Ajali mbaya leo asubuhi Dar es salaam

Ajali mbaya leo asubuhi Dar es salaam

Ajali mbaya imetokea leo asubuhi baada ya gari ndogo kuhama njia na kutumbukia kwenye mtaro na kisha kuwaka moto na kuteketea maeneo ya kati ya Africana na Mbuyuni(Bagamoyo road).

Ndani ya gari kulikua na mtu mmoja tu, inasemekana dereva alikuwa katika mwendo kasi kisha kwa mbele ikatokea gari nyingine ambayo ilikuwa ikivuka kuenda upande wa pili (Mwenge) hapo ndio dereva wa hili gari katika kufanya juhudi za kukwepa akaingia mtaroni na baada ya muda gari ikalipuka kwa moto na kuteketea yote.

Mungu ampumzishe kwa Amani.

Chanzo: Mimi na Baadhi ya mashuhuda.
Kwanini tuangamie? soma hapa

 
R.I.P ndugu jamani nduguzanguni tupunguze mwendo kasi ni hatri kwamaisha ya vijana nyakati hizi nimepoteza close friend's wawili in one week ajili ya speed
 
Dah!RIP maranyingi ajali za aina hii kwa weend husababishwa na ulevi.

Hayo ndo matunda ya barabara kuwa nzuri kwa vijana kati ya 20 - 35 years. Akiendesha gari au pikipiki utadhani anakwenda Mwanza kumbe Kunduchi tu. Ni ulimbukeni wa vijana

Poleni sana wafiwa and may his soul R.I.P

Jamaa kaisha kwa moto mpaka kichwa kimepasuka,nimeshuhudia pia wakati inawaka mpaka ilipozimwa. So sad

Barabara haina mbwembwe vijana

Ni kweli ya kusikitisha lakini hao moto chini na moto bati ni wapo wengi hao na sijui hawa wanajiamini kivipi au roho zinauzwa madukani ndo kujiamini hivo tena kila siku hayo hayo tuu

Msilaumu sana eti dereva alikuwa mlevi. Kwa mwendo kasi inawezekana na inapotokea dalili ya ajali kila dereva ana panic na kuchukua maamuzi ya haraka. Na kila amuzi la haraka lina matokeo yake kulingana na mhusika alivyo sharp kupata the best or the worst quick option. Hakuna kulaumiana hapa hasa kama wewe ni dereva. Rest in Peace ndugu.

Ajali hiyo mmmmh

R.I.P dereva wa mwendo kasi

Amevuna alichopanda unaenda mwendo wa kasi wa nn wakati gari ni mali yako

Duh,kweli katangulia huyo ...madreva jamani ni bora uchelewe kazini lakini ujari uhai wako vinginevyo utakufa na kuacha simanzi kwa jamaa

RIP dereva. Daah ila hii njia inaita sana asee. yaani kila ukikanyagia waona kama gari haiendi hasa pale bondeni.

ila mm nawachukiaga wale wanaowachomekeaga wenzaoo.......
Suluhisho pekee la ajari liko hapa
 
Khaa!! Kumbe JF hapa wengi akili zao za kushikiwa. Mnapewa picha na vimaneno kidogo tu basi mnatoa hukumu. Mungu awasamehe kisha awajaze busara japo kidogo.
 
Hayo ndo matunda ya barabara kuwa nzuri kwa vijana kati ya 20 - 35 years. Akiendesha gari au pikipiki utadhani anakwenda Mwanza kumbe Kunduchi tu. Ni ulimbukeni wa vijana
thou its nt gud to blame the dead body but i do agree with u
 
RIP....huwa sipendi madereva wanaochomekea na wale wanaolazimisha MTU uongeze mwendo...
 
Hayo ndo matunda ya barabara kuwa nzuri kwa vijana kati ya 20 - 35 years. Akiendesha gari au pikipiki utadhani anakwenda Mwanza kumbe Kunduchi tu. Ni ulimbukeni wa vijana

MIDFIELD Ndiyo Maana NAKUKUBALI Sana Na Mno Na Hiyo Picha Ya AVATAR Yako Ndiyo INANIPA RAHA ZAIDI.
 
Msilaumu sana eti dereva alikuwa mlevi. Kwa mwendo kasi inawezekana na inapotokea dalili ya ajali kila dereva ana panic na kuchukua maamuzi ya haraka. Na kila amuzi la haraka lina matokeo yake kulingana na mhusika alivyo sharp kupata the best or the worst quick option. Hakuna kulaumiana hapa hasa kama wewe ni dereva. Rest in Peace ndugu.

Utawaweza wabongo, sehemu aliopata ajali ni mbaya sana, na ikumbukwe kuwa ni highway , aliyekuwa na makosa ni yule aliyeingia kutoka salasala bila kuangalia huyu aliyekuwa highway akitokea bagamoyo.
 
Khaa!! Kumbe JF hapa wengi akili zao za kushikiwa. Mnapewa picha na vimaneno kidogo tu basi mnatoa hukumu. Mungu awasamehe kisha awajaze busara japo kidogo.

Wewe Yako Mbovu UMEKOPESHWA na Nani?
 
Utawaweza wabongo, sehemu aliopata ajali ni mbaya sana, na ikumbukwe kuwa ni highway , aliyekuwa na makosa ni yule aliyeingia kutoka salasala bila kuangalia huyu aliyekuwa highway akitokea bagamoyo.

Lakini aliyefariki je, ni nani? Lesson number one: Kuwa highway sio tiketi ya kuendesha gari kwa mwendo mkali kwani likitokea jambo lolote itakuwa vigumu kujikinga.
 
Back
Top Bottom