Ajali mbaya leo asubuhi Dar es salaam

Ajali mbaya leo asubuhi Dar es salaam

Jamaa alikua ametoka kwa mshkaji wke maeneo y kunduchi anafanya stanbic headoffice so sad
attachment.php

Kwani hufahamu ana maana gani?

Basi yaishe lakini muwe na huruma na uendeshaji wenu,
kwani tunaambiwa alichomekewa na ili kunusuru maisha ya wengine akachepuka pembeni, mtaro ndio ukambeba na milango haikufunguka hapo huoni hata magari yana makosa kiji-lock?
 
Ajali,bodaboda,majambazi,ebola,kulogwa!ukimwi,malaria.na yote hayo yakitokea umepatta janga hospitali hakuna dawa.vijana wa kova nao wanataka chao kuandika sick sheet.unaweza kuporwa hata kupigwa risasi na majambazi ukienda polisi wanataka petroli au chai wakamtafute muhalifu.
kuna haja gani ya kuwa mzalendo????
hapo sijaweka mgao wa Maji na umeme!
 
Mkuu umenena ila cha ajabu mara nyingi haya majanga yanatufuata sie wadhurumiwa tu, hata vifo wanaokufa sana ni wale waungwana, yenyewe yanapeta tu.

Wenzenu wana akili wanazingatia sheria za barabara upasavyo kuepuka kukatisha maisha ili wafaidi Mali walizofisidi.
pale panaonesha speed 60 we unatembea 120 kichwani kuna funza au tope?
aliyejenga kakuwekea alama nyingi kuku linda mtumiaji wa barabara! lakini vijana wengi tunajifanya ujuaji haswa na vibabe walkers vyetu!
 
Kwa comment nyingi hapo juu mwanangu mdogo <5yrs angesema "Pumbafu alah!", watu hatukuwepo hatuji kilichojiri, na wala hatujui huyo dereva alikuwa anakimbilia wapi lakini sisi tunatoa hukumu na maneno ya kejeli. Kumbuka ajali haina kinga jamani ingawa tunatikiwa tuchukue tahadhari, pia kumbuka waweza kuta ni jamaa yako halafu umeishabwabwaja maneno kama ya baadhi ya comments hapo juu.

Hata kama ni jamaa yangu akiwa mpuzi asiambiwe? Unapowekewa alama na sheria za barabarani lazima uzingatie! Haijalishi na haraka zako bado sheria ziko pale pale period!
 
attachment.php



Basi yaishe lakini muwe na huruma na uendeshaji wenu,
kwani tunaambiwa alichomekewa na ili kunusuru maisha ya wengine akachepuka pembeni, mtaro ndio ukambeba na milango haikufunguka hapo huoni hata magari yana makosa kiji-lock?

Hey hey za ujana hizo! usikute ni altezza hiyo! kapiga kitabu weee sasa maisha kayapatia kazi nzuri kaondoka kwa shemeji, kapanga sinza, mkopo wa gari lol, demu mkali, humwambii kitu!
Mjanja yeye!
 
Utawaweza wabongo, sehemu aliopata ajali ni mbaya sana, na ikumbukwe kuwa ni highway , aliyekuwa na makosa ni yule aliyeingia kutoka salasala bila kuangalia huyu aliyekuwa highway akitokea bagamoyo.

Hata yeye ana makosa eneo lile kuna kibao cha speed 60! kwa sababu ya tahadhari kama hizo za kwenye makutano! Sasa kama alikua anaenda 80 au 120 tutarajie nini?
 
Tatizo kubwa ni mijitu inayo elekea mwenge ikishaweka mafuta apo Total basi wanaona taabu kurudi mbuyuni, wanalazimisha kuchepuka apo kwenye T junction, alafu wanajiona wajanja/wabunifu fulani hivi kumbe.... likewise, at the Mwenge round-about, some MFs play crazy games to get to the service road by the oilcom garage. We have to change!
 
Msilaumu sana eti dereva alikuwa mlevi. Kwa mwendo kasi inawezekana na inapotokea dalili ya ajali kila dereva ana panic na kuchukua maamuzi ya haraka. Na kila amuzi la haraka lina matokeo yake kulingana na mhusika alivyo sharp kupata the best or the worst quick option. Hakuna kulaumiana hapa hasa kama wewe ni dereva. Rest in Peace ndugu.

Dereva kama si mlevi mshamba, kama si mshamba mjinga kama si mjinga basi lena mbaya!
Akome huko aliko! Dar ukitaka uishi usizidi speed 60! Unakimbiiiiiiiiiia jiulize, ikitokea rabsha utajiokoaje?

Halafu nyi mnaotumia barabara hii ya Bagamoyo kipande cha Mwenge hadi Tegeta nawaangaliaga tu!


Kipya kinyemi ooooohhhooooooo! Mtaanza kutujazia mituta buuuuuuuure!
 
Jamaa kaisha kwa moto mpaka kichwa kimepasuka,nimeshuhudia pia wakati inawaka mpaka ilipozimwa. So sad


Hii ajali mbona inaonekana kama kagongwa kwa nyuma? labda pia kupasuka kichwa ni kutokana na impact ya ajali, je kulikua na sign zozote kuonyesha marehemu alikua hai wakati moto una waka? ina sikitisha sana R.I.P.
 
Hii ajali mbona inaonekana kama kagongwa kwa nyuma? labda pia kupasuka kichwa ni kutokana na impact ya ajali, je kulikua na sign zozote kuonyesha marehemu alikua hai wakati moto una waka? ina sikitisha sana R.I.P.

Signs zipi zingekujulisha kuwa alikua hai wakati anaungua??
Fuvu lilikuwapo hapo kwenye kiti chake na namna gari ilivokaa asingeweza fungua mlango wake hata kama alikua hai.
 
amevuna alichopanda unaenda mwendo wa kasi wa nn wakati gari ni mali yako
na wanaokufa usingizini huwa na kasi? Watakuja watu baadae watatuambia kifo hupangwa na mungu na wakati huo huo wakimlaumu dereva sisi wanaadamu sisi tuna shida sana mkuu.
 
Hata yeye ana makosa eneo lile kuna kibao cha speed 60! kwa sababu ya tahadhari kama hizo za kwenye makutano! Sasa kama alikua anaenda 80 au 120 tutarajie nini?
Lakini ukiangalia hii barabara ilivyojengwa kuna kasoro kubwa na hili swali limewahi kujadiliwa hapa jf.
ukihesabu rate ya ajali kwa muda mfupi ilioanza kutumika ni wazi ikitumika miaka 10 waathirika watakuwa wengi pia.
Chukulia mfano kwenye barabara za kuingia au kutoka main road, hazina kibarabara cha kutokea hivyo ukipunguza mwendo kutoka aliyeko nyuma yako kama si mwelewa anakugonga au unataka kuingia barabara kuu sana sana utaangalia kulia na sio rahisi kujua kushoto kuna nini.
ukiangalia michoro kama ya Mandela rd au Pugu rd za architectures wa zamani ni bora kuliko hawa wa sasa hivi wakati ilipaswa kuwa visvesa!

Kidogo hapa angalia hii idea japo imechora kienyeji.
rd.jpg
 
Hey hey za ujana hizo! usikute ni altezza hiyo! kapiga kitabu weee sasa maisha kayapatia kazi nzuri kaondoka kwa shemeji, kapanga sinza, mkopo wa gari lol, demu mkali, humwambii kitu!
Mjanja yeye!
Post nyingine bwana, utadhani haijaandikwa na mtu mwenye akili timilifu.
 
Back
Top Bottom