Ahadi ya Njia Nne Usagara – Mwanza Mjini (KM 25) Imefikia Wapi?

Ahadi ya Njia Nne Usagara – Mwanza Mjini (KM 25) Imefikia Wapi?

Dalton elijah

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2022
Posts
780
Reaction score
1,831
Mwaka jana, Serikali ya Tanzania ilitangaza mpango wa kujenga barabara ya Usagara – Mwanza Mjini (KM 25) kwa kiwango cha njia nne (dual carriageway) ili kupunguza msongamano na ajali zinazoendelea katika lango kuu la kuingia Jiji la Mwanza

Lakini leo, zaidi ya mwaka mmoja baadaye, wananchi wanauliza:
Mbona hatuoni maendeleo ya kile kilichoahidiwa?

Kupitia hotuba za bajeti na maelezo ya mipango ya maendeleo ya sekta ya ujenzi, kipande hiki kilitajwa kama sehemu ya kuboresha miundombinu ya Jiji la Mwanza linalokua kwa kasi.

Eneo la Usagara limekuwa:
Kitovu cha makazi mapya.
Njia kuu ya malori yanayoingia na kutoka Mwanza.
Sehemu yenye msongamano mkubwa nyakati za asubuhi na jioni.
Kwa mantiki ya mipango miji, upanuzi wa KM 25 kuwa njia nne ungekuwa suluhisho la muda mrefu.
 
Wakati wa kuzindua Uhenzi wa daraja la JPM, kuubganisha Mwanza na Sengerema, Rais wa wakati huo, aliahidi kuwa barabara hii ya njia nne itakamilika sambamba na daraja hilo.

Bajeti za wizara ya ujenzi kwa miaka yote tangu kifo cha mwendazake, zimekuwa zikieleza, kuanza kwa ujenzi huo lakini hakuna kitu hadi sasa.
 
Back
Top Bottom