Ah.. Sijui wenzangu...ila kwa sisi tuliowahi kutumia usafiri huu tuli-enjoy sana!!

i missed this!..sijapanda mpaka leo...nahisi mlikula happy sana wakubwa!..
 
Kamanda miye umekumbusha machungu na raha, machungu ni msiba wa baba yangu mdogo ambaye alikuw akifanya kazi stesheni Tabora, nilikuwa sipandi kajamba nani, nimeshuka sana daraja la pili, nilikuwa sijui kabisa adha za daraja la tatu wakati nikitoka Dar kwenda shule ya Uyui pale Tabora, raha nakumbuka nilipata mademu wawili mmoja wa Kigoma alikuwa akiitwa Kidifa.... sijui yuko wapi na mwingine Mchaga alikuwa akiitwa Haika.... hata huyu sijui yuko wapi. Treni ulikuwa bonge la usafari jamani.

1st class ilikuwa chumba wanakaa wangapi?
Mi nilikuwa naiogopa kwani walikuwa wakisema kuna wizi wa madirishani,na wezi wanapapenda kwani abiria katika chumba si wengi...
 
duh me kwa mara yakwanza nilpanda 2002,raha kweli tho ilikuwa third class mtoto niliona ka daraja la kwanza afu 2likuwa company kubwa!
 
Nakumbuka mkifika Korogwe mnabadilisha mabehewa yale ya kwenda tanga na ya kuelekea Moshi yanaunganishwa na kuendelea na safari!!

Mi nilipanda la Reli ya kati hadi Mwanza na ya Tazara nilifika Kapiri Mposhi..
 
mweeh enzi hizo nipo sangu secondary mbeya huko.
Nilikuwa bingwa wa kula nauli ya kupandia basi.
Shule ikifunga tunashinda disko mount au soweto complex unatumia nauli ya basi kesho mchana iyunga moja mmebakiwa na hela ya treni tu mnanunua karata mnachukua draft then mdogo mdogo mpk kitu mzizima kipind hcho tren mpk tanga na moshi,
Tren tena mpaka tanga kunani raha kwel humo ndan ni karata draft, kuku wa mrimba mweeh raha kwel kwel.
 
Halafu daraja la pili kunakuwa na aina mbili... "Second seating" na "Second sleeping"
 
mweeh enzi hizo nipo sangu secondary mbeya huko.
Nilikuwa bingwa wa kula nauli ya kupandia basi.
Shule ikifunga tunashinda disko mount au soweto complex unatumia nauli ya basi kesho mchana iyunga moja mmebakiwa na hela ya treni tu mnanunua karata mnachukua draft then mdogo mdogo mpk kitu mzizima.

Ha ha ha .... We ni kiboko Kapala...
 
Ni noma! hasa ukute behewa wamekata wajeda hukatishi kwenda behewa jingine, au mmetoka Mwz na kufika Tbr kumbe hilo behewa wamepangiwa Tbr boys mtapigwa mikanda hadi muhame
 
Kipind hicho ilikuwa inahusika, nan apande scandinavia atoe 8000 mpk chalinze au dar wakati tazara ni wewe na id yako.

Dah.. Si mchezo!

Kwenye TAZARA ukiwa unaenda,utashangaa watu wengine wanaongea Kiwemba(Bemba),baadaye Kiswahili kumbe kuna Wazambia kibao na Wabongo wanaoishi huku kwetu na kwao...

Halafu kuna mahali mnapita mchana,lakini kuna giza kama la dakika kumi hivi! Wala humuoni mwenzako! Waliowahi kutumia Tazara wanafahamu. Na ni full wanyama wa maporini.

Saa nyingine "pipa" wala hau-enjoy nature ya nchi yako..
 
Ni noma! hasa ukute behewa wamekata wajeda hukatishi kwenda behewa jingine, au mmetoka Mwz na kufika Tbr kumbe hilo behewa wamepangiwa Tbr boys mtapigwa mikanda hadi muhame

Ha ha ha... Ilikuwa raha... Wengine wanapotea,wanakuja kuonekana asubuhi kwenye mabehewa yao..
 
Na kweli ujasiriamali wa kipindi kile jamani,we acha tu!

I miss kile chombo kwa sana..

Mnakutana hadi watu mliopoteana muda mrefu,mnaungana hata na kufahamiana na watu wapya,it was fun pia..
Yaani raha nyingine mnapokutana lile la bara na la kutoka dar maeneo with majina ya shule yalivyobandikwa ubavuni na basi vifijo na kelele wapeleke wa bara hao !!
 
Yaani raha nyingine mnapokutana lile la bara na la kutoka dar maeneo with majina ya shule yalivyobandikwa ubavuni na basi vifijo na kelele wapeleke wa bara hao !!

Poa sana.. Basi tu siku hizi,si la ukweli kama zamani..
 
Dah ilikuwa raha sana sana, Reli ya kati nilishawahi panda na Tazara, mpaka pale Salanda aisee raha kweli na Dodoma unapita mida ya mchana mchana unachapa usingizi weeee mpaka unachoka mwenyewe!

Kiukweli, wanasiasa ndo wameharibu ladha zote za usafiri wa reli kwa lengo la kuhakikisha tumbo lao lina shibe ya kutosha!

LIMENIUMA SANA!
 
Usafiri wa treni...

Ah... Tuliowahi tukumbushane,mabehewa marefu kama nyoka,hekaheka za ma-TT, mambo ya "buffet car",enhe...

Tukumbushane jamani..
Dah umenikumbusha mbali sana....yan enzi zileeeee nasoma zangu Kigoma.....
 
Back
Top Bottom