeshe mwenyewe, unless u're vice president.
 
.......Sijui nini kifanyike lakini mimi nina wasiwasi kweli na hizo barabara zetu.

Mkuu Mtanzania,

Trust me barabara zetu nyingi, as they stand are MONSTERS ready to kill...any time kwa yeyote yule ambaye ni makini na ambao si makini...the reason behind being

1. Maintenance issues.........it wil be very lucky ku-find barabara inayo-receive timely mtce...na hata zinapo receive hizo mtce.......traffic management facities kwenye sehemu hizo HAKUNA.......imagine Mtce engineer ana-send crew yake ku-deal na let say potholes......wale vibarua watachimba chimba na kuacha lile shimo unattended....i.e without any traffic control measures......one would ask really....why would someone go there in the first place......to make things worse wakti mwingine wana-spray lami...yaani wee acha tu.....in shor tuna tatizo kubwa kwenye mtce
NOTE: mtce si kuziba mashimo peke yake, hata traffic sign posts inabidi ziwe replaced pale zinapokuwa vandalised....usiniulize utazuiaje vandalism.....lol

2. Nafikri Design zetu wakati mwingine zinatakiwa ziwe assessed baada ya kipindi fulani kuangalia kama zina-meet demands/requirements/standards/safety issues.........sina uhakika kama hayo mambo yanafanyika......nasema hivyo kwa sababu miji yetu siku hizi inakuwa haraka sana nahivyo travel parttens zinabadilika

3. Enforcement ni tatizo nalo.....pengine sheria zetu zinahitaji kuangaliwa upya........

4. Public awareness........ni hatua gani serikali inachukua kuelimisha wananchi juu ya matumizi bora na salama ya barabara

well nafikir Morani75 na Fundi Mchundo watakuw ana mengi ya kuelezea ju ya hilo
 
Ninachoshangaa ni jinsi watu wanavyozungumzia matatizo ya barabara na ubaya wake kana kwamba hao wanaotunga sheria, kusimamia fedha za umma na ambao wanakuja kwenye misiba ya wahanga wa ajali na kuwatembelea majeruhi, wao wanapita angani!


Mnachotegemea ni kuwa mkiimba wimbo mzuri, na kuongeza ala na vibwagizo basi mbuzi atacheza! kwenye suala la barabara na mambo ya ajali hakuna kipya ambacho hawakijui. NONE. Kwani mmeshasahau mwaka huu ulivyoanza?
 
Ninachoshangaa ni jinsi watu wanavyozungumzia matatizo ya barabara na ubaya wake kana kwamba hao wanaotunga sheria, kusimamia fedha za umma na ambao wanakuja kwenye misiba ya wahanga wa ajali na kuwatembelea majeruhi, wao wanapita angani!


Mnachotegemea ni kuwa mkiimba wimbo mzuri, na kuongeza ala na vibwagizo basi mbuzi atacheza! kwenye suala la barabara na mambo ya ajali hakuna kipya ambacho hawakijui. NONE. Kwani mmeshasahau mwaka huu ulivyoanza?

........si vibaya kuwakumbusha
 
Mkuu Mtanzania,

Trust me barabara zetu nyingi, as they stand are MONSTERS ready to kill...any time kwa yeyote yule ambaye ni makini na ambao si makini...the reason behind being

1. Maintenance issues.........it wil be very lucky ku-find barabara inayo-receive timely mtce...na hata zinapo receive hizo mtce.......traffic management facities kwenye sehemu hizo HAKUNA.......imagine Mtce engineer ana-send crew yake ku-deal na let say potholes......wale vibarua watachimba chimba na kuacha lile shimo unattended....i.e without any traffic control measures......one would ask really....why would someone go there in the first place......to make things worse wakti mwingine wana-spray lami...yaani wee acha tu.....in shor tuna tatizo kubwa kwenye mtce
NOTE: mtce si kuziba mashimo peke yake, hata traffic sign posts inabidi ziwe replaced pale zinapokuwa vandalised....usiniulize utazuiaje vandalism.....lol

2. Nafikri Design zetu wakati mwingine zinatakiwa ziwe assessed baada ya kipindi fulani kuangalia kama zina-meet demands/requirements/standards/safety issues.........sina uhakika kama hayo mambo yanafanyika......nasema hivyo kwa sababu miji yetu siku hizi inakuwa haraka sana nahivyo travel parttens zinabadilika

3. Enforcement ni tatizo nalo.....pengine sheria zetu zinahitaji kuangaliwa upya........

4. Public awareness........ni hatua gani serikali inachukua kuelimisha wananchi juu ya matumizi bora na salama ya barabara

well nafikir Morani75 na Fundi Mchundo watakuw ana mengi ya kuelezea ju ya hilo
Ndugu yangu barabara zetu nyingi, zilizojengwa zamani zile hazina standard zinazokubalika kwa sasa. design life ya barabara ya lami ni miaka ishirini pia inatakiwa iwe inapata matengenezo ya mara kwa mara lakini ni bahati mbaya hizi barabara zetu huwa hazifiki hiyo miaka ishirini kwa sababu hazipati matengenezo ya mara kwa mara. standard ya highway carriage way(sehemu ya kupita magari) inatakiwa iwe na upana wa mita saba nakila bega (shoulder) inatakiwa iwe na upana wa mita moja na nusu. lakini ukiangalia leo hii barabara ya Dar Mbeya hasa maeneo ya iringa hazo hizo shoulders hazionekani, mashimo kibao, corrugations na ruts ndiyo usiseme kabisa yaani ni hatari tupu. Hata design life ya hiyo barabara ilishapita muda mrefu na wanachofanya sasa hivi ni kuweka patch kibao ambazo pia zinachangia zaidi kuharibika kwa barabara.
Barabara zetu nyingi design zake zinawabagua watembea kwa miguu na watumia baiskeli hakuna sehemu za kupita watu wa namna hiyo wakati nao kodi zao zinajenga hizi barabara, ambapo hilo ni tatizo kubwa inabidi tuzingatie pia route za watembea kwa miguu na wa baiskeli. ukienda moshi unaweza toa machozi. barabara inayokwenda KCM toka mjini haina shoulder kabisa mie huwa najiuliza hawa waliodesign hii barabara walikuwa wanafikiria nini sijui ,sasa hivi watu wanapita katikati ya barabara.
Pia barabara zetu nyingi hazina alama za barabarani ambazo zinasaidia kutoa tahadhari, wakati mwingine wananchi huzing'oa hizo alama na kwenda kujengea vyoo na kutengenezea mipini ya mashoka na majembe. watu wanaelimishwa sana lakini hawaelewi. wakati mwingiine hung'oa hata bomba za kwenye madaraja ambazo ni muhimu sana. yaani utafikiri watu tumelogwa yaani kazi ipo.
 
ya nini? hujiamini, huamini ulichoandika, hujui matumizi ya hilo neno.

- Nimelikoroga na sasa nataka kulinywa, sema tatizo lako acha kuzunguka mbuyu, lets cut the slacks now and get on the business unayoijua better! Bwa! ha! ha! ha!, au?

- Wewe hujamaliza mimi ndio kwanza nimeanza! Bwa! ha! ha!

Respect.

FMES
 
Ogah,
Mkuu wangu nadhani hapa kidogo hatukuelewana. Unapofikia Ku diesign kitu ina maana tayari una matumizi yake.. Hiyo safety ni kati ya vitu vinavyoambatana na muundo wa kitu hicho iwe hata gari au shati la kuvaa. sababu kubwa ya kutengeneza gari ni kurahisisha Usafiri, na katika kurahisisha usafiri huo unatazama kwanza faida zake kiuchumi na maendeleo ya jamii..

Hivyo fikra ya kwanza ktk maendeleo ya nchi au hata mtu binafsi ni Umuhimu wa kuendelea, kujijenga kiuchumi na kuweka mapango madhubuti wa vyanzo vya kukuwezesha kufanikiwa..Na mara zote vyanzo hivi (miundombinu) ni long term strategy inayotazama kukuza uchumi wa nchi na ndicho nachozungumzia..
Barabara ya Kwenda Iringa, Mwanza, au hata Arusha ni barabara zinazojengwa/kukarabatiwa kwa sababu wananchi wanalalamika au matokeo ya vifo na kadhalika ndizo sababu zinazowasukuma serikali kuweka safety badala ya kutazama malengo ya barabara hizo kwanza..
Ukitazama barabara zote hizi vimejengwa bila plan ya miaka mingi na hasa tukilenga kukuza uchumi wetu kwani mara zote barabara zetu zina mapungufu ya safety kwa sababu tunatazama karibu matumizi tofauti ya barabara hizo.. Kila Highway nchini ina lane moja au mbili at the maximum na zote zinapita katikati ya vijiji au kando ya mji mkuu..meaning kila Freeway inapokaribia mjini hugeuka na kuwa barabara ndogo yenye traffic lights..Na ndio maana sikuona ajabu Mtanzania aliposema kuna mtu akiendesha baiskeli alikatiza..
Hivyo hata kama barabara hizi zimejengwa kwa alama za kutosha, lami, sheria na kila pambo linaloweza kupendeza, hiyo safety haiwezi kuwepo kwa sababu tunajenga mabarabara haya pasipo sababu ya maana kiuchumi. Hivyo sii tu tunaongeza ajali bali pia hatujengi miundombinu imara kwa malengo marefu ya matumizi yake kulingana na ukuaji wa uchumi tunaotegemea..

Trust me mkuu wangu hata hao watengeneza magari hutazama mahitaji ya gari ktk Usafiri unaokusudia kujenga Uchumi wa shirika husika mbele ya Quality (safety, mahitaji ya nguvu ya gari hilo, matumizi ya mafuta, na kadhalika) na ndio maana kila shirika la kutengeneza magari huwa na viwango tofauti na shirika jingine..Kitu muhimu ni kuhakikisha vina pass viwango vya standard vilivyowekwa.. Sasa kama watu tungekuwa tunapanda magari au kutengeneza magari kwa sababu ya safety, trust me by now labda magari yote yangekuwa kind of robotic engineered...
Sasa nachojaribu kusema hapa ni kwamba inatakiwa sana sisi tufikirie umuhimu wa barabara kiuchumi.. Kumwezesha wasafri, mizigo, na mazao wafike haraka, salama na katika wakati unaohitajika bila kusababisha machafuzi ktk mazingira.Barabara kuu za Mbeya, Songea, Moshi, Tanga na Kigoma, Mwanza na pengine mikoa yote zinatakiwa zijengwe na plan ya miaka kama 50 ijayo kulingana na shria za ujenzi wa Highway. Na sababu kubwa inayotanguliza ni kuunganisha sehemu hizi ili kuweza chumi za sehemu hizi kukua kiharaka... safety itakuwepo tu kwani hii ni sheria ambayo hutungwa bila gharama kubwa lakini sii ujenzi wa barabara..
Leo hii ukitaka kupanua barabara kuu yoyote ile unalazimika kuhamisha watu waliojenga kando ya barabara hizi lakini badala ya kufanya hivyo serikali yetu ikiwa ni pamoja na halmashauri za miji huweka bumps barabarani, traffic lights na kadhalika wakati hii barabara inatakiwa kuwa Freeway..haisaidii kitu kwani ajali bado zinatokea kwa wenda miguu!


Hizo barabara za Mbeya, Mwanza na hata Moshi zingejengwa kama Highway zinavyotakiwa kuwa kwa jina la Freeway..safety ingekuwepo kwani mara zote ujenzi wa Highway una viwango vyake ambavyo vinaleta hizo safety tofauti na barabara ndogo za mtaani..
 
Ndugu yangu barabara zetu nyingi, zilizojengwa zamani zile hazina standard zinazokubalika kwa sasa. design life ya barabara ya lami ni miaka ishirini pia inatakiwa iwe inapata matengenezo ya mara kwa mara lakini ni bahati mbaya hizi barabara zetu huwa hazifiki hiyo miaka ishirini kwa sababu hazipati matengenezo ya mara kwa mara. standard ya highway carriage way(sehemu ya kupita magari) inatakiwa iwe na upana wa mita saba nakila bega (shoulder) inatakiwa iwe na upana wa mita moja na nusu. lakini ukiangalia leo hii barabara ya Dar Mbeya hasa maeneo ya iringa hazo hizo shoulders hazionekani, mashimo kibao, corrugations na ruts ndiyo usiseme kabisa yaani ni hatari tupu. Hata design life ya hiyo barabara ilishapita muda mrefu na wanachofanya sasa hivi ni kuweka patch kibao ambazo pia zinachangia zaidi kuharibika kwa barabara.
Barabara zetu nyingi design zake zinawabagua watembea kwa miguu na watumia baiskeli hakuna sehemu za kupita watu wa namna hiyo wakati nao kodi zao zinajenga hizi barabara, ambapo hilo ni tatizo kubwa inabidi tuzingatie pia route za watembea kwa miguu na wa baiskeli. ukienda moshi unaweza toa machozi. barabara inayokwenda KCM toka mjini haina shoulder kabisa mie huwa najiuliza hawa waliodesign hii barabara walikuwa wanafikiria nini sijui ,sasa hivi watu wanapita katikati ya barabara.
Pia barabara zetu nyingi hazina alama za barabarani ambazo zinasaidia kutoa tahadhari, wakati mwingine wananchi huzing'oa hizo alama na kwenda kujengea vyoo na kutengenezea mipini ya mashoka na majembe. watu wanaelimishwa sana lakini hawaelewi. wakati mwingiine hung'oa hata bomba za kwenye madaraja ambazo ni muhimu sana. yaani utafikiri watu tumelogwa yaani kazi ipo.

mbali ya kuzungumzia Non Motorised Transport.....nafikri mengine uliyoandika ndio ambayo nimeelezea nikiwa najaribu kutoa mapendekezo...

Mkuu Mwakalele nini kifanyike ili tumuondoe hofu "Mtanzania" barabarani?
 
Back
Top Bottom