MGANYIZI john
New Member
- May 4, 2014
- 4
- 0
Poleni wahanga wote wa ajali hii.Mungu atatuvusha salama huu ni upepo tu wa uchaguzi.
hivi chanzo haswa cha ajali kufululiza ni nini haswa
kwa hiyo gari zinazo ovatekiwa 3 na zinazo ovateki
3 pamoja na ya huyo anayepiga picha maana ukiangalia utaona yupo upande ambao si wake
poleni wafiwa.Maombi nayo muhimu,Maana shetani ni muuaji.
Serikali haikutakiwa kusalimu amri kwa madereva na wenye mabasi krahisi .
Kova kusema "Madereva Hoyeee" Ubungo amekosea sana!.
Hakupaswa kuwafagillia. Eti hakuna tochi tena kwamaderva/ mabasi wala...... Amefanya kisiasa zaidi
Naisikitikia nchi yangu. Hili lawezekana TZ tuu!
Sawa asante sana. Sikuwa na muda wa kupiga picha ila nilifanya kazi ya kutoa taarifa husika sehemu sahihi na ndio maana polisi na ambulance walifika na kutoa msaada, we unaongea kwakuwa una bundle ila mie ndio nimetoka hosp muda huu saa 4. Ila asante sana kwa mtazamo wako. Kuona picha za watu waliojeruhiwa ndio furaha yako! Well umejiuliza hao majeruhi wametokaje hapo na kufika hosp? Umeona picha ya watu wawili, mbona unajiaminisha rafiki? Mtu kulala chini ni amekufa? Nikwambie nimetoka hosp na nimefanya jitihada nyingi tu ambazo sihitaji kujitangaza ila Mungu anajua. Sio kila hero unamjua, kuna watu ambao wapo wanamchango mkubwa tu na hawafahamiki na hao ndio wanamake change. Haya asante sana kwa mtazamo wako. Nikutakie usk mwema
Ile ajalii ya Majinja ilikuwa sehemu yenye mahandaki kwa hiyo hata hilo sidhani kama ni suluhisho mkuu.Hapa dawa ni kuacha mashimo barabarani ili mabasi yapunguze mwendo kipande Dar..Moro siku mbili hiviii..
Basi la kampuni ya Jordan limepinduka na kuua watu 8 Kilometa 6 kutoka mji wa Nzega.
Lilikuwa likitokea Mwanza kwenda Moshi.
Jembe chanzo cha ajali ni nini?
ujinga na upumbavu wetu wenyewe sisi wanadamu usitupeleke kuanza kumshutumu illuminati ( shetani ) kuwa yeye ndiyo chanzo cha mara kwa mara za hizi ajali. siyo kweli hata kidogo na nakupinga tena kwa 100%. shetani ndiyo anawaambia abiria " oya wewe dereva hebu nyoosha mguu wako bhana alah " au " dereva tukiwahi kufika tunakokwenda kuna zawadi yako hapa " au " dereva tuwahishe bhana kama huwezi sema tukusaidie " au " dereva usipowahi sikupi dada yangu au sikupi nanihiiii yangu tukifika ". kwa kauli kama hizi unadhani hatutajipanga kweli kila siku kununua majeneza ya mazishi ya wahanga wa hizi ajali.