Aisee utajiri sio kitu rahisi kumbe

Aisee utajiri sio kitu rahisi kumbe

Fene

JF-Expert Member
Joined
May 4, 2021
Posts
2,940
Reaction score
4,811
Yani najikuta nachimba sana na sometimes naona nimepata hela ya kutosha per day

Lakini nikiiweka mezani naona bado si kitu, akili inaniambia kwa hela hiyo bado huwezi hata kupata kiwanja town (sio kujenga)

Au hela Mazee imepungua thamani

Najikuta na grind sometimes lakini nikijaribu kufanya relevance ya mtonyo na materials world naona still, hadi najihisi kuchoka

1775410617455.jpg
 
Huwa ninapambana kwa juhudi nyingi nipate cha kunitosha, kile kinacho ongezeka kinakua ziada alihamdulillah lakini lengo si kutajirika, ikitokea mashaallah, ukipenda sana mali utajikuta unafanya mambo ya ajabu hata kuliwa utamu na wahuni.
Upo sahihi kwa upande fulani
Ila fahamu nguvu zinaenda na kuisha, kazi unafanya ila kuna kustaafu

Ila ukiwa na Uhuru wa fedha una nafasi nzuri zaidi ya Ku support famiy
 
Lengo sio utajiri, lengo ni financial freedom

Utajiri tunawaachia wao
Samahani, lakini huu mtazamo wa kitu kinaitwa financial freedom.!

Unajua ni umagharibi katika kufariji tabaka la kati la wafanyakazi

Binadamu akichoka kula kuku anatamani bata,tena mbuzi tena Ng'ombe anamaliza kwa ngamia anapohisi atajipata

Maana yake hakuna siku utakuwa free kila unapoongezeka na mahiji yanaongezeka

Financial freedom ni msemo wa vijana wanapojifunza kuwa Wazazi hakuna kitu kama hicho ukiyaelewa majukumu
 
Niliwahi kushika pesa yangu nyingi kabisa tangu nizaliwe na iliisha ndani ya siku mbili. Nakuelewa mzee.

Ila nipo free kiakili coz nililipa madeni pia.
 
Back
Top Bottom