Agano Jipya

Gamba,

Azimio la Arusha ni mali ya Taifa na si chama. Chama kilitumika kama chombo kutangaza na kulitekeleza.

Katiba na Sheria zote tunazo na tulizirithi kutoka kwa mkoloni na kwa kiasi kikubwa bado tunazitumia kama zilivyokuwa. Azimio ni Manifesto ya Taifa kuatika kulijenga Taifa letu.

Kwa nini nasema Azimio ni mali ya Taifa na si TANU au CCM? Ni kwa kuwa wakati wa mfumo wa chama kimoja, kila Mwananchi alikuwa ni lazima awe mwanachama wa TANU na hata CCM. Mashuleni, makazini, viwandani, biashara, mashambani, vijijini na mijini, kutokuwa mwanachama wa TANU au CCM ilikuwa ni usaliti kwa Taifa. Hivyo basi, kimsingi hata TANU na CCM ni mali za wananchi.

Kilichotungwa na TANU na kumilikiwa na TANU ni mali ya wananchi. Same goes with CCM. Yaliyoandikwa ndani ya Azimio si lazima yawe katika Katiba au kuundiwa sheria. Bali ni dira, mfano wa Ilani ya CCM ya Uchaguzi, Sera ya Chadema au Utajirisho wa UDP.

Hatuwezi kuendelea kudai eti Azimio ni maliya CCM na si ya Taifa. Kusema hivyo kuna maana kuwa kila kilichofanywa na CCM basi ni mali yao hivyo mwingine akiingia basi atengue kila kitu.

Naomba ulipitie Azimio tena ujisomee na utabaini kuwa Azimio, limetumia Katiba na Sheria zilizokuwepo wakati huo. Ukija kwenye suala la miiko ya uongozi, hata Sheira ilikuwa imelizungumzia hilo, ila tuu Azimio lilitoa msisitizo zaidi.

Sisi Wakristo, tuna Biblia, Amri Kumi, kisha tuna Sala ya Bwana na baadaye ni Imani ya Mitume. Kama Biblia ni Katiba, Amri Kumi (kumi na mbili)ni Sheria, Sala ya Bwana na Imani ya Mitume ndio Manifesto yetu na si lazima ibadilishwe kuwa sheria au katiba.
 
Kitila,

Si lazima kuleta mabadiliko tuwe wanachama wa CHADEMA pekee. Hata CUF, UDP au CCM tunaweza kuungana na kuleta mabadiliko.

Nitakuunga mkono wewe kama Kitila Mkumbo kwa maana nina imani utafanya kazi sahihi. Kukuunga mkono haina maana basi mimi sasa ni CHADEMA. Same goes na kumuunga kwangu mkono Mwakipesile RC wa Mbeya, Magufuli waziri na wachapa kazi wengine.

Utaifa wetu unatakiwa uimareke bila kuegemea chama fulani. Hii ndio nia yangu ya Agano Jipya. Tusirudie makosa ya CCM kuwa chama Hatamu kushika Utamu!

Hata nyinyi CHADEMA mkiingia, tutawaona kama CCM walivyo, hivyo kunahitajika taasisi huru isiyofungamana ili kuhakikisha kazi ya Kujenga Taifa inafanyika kwa manufaa ya Taifa na si CCM au CHADEMA!
 
Hii ni sehemu tu ya mahojiano ya Mwalimu na IB. unaweza kuyasoma yote hapa: MAHOJIANO NA MWALIMU

IB: Does the Arusha Declaration still stand up today?


MJN: I still travel around with it. I read it over and over to see what I would change. Maybe I would improve on the Kiswahili that was used but the Declaration is still valid: I would not change a thing. Tanzania had been independent for a short time before we began to see a growing gap between the haves and the have-nots in our country. A privileged group was emerging from the political leaders and bureaucrats who had been poor under colonial rule but were now beginning to use their positions in the Party and the Government to enrich themselves. This kind of development would alienate the leadership from the people. So we articulated a new national objective: we stressed that development is about all our people and not just a small and privileged minority.

The Arusha Declaration was what made Tanzania distinctly Tanzania. We stated what we stood for, we laid down a code of conduct for our leaders and we made an effort to achieve our goals. This was obvious to all, even if we made mistakes - and when one tries anything new and uncharted there are bound to be mistakes.

The Arusha Declaration and our democratic single-party system, together with our national language, Kiswahili, and a highly politicized and disciplined national army, transformed more than 126 different tribes into a cohesive and stable nation.

However, despite this achievement, they say we failed in Tanzania, that we floundered. But did we? We must say no. We can't deny everything we accomplished. There are some of my friends who we did not allow to get rich; now they are getting rich and they say `See, we are getting rich now, so you were wrong'. But what kind of answer is that?

The floundering of socialism has been global. This is what needs an explanation, not just the Tanzanian part of it. George Bernard Shaw, who was an atheist, said, `You cannot say Christianity has failed because it has never been tried.' It is the same with socialism: you cannot say it has failed because it has never been tried.

Asante sana Mwanakijiji kwa hii clip,

Katika moja ya madarasa niliyofanya hapa US niliwahi kumuuliza Mwl mmoja wa falsafa aliyekuwa anapondea nchi za kiafrika na ulaya mashariki kuwa ziko masikini kwa vile zilifuata sera na falsafa za kijamaa.

Nilimuliza swali kama Marekani au ulaya magharibi zilikuwa nchi za kijamaa au za kibepari kwa mtizamo wake. Kwa vile nilikuwa mmoja wa wanafunzi wakimya sana darasani, yule mwalimu alisita kidogo kabla ya kujibu swali langu. Baada ya kama sekunde 30 hivi akasema you know anhaa hooo, what was your question again?

Nikauliza the same question, kisha akajibu kuwa (baada ya kugundua mtego kwenye swali langu) hana uhakika kama Marekani na nchi za ulaya magharibi ni za kijamaa au kibepari.

Kitu kimoja nilichojifunza ni kuwa labels na majina vinasumbua watu wengi sana. Watu hawachukui muda kujifunza content ya kitu badala yake wakisikia tu ujamaa basi wao wanakimbilia kwenye socialism (anti-GOD0 bila kukumbuka kuwa Azimio la Arusha lilikuwa ni la ujamaa na kujitegemea. Neno la kujitegemea watu wengi sana Tanzania na nchi zingine walilisahau kabisaaaaaa
 
Rev. Kishoka,
Wanabodi wengi watatukumbuka sana toka Bsctimes tulipokuwa tukipiga makelele kuhusu Ujamaa - Azimio la ARUSHA kwa mazuri yake pamoja na kwamba kulikuwa na kasoro zake.
Nitarudia kusema kulikuwepo na mada hapa inayosema kitu kama :- Ili tuendelee Tanzania tunahitaji kufanya nini?...
Nakumbuka vizuri tulijaribu kuchangia mengi mazuri kisha kuna wakati niliomba mchango wa wengi nikiwa na haja kubwa ya kuorodhesha maoni ya watu na kutunga Azimio jipya (Agano jipya) lakini baada ya kwenda Tanzania Mwezi March hadi May nilirudi na kusema kuwa mawazo yetu yote hayawezi kufanya kazi ama kuleta mabadiliko hadi pale tutakapo weza komesha UHUJUMU UCHUMI....
Wapo ambao hawakuniamini kwa sababu tu hizi habari za BoT zilikuwa kapuni...tukaitwa majina ya Wapinzani na kadhalika kuwa kelele za mlangoni haziwezi kuwazuia kulala..
Leo hii zimeibuka na wao ndio wamekuwa Wapinzani!...The hunter amekuwa the hunted one, ule ule mchezo wa Predator na Pray, hivi sasa wanaanza kujikanyaga ovyo.

Kama ulivyosema mkuu wangu - Aluta continua tutaendelea kujenga hoja hata kama zinaonekana kuwa pingamizi kwa baadhi ya watu wasokuwa na upeo. Mantiki yake itakuja onekana na Mungu kuibariki Tanzania kwani hata Yesu mwenyewe ktk mafundisho yake zilipita karne tatu ndipo Biblia ilipokusanywa... aliondoka akiwa na wafuasi wachache sana pengine naweza sema 0.00000000001 yaani hapakuwa na posibility kabisa ya neno la Mungu kuweza kuenea duniani nzima.
 
Kitu kimoja nilichojifunza ni kuwa labels na majina vinasumbua watu wengi sana. Watu hawachukui muda kujifunza content ya kitu badala yake wakisikia tu ujamaa basi wao wanakimbilia kwenye socialism (anti-GOD0 bila kukumbuka kuwa Azimio la Arusha lilikuwa ni la ujamaa na kujitegemea. Neno la kujitegemea watu wengi sana Tanzania na nchi zingine walilisahau kabisaaaaaa

Thanx so much Mwafrika wa Kike kwa rise the very important issue! Ni problem - "Psychological association." Kwa kuwa ulivivyokuwa darasa la kwanza Ulichapwa na kuumizwa sana na Mwalimu aliyekuwa amevaa kaptula na soksi nyekundu. Unapokuwa mtu mzima unawachukia watu wote wenye kuvaa mavazi hayo. Bila hata wewe kujua unafanya hivyo. Kiukweli huwatendee haki. Kwenye basi/sherehe etc viti viwili vikiwa wazi unajikuta hukai kile jamaa aliyevaa kaptula na soki nyekundu.

PERSONALY MPAKA HIVI KARIBUNI NILIKUWA NA PHOBIA NA HII LABLE " AZIMIO LA ARUSHA, UJAMAA NA KUJITEGEMA, MAADUI WATATU..etc"

Lakini inabidi tuamke, tuende zaidi ya lables. Tuwe objective. Tukae chini tutulie tuangalie mambo kwa undani. uchunguzi wa kina unahitajika ili kupata ushindi na mwelekeo wenye tija dhidi ya ufisadi nk. Kuchukulia mambo juujuu tu si silaha kabisa.

Ndio maana nilifurahia hii thred ilikuwa inajadili maana ya Ujamaa ni nini? Kujitegemea nini? lakini naona haiendeleei. nilifikiri hapo pangeguwa pa zuri kwani hapakuwa na lable, itikadi, imani etc. http://www.jamboforums.com/showthread.php?t=8950.

Maana ukweli with a very deep and detailed analysisi Ujamaa wa Tz sio ule wa Urusi wa china..etc.

Maana kama alivyosema MW.Kike. Dhana ya "kujitegeea" ikifuatiliwa kwa undani kabisa na mapana yote itagundulika kuwa sio GODLESS. Hata hilo likishindikana kueleweka, Ukichukua dhana ya ujamaa nakujitegemea + wimbo wa taifa la TZ linalifanya Taifa hili tofauti na Wachina, warusi na wote Wasiomuabudu MUNGU. Utagundua pia kuwa Serekali ya Tanzania haina dini. Bali Watanzania wana dini. Ni "waumini Wa Mungu" kupitia dini zao na hata wale wasio na dini. Utaona wakati wa viaopo vya Viongozi Wa Taifa.
 
Rev.Kishoka,

..Maandiko ni tofauti kabisa na utekelezaji.

..Uongozi bora siyo umahiri wa kutoa maandiko/maazimio mazuri tu. Tunapaswa kwenda mbele na kuangalia mbinu za utekelezaji wa hayo maazimio tunayoandika.

..Watanzania tufike mahali tupime UONGOZI kwa REKODI YA UTENDAJI na siyo DHAMIRA NZURI ya maandiko ya viongozi.

..kila siku utasikia oooh Raisi ana nia nzuri lakini anashauriwa vibaya. Hivi mbona wenzetu wanachagua Maraisi wenye nia na washauri wazuri? Kinachotushinda Watanzania ni nini?
 
Rev.Kishoka,

..Maandiko ni tofauti kabisa na utekelezaji.

..Uongozi bora siyo umahiri wa kutoa maandiko/maazimio mazuri tu. Tunapaswa kwenda mbele na kuangalia mbinu za utekelezaji wa hayo maazimio tunayoandika.

..Watanzania tufike mahali tupime UONGOZI kwa REKODI YA UTENDAJI na siyo DHAMIRA NZURI ya maandiko ya viongozi.

..kila siku utasikia oooh Raisi ana nia nzuri lakini anashauriwa vibaya. Hivi mbona wenzetu wanachagua Maraisi wenye nia na washauri wazuri? Kinachotushinda Watanzania ni nini?

Joka,

Ndio maana nimeanzisha mjadala wa kudai Katiba mpya ambayo itawapa wananchi nguvu za kweli na uhuru na si mazingaombwe. Kushindwa kwa ufanisi kwa Serikali yetu kunatokana na Sheria na Katiba ambazo zinaipa Serikali nguvu na mamlaka ya kukataa kuhakikiwa na kuwajibishwa mpaka wakati wa Uchaguzi.

Mfano, mhimili wa Bunge, hauna nguvu za kutosha kutokana na Siasa kuwajibisha Mhimili wa Serikali. Mhimili wa Mahakama, hauna nguvu zaidi ya kutafsiri sheria lakini umejengwa kwa kutumia mwelekeo wa kisiasa na kuwa kigaragosi cha Serikali.

Katiba yetu inataja hii mihimili mitatu, Serikali Kuu, Bunge na Mahakama, lakini Serikali Kuu ina uhuru wa kuburuza mihimili mingine kwa kujinufaisha na kutimiza matakwa yake na si ya Wananchi, hivyo kufikia kulelea uzembe na kukosa ufanisi na uwajibikaji.

Ama Katiba yetu imeundiwa visheria ambavyo vinabana uhuru wa kukosoa na habari(freedom of opinion, freedom of press), kwa kutumia vitu kama sheria za usalama wa Taifa, dhihaka au kashfa kwa utukufu wa Raisi, na ujinga mwingi ambao hauna msingi.

Mtikila sasa hivi ana kesi ambayo Serikali inaishikilia bango kwa kumkasifu Raisi. Laiti kama nguvu na ufanisi wa kusikiliza kesi hii ya kijinga ungetumika kuwajibisha Serikali kwa matumizi mabaya ya fedha!

Bunge letu ambalo hupitia na kuidhinisha mipango na matumizi ya fedha halina nguvu ya kuletea Serikali tawala mgomo bila kugeuka kuwa chombo cha chama.

Moja ya mapendekezi ya Katiba yatakua ni kuondoa Watendaji kama Mawaziri kuwa wawakilishi wa majimbo(Wabunge). Mawaziri wawe watu huru ambao si Wabunge. Kuwepo na uhuru wa wagombea huru katika ngazi zote bila kuwa mwanachama wa chama fulani. Hili litasaidia ikiwa mwanachama wa chama fulani ambaye ni mbunge akiamua kuachana na hicho chama au kufukuzwa, haki yake ya kuchaguluiwa na wananchi kama Mbunge ibakie.

Kuna mengi ya kuhakikisha kuwa Serikali ni fanisi na kuwajibika, kinachohitajika ni kuunda mfumo huru na wa kweli utakao hakikisha hilo. Kama Watanzania wataafiki haya mabadiliko ambayo ni kwa faida ya taifa na maendeleo yao, basi haitatokea tena Raisi kuendelea kutoa ahadi hewa na kupitisha bajeti kila mwaka bila kushikiwa bango!

It can be done, play your part!
 
JokaKuu,
Maneno yako kweli kabisa inashangaza sana kuwa lawama zetu zinawaendelea washauri wa rais hali Rais huchaguliwa hata kabla hajapanga wala hatufahamu ni akina nani Washauri wake...Hadi leo hii hatufahamu isipokuwa tunakisia tu kuwa ubovu uko huko.
Nadhani hiki kijimila kinatokana na vitu kama vile mazoea yetu. Ktk ndoa huchagua mke/mme kutokana na hali ya Ukoo wake badala ya uzuri na uwezo wa mwanamke/mwanaume mwenyewe ktk ndoa.
 
Naomba nijirudi kutokana na majibu yangu kwa Gamba.

Azimio ni mali ya Taifa na si chama. Baada ya kutafakari kwa mara nyingine, nakubaliana nawe kimsingi kuwa malengo ya Azimio la Arusha hasa kuhusu maendeleo (watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora) azma ya kujenga Taifa linalojitegemea kwa kutumia Juhudi na Maarifa kuondoa Umasikini, Ujinga na Maradhi, yanabidi yawe sehemu ya Katiba kama muongozo na matamshi ya sisi kama Taifa.

Vipengele kama miiko ya uongozi, haki za kumiliki na mikataba ni sehemu ambazo zinahitaji kuwa katika Sheria za nchi ambazo zinalindwa na Katiba.

Vitu hivi ni suala la Taifa na kwa ridhaa ya Taifa na si chama kimoja cha siasa.
 
Kitila,

Si lazima kuleta mabadiliko tuwe wanachama wa CHADEMA pekee.
Hata nyinyi CHADEMA mkiingia, tutawaona kama CCM walivyo, hivyo kunahitajika taasisi huru isiyofungamana ili kuhakikisha kazi ya Kujenga Taifa inafanyika kwa manufaa ya Taifa na si CCM au CHADEMA!

Mkuu, hii safi kabisa lakini nafikiri huu mfumo wa NGO ambazo tayari tunazo siku zote. Ideas zote kubwa na nzuri ili zilete impact at the end of the day lazima zitekelezwe. Unachoongelea wewe ni mambo makubwa yenye kutaka kubadili mfumo wa namna tunavyoishi katika nchi yetu. Hili haliwezi kufanyika bila kugusa katiba, sheria na taratibu zingine katika nchi yetu. Huwezi kufanya haya mambo bila kubadilisha serikali. Na kwa utaratibu tuliojiwekea katika nchi yetu huwezi kubadilisha serikali bila kupitia katika chama cha siasa. kwa hiyo kumbe hii ya kusema kwamba "kunahitajika taasisi huru isiyofungamana" ni nadharia.

Nafikiri ifike mahala wanaharakati wa Tanzania waone umuhimu wa kushiriki katika siasa moja kwa moja ili kutekeleza kwa vitendo yale wanayoyaota. Hii ya kusema "huru", "isiyofungamana na upande wowote", sounds great, lakini ni nadharia. Huwezi kutaka kufanya jambo kubwa la kisiasa kama hilo la itikadi halafu useme utaweza kuwa huru au neutral! If you wanto go political, there is no way you will avoid taking political sides simply because not everybody will accept your political inclination au sio mkuu? Hata hilo Azimio la Arusha, whether ni la kitaifa au la CCM/TANU, sio kila mtu atakubaliana nalo!

Na mwisho, sidhani kama ni kweli kwamba kwa kuwa hatukuwa na chama kingine kabla ya mfumo wa vyama vingi basi kila mtu alikuwa mwana TANU au CCM; na kwa hivyo haiwezi kuwa kweli kwamba kila kilichokuwa cha CCM/TANU kilikuwa cha kila mtu au ni cha nchi, sidhani kama hivi ndivyo.
 
Mkandara,

Wananchi huchagua Raisi kutokana na Imani na kujiuza kiitikadi na kuonekana kwa utendaji wa kihistoria kwake binafsi na hata kupitia utendaji na ufanisi wa Chama.

Mategemeo au matarajio yetu ni kuwa Mtu huyu ni mahiri, mwenye busara, mpenda haki, mchapa kazi, mwajibikaji na atatumia hekima kuunda Serikali na kuteua watendaji ambao ni wasaidizi na washauri ili kushikilia dhamana ya Kulijenga na Kulilinda Taifa!

Inapotokea kwa Mkuu huyu anashindwa kazi, ni haki ya wananchi kuhoji na kama Sheria na Katiba zingekuwa ni huru na Makini, basi wananchi kwa kupitia wawakilishi wao wangekuwa na Uhuru wa kutgoa tamko la kutokuwa na Imani na Raisi wao au Serikali yake na kushurtisha kuundwa kwa Serikali mpya au Uchaguzi mpya wa Raisi.

Lakini kwa kuwa Uraisi kwa Tanzania ni "Umungu" ambao unaanzia kwenye Chama cha huyu raisi, Bungeni na hata Mahakamani, basi ni vigumu kumwajibisha ipaswavyo Raisi bila kubadili Katiba na Sheria.
 
Kitila,

Nimekupa endorsment yangu kwako binafsi kama mgombea uwakilishi. Je ni lazima niwe CHADEMA?

Ndio nakubali, kama chombo huru, matokeo yake hata kama ni ya Kisiasa, ni muhimu kuwa na nguzo huru ambayo itajumuika na ule mhimili mwingine wa Uhuru wa mawazo na habari.

Mfano, leo ikiwa ni uchaguzi mkuu na wewe ukagombea Ubungo, nitakupiia kura, lakini naweza nisimpigie kuwa Slaa kama Raisi kwa kuwa siamini kama yeye ana uwezo na ni makini. Hivyo kura yangu itakwenda kwa Mtu wa Pwani ambaye ni TLP!

Tunataka watu ambao watajiuza kwa kutumia Utaifa na kuwa na nguvu kurutubisha Utaifa na si Chama. Chama ni chombo tuu ambacho mkusanyiko wa mawazo yanayofanana fanana hukaa pamoja.

Nakubali ni lazima kupata chama kuleta mabadiliko haya kutoka nadharia mpaka vitendo. Lakini kampeni yangu si kusubiri 2010 au 2015 kwa huu msukumo kuanza kushika hatamu kuelekea kutimilika.

Msukumo huu unaanzia sasa hivi hapa miongoni mwetu na tuutangaza kwa Wananchi wenzetu 96% ambao hawasomi magazeti au kuwa kwenye mtandao wa umeme kama FISADIST alivyodai.

Chadema mkitaka kutumia msukumo wa FocusTanzania Group, ni ruksa, CCM wakijiiona na kujisahihisha wakasema twajirekebisha kwa manufaa ya Taifa ni Ruksa, same will be if CUF, TLP, UDP, NCCR will pick up the ideas and preach the gospel of Utaifa.

Narudia tena kwenye Ukristo maana ni mfano hai nilionao. Tuna Biblia, mafundishi ya Kristo na wote twataka kwenda mbinguni. Kati yetu kuna Wakatoliki, Waluteri, Waanglikana, Wasabato, SDA, Walokole, Assembly, Orthodox na free spirit, wote lengo letu ni moja, twatumia kitabu kimoja na kujenga imani za kiroho kuwa kuna maisha ya baadaye ya raha mbinguni kwa kumfuata Yesu.

Katika vikundi hivi, tunamgawanyiko wa mawazo na itikadi kuhusiana na kitabu hiki biblia na Yesu wetu. Lakini Yesu na Biblia ni huru, ni juhudi binafsi za kila muumini kuhakikisha anaelewa habari njema na mafundisho ili kwenda peponi na si umahiri wa Kanisa au mhubiri! Nikimpenda mhubiri au Kanisa fulani ni utashi binafsi, lakini kumkubali Yesu na kufuata mafundisho ya Kikristo kupitia Biblia na Amri, hilo halina Kanisa au Mhubiri.

Same logic applies to CCM, CHADEMA and TLP.
 
Chadema mkitaka kutumia msukumo wa FocusTanzania Group, ni ruksa, CCM wakijiiona na kujisahihisha wakasema twajirekebisha kwa manufaa ya Taifa ni Ruksa, same will be if CUF, TLP, UDP, NCCR will pick up the ideas and preach the gospel of Utaifa.

Rev: That is very powerfull!! Huku ndio kupona Fikra Kwanza kabla ya kujisukumizia mambo kimtulinga.
 
Rev Kishoka.

Nimepitia kwa karibu majibu uliyowatumia, Kitila, Mkandara. Joka Kuu etc. Katika kuyachamba kwa kina. Ninaona Jambo moja la msingi DIRA YA KITAIFA yenye kuzingatia Historia na mwenendo wa taifa tangu uasisi wake!Kuugunisha nguvu yote na kuelekea kwenye lengo moja. Na kulilinda Lengo hilo kikatiba

Umetumia maneno msukumo wa FocusTanzania Group.

Focus Tanzania Group! unaweza kuliweka wazi zaidi jambo hilo?
 
Rev Kishoka:

Your latest post makes more sense to me; hapo sina cha kuongeza maana ipo clear sana. Nakubali kabisa sio lazima chadema, of course mimi being chadema was easier to pick this example. Otherwise, chama chochote kinachosimamia uhai wa nchi yetu ni ruksa kabisa kama ulivyosema. Hata hivyo I doubt kama CCM kinaweza kikawa ni kati ya vyama vinavyosimamia uhai wa nchi angalau kwa sasa!

I like ur idea about focus tanzania groups, fantastic!

Interesting discussion!
 
Rev Kishoka.

Nimepitia kwa karibu majibu uliyowatumia, Kitila, Mkandara. Joka Kuu etc. Katika kuyachamba kwa kina. Ninaona Jambo moja la msingi DIRA YA KITAIFA yenye kuzingatia Historia na mwenendo wa taifa tangu uasisi wake!Kuugunisha nguvu yote na kuelekea kwenye lengo moja. Na kulilinda Lengo hilo kikatiba

Umetumia maneno msukumo wa FocusTanzania Group.

Focus Tanzania Group! unaweza kuliweka wazi zaidi jambo hilo?

Azimio,

FocusTanzaniaGroup is on pipeline, if your interested to be part of it, PM me your email and we will carry on!
 
Rev. Kishoka.

I never thought there some people with such a positive clear understanding of arusha declaration as i have seen on this thread. I would like to thanks the contribution of links given by MMwanakijiji it contains such a valuable informations of the declaration. Also the doc. from Dr shoo and Mihangwa.

Kishoka mawazo yako yataishiahivi hivi? Ok Tunakuunga mkono hasa baada ya kuona mchakato wa kina.

Naamini hata kama ni watu wachache wanaosoma hii forum kama inavyosemekana lakini nafikiri inawapatia watu a lot of knowledge na sharing of information.

Nichangie kidogo: You can read from this link. They try to analyse Arusha declaration by using The CONCEPT ON "EI" that is Emotional Intelligence. Wanakuja na matokeo mazuri dhidi ya Nchi Tanzania, Lengo la Uhuru na Azimio la Arusha.
[media]http://www.duniahai.com/Articles/Tumepoteza%20agano%20la%20uhuru.pdf[/media]

Hii ni hoja nzuri sana.
 
JC,

Hiyo interview ya Nyerere, nafikiri ni ile aliifanya NPR/PBS 1996, nilibahatika kuinoa na yale maneno ambayo Mwanakiji kayaleta hapa yalinikaa sana moyoni.

Watanzania tumeamka kutoka kwenye Usingizi wa uzembe wa kufikiri. Tulilipuuzia Azimio la Arusha na kudai eti limetuletea Umasikini.

Ukilisoma Azimio kwa makini, halikutamka eti haturuhusiwi kuwa wafanyabiashara, au kuwa na mali (utajiri). Ni kweli lilidhibiti mfumo wa uzalishaji kwa wawekezaji wa nje, lakini nia ilikuwa si kuua ushindani bali kutoa nafasi kwa Watanzania kujijenga na kupata nafasi ya kuingia katika mashindano ya kibiashara. Ndio maana katika kipengele cha Kujitegemea, kuna mkazo kuhusu Juhudi na Maarifa!

Natumaini kubadilishana kwetu huku mawazo kutachipua mbegu mpya ambayo italenga katika kuwekeza nguvu mpya za Kujenga Taifa na kudumisha Utaifa.

Hata Wamarekani iliwachukua muda na majaribio kufika mahali walipo. Sisi hatuhitaji kupitia safari ndefu tena. Tunaishi katika karne yenye maendeleo ya hali ya juu na ni jukumu letu kama Wananchi, kujifunza kutoka kwa wenzetu kuharakisha safari ya Maendeleo.

Miaka ya sitini, Nyerere alisema, wakati Mmarekani ameanza kwenda mwezini, sisi bado tunatembea (natumaini nukuu ni sahihi), tuamke na kuanza kukimbia lakini si kwa ule mwendo wa kasungura na ndege inayopaa!

Nashukuru kwa nyaraka uliotuma na baada ya kuipitia nitakuja na majibu.
 
Mchungaji,

Kudos kwa kuanzisha huu mjadala. Mimi niko interested zaidi na uhuru wa mihimili ya serikali. Kwa kweli inaniuma sana kuona wabunge walioteuliwa na wananchi, wengi wao wakiwa vijijini, wanageuka kile walichokisema wakati wa kampeni kwa kuwa wamepata uwaziri.

Mawaziri wangepaswa wasiwe wanasiasa. Kuhusisha kila kitu na siasa ndio chanzo cha rushwa na ufisadi, at least kwa sasa. Mawaziri wanatakiwa wawe wajuzi katika wizara zao, wapendekezwe na Rais, wapitishwe na Bunge. Hii itamfanya Rais (and consequently Prime Minister) asiwe na nguvu za kuburuza Bunge au Mahakama.

Hali iliyopo kwa sasa ni kuwa Bunge lipo pale kwa jina tu, halina nguvu. Mwananchi mmoja aliuliza majuzi, kwa nini CCM yenye wabunge wengi walipitisha bajeti na kuafikiana na kamati ya kina Malima na Kigoda kuhusu uozo wa BoT? Spika naye kwa kuona hana ubavu wowote wa size yake anaanza kuonea kina Zitto kwa mambo ya kichama. Kama wabunge (na Bunge) wangekuwa huru kutoka kwa serikali na hususan chama tawala, bila kuogopa nidhamu ya chama.

Kwa upande mwingine, angalau Mahakama ndio imekuwa ikilalamika juu ya kuporwa uhuru wake na Bunge. Kama utakumbuka, hivi karibuni Jaji Mkuu Samatta alistaafu. Baada ya kustaafu alielezea kutopendezwa kwake na ubabe unaotumiwa na Bunge katika kuingilia uhuru wa Mahakama. At least, he spoke out, even though it really should have been when he was still in the office.

Jibu lako kwa Kitila juu ya kumsupport yeye kama Kitila bila ya wewe kuwa mwanaChadema ni jambo jema. Nimependezwa sana si kwa ajili ya msimamo wako, bali ni kitu kinachoashiria kuwa katiba inapaswa irekebishwe (na kufanywa katiba ya nchi na si ya CCM)na sasa ni muda muafaka wa kuruhusu wagombea binafsi.

Wagombea binafsi, naamini, wataleta chachu mpya katika siasa na maendeleo ya taifa letu. Kuna watu wengi tu wenye uwezo na uchungu wa kuongoza lakini hawataki wawe associated na chama fulani kwa sababu mbalimbali. Sasa hao watu tuwaache tu wasiwe katika vyombo vyetu vikuu? Sikubaliani nalo.

Once again, many thanks for starting such a stimulating debate. Kumbuka, kama jinsi Azimio la Arusha lilivyoshindwa (kutokana na utendaji mbovu) basi nasi tujifunze katika makosa hayo ili tusije tukasutwa na watoto wa watoto wetu siku za usoni!
 
Rev Kishoka.

Nimepitia kwa karibu majibu uliyowatumia, Kitila, Mkandara. Joka Kuu etc. Katika kuyachamba kwa kina. Ninaona Jambo moja la msingi DIRA YA KITAIFA yenye kuzingatia Historia na mwenendo wa taifa tangu uasisi wake!Kuugunisha nguvu yote na kuelekea kwenye lengo moja. Na kulilinda Lengo hilo kikatiba

Azimio,

Sisi ni jamii moja. Tunatofautiana umri, lugha, dini hata jinsia. Lakini ni wajibu wetu kujenga umoja wa kitaifa na kuimarisha misingi ya haki na usawa ambao utasaidia msukumo wa maendeleo na kutuwezesha kujijenga kiushindani ndani na nje ya nchi.

We can only make profound bipartisan political changes if we first change the spirit of community. If a few of us will stand up to champion these changes to overhaul our political structure by empowering our citizens, then by small quantities we will make progress and gain followers who will think of their nation first, before their political affiliation.

We the 1% are starting the progress here at JF, trying to mobilize our common energies and eventually, the 3% of those who read newspapers, will hear our voices. Then the 3% will share news of our movement to the 96% of have no access to internet or newspapers.
 
Back
Top Bottom