Watu waliopigana vita ya Badr wamesifiwa na Mwenyezi Mungu ndani ya Qur'an na mpaka leo hao watu wanaruzukiwa mpaka siku ya kiama. Vita ya Badr walipigana mpaka Malaika. Makafiri walikuwa wamekusudi kuufuta Uislaam, walikuwa jeshi kubwa la wapiganaji zaidi ya 1,500 wakiwa na tembo 300, ngamia na farasi jumla ya 700 wakati Jeshi la Waislaam likiongozwa na Mtume Muhammad saw, Wapiganaji 300 na farasi kama 50 na ngamia kadhaa ! Makafiri wangeshinda, basi Uislaam ungefutika, na Waislaam walishinda huku Makafiri wakishangaa kuona kinachotokea uwanja wa mapambano.