Airtel: Kifurushi cha intaneti cha TSHS 2,500/-

Airtel: Kifurushi cha intaneti cha TSHS 2,500/-

hawana maisha mda c mda wataifuta! maana hiyo plan walio iandaa kutake over ukidial *154*44 si ya kishindani! wiz mtupu! goti offer nyingi ila on daily basis nao wanaboa! foda majeur hayo kwenye intenet offers
 
Wakuu si tuliambiwa kuwa ule mkongo wa mawasiliano utakuja kushusha gharama za mtandao wa mawasiliano na internet inakuwaje tena kila siku maumivu?!
 
kinyoba hizo ni bundle tofauti hii ilikuwa unatuma neno internet kwenda 15444
 
Last edited by a moderator:
Hata mimi nimepata huu ujumbe nangoja hii bundle iishe nione itakuaje!
 
washenzi mimi nilikua nakula kitu cha 400 sasa nawaza kusepa nishaurini niruke wapi
 
Acheni Hofu!

Hayo matangazo ya kwenye SMS ni uda mrefu sana sasasa wamekua wakiyatuma kwa wateja. Naamini ni njia mojawapo ya kuwapunguza wateja kutumia mtandao kwa muda mrefu(scare tactics) ili kuwafanya wengi wabaki within fair usage limit ambayo kwa ile 2500/400Mb ni ngumu kuifuata.

Wewe tuma Internet kwenda 15444 hata kesho itakupa 400Mb kama kadawia na inakaa mwezi mzima. Naitumi hiyo bundle kwenye modem na kwenye iPad na kote inapiga kazi hata sasa ninapoongea hapa.

Kufanya modem iwe fast:
Hii najua ni ngumu kwa wengi kuamini lakini kuna viujanja vidogo vidogo vya kufanya modem yako ya airtel iwe faster. Kwanza kabisa naanza kwa kusema kwamba kitu rahisi kabisa kutumia ni modem ya Vodafone kisha ndani weka laini ya Airtel. Kuitumia, wewe install ile software inayokuja na hiyo modem ya Vodacom kama kawaida kisha ikishamaliza weka laini yako ya Airtel, ukienda kwenye upande wa kulia chini ya display yako utaona kale kasehemu ambako huwa tunatumia kutafuta wireless networks, kuna moja itakua inaitwa Vodafone web sessions, ifungue hiyo itakuuliza Username, Password na Access Point Name, hizo username na password acha tupu, kwenye access point weka neno Internet. Ukifanya hivyo mara nyingi nimeona modem za vodafone(ZTE) zinakamata 3G kirahisi kuliko za Airtel(wamezibana wenyewe = FUP again).
Kama huna modem ya Voda, namna nyingine rahisi ni kuingia kwenye settings za hiyo hiyo modem ya Airtel na kutafuta settings za connection options, humo wewe uchague 3G tu itakua kwa maneno kama UMTS Only au HSPDA only ama HSUPA only ama hata 3G only. Uliishaiweka hiyo save settings kisha ichomoe na kuirudisha modem. Ukiona imewasha taa ya bluu inablink, jua unakula 3G na ni kwa spidi ya hatari, ukiona inawaka taa nyekundu tu, jua hilo eneo halina 3G rudi kwenye settings na urudishe Dual Mode.

Sina lugha rahisi ya kuelezea hili jambo ila in summary, limit your Airtel modem to 3G Only ama timua modem ya Voda/Tigo na laini ya Airtel.
 
Hawa airtel waongo sana mimi nimejiunga sasa hvi nimepata mb 400 hzo mb 200 sijapewa waongo sana hawa airtel.
 
Wameondoa kweli sasa mtandao gani mwingine sijui wa kukimbilia..

Kama upo maeneo yenye coverage ya TTCL nunua modem zao....kitu hybrid speed safi. Mimi natumia package ya BANJUKA kuanzia saa tatu usiku sh.300 kwa saa! Full kudownload!
 
Wakuu si tuliambiwa kuwa ule mkongo wa mawasiliano utakuja kushusha gharama za mtandao wa mawasiliano na internet inakuwaje tena kila siku maumivu?!

Mkuu mbona gharama zimeshuka sana, kumbuka nyuma tuliko toka.
 
Wajameni naombeni msaada, hivi hawa airtel ndo wameisha ifuta ile "bando" yetu ya shs. 2500? Nimejaribu kutumia ile njia ya kutuma sms kwenda 15444 inakataa, na ile ya *154*44# ndio kabisaa, ina nipeleka kwenye mahela mengi tu. Jamani airtel kulikoni?
 
TUMA SMS internet KWEND A 15444 PIA HAKIKISHA UNA ZAIDI YA 2,500
 
wameishusha lakini kutoka mb 400 hadi mb 250 kwa 2500 tuma neno internet kwenda namba 15444 wakikuzingua usijali subiri kisha tuma tena baadae hadi itakubali
 
wameishusha lakini kutoka mb 400 hadi mb 250 kwa 2500 tuma neno internet kwenda namba 15444 wakikuzingua usijali subiri kisha tuma tena baadae hadi itakubali
@mjoki mie walinitumia text, sio 250 tena ni 200 tu!
 
Back
Top Bottom