Afrika hatukua tayari kupata Uhuru miaka ya 50-60

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,597
215,270
Miaka karibia 60 baada ya uhuru 50% ya raia hawana uhakika wa huduma za jamii. Kuna vijiji huko unasafiri siku mbili kabla hujafika kituo chako cha karibu cha polisi. Mtu akifariki kama ni kifo chenye mashaka inabidi maiti ikae siku mbili ndani kabla polisi hajafika.

Elimu, Afya, Maji hali ya huduma ni hivyo hivyo. Huduma za jamii zimekua mtaji wa siasa. Wananchi wanaahidiwa, serikalili inaingia madarakani na baada ya miaka mitano mnaomba mambo yale yale.

Katika harakati za siasa, TANU ilipaswa kuhimiza watu wapate elimu. Wengi wangeelimika wangesukuma maendeleo. Kukosa elimu watu wanafikiri wanapata huduma za jamii kwa hisani ya serikali. Hawafikirii kuwa Hii ni kodi wanayolipa na huduma ni jukumu la serikali si hisani.
 
Kwa mfumo wa utawala wetu wa kutegemea kila kitu kifanywe na mtu moja, Tanzania haitaendelea mpaka huu mfumo ubadirishwe. Haiwezekani kuchongwa kwa Barabara kijijini kwetu au kupata Bomba la maji ni mpaka Yohana aamue au akubali kwanza ndiyo kifanyike.
 
Kweli kabisa hata ukiangalia nchi zote zilizo chelewa kupata uhuru ndio zenye maendeleo

Sent using Damu ya Yesu
 
Not at all.
Waliokabidhiwa madaraka ndio vibaka, watoto wa mjini, wahuni n.k
Waliokua na wako tayari kuwa huru ndio wale mliowapitishia viongozi bila kupingwa wala kupigiwa kura.
 
Hii hapa Ndiyo mizoga inayosumbua Tanzania

1. Mzoga wa FEDHA maana hakuna fedha isiyo na matumizi

2. Mzoga wa Wivu hata VIPI watu hawatakiwi kufaniniwa hata Kwa njia Hali

3. Mzoga wa Dharau hapa watu wanadharau hata kitu unachofanya mwenyewe

4. Mzoga wa kila kitu chako hapa ni maandalizi ya kuuwa kila kitu ili tupate UHURU Bora ni RAIS WA Kenya

5. Mzoga wa connection hapa hata VIPI kuna baadhi ya wadau wasahau kupata huduma MTU wa connection akifa

6. Mzoga wa kutengana kwenye maamuzi HaPA ni rais kuelewa kuwa RAIS, makamu wake, waziri mkuu wake, mawaziri wapo Kwa ajili ya fursa ya IPO siku na Mie nitakuja rais mapungufu yako ni fursa
 
Kwani kabla ya wakoloni tulikuwa tunaishi vipi?

Wakoloni wamedidimiza maisha ya wananchi waliowatawala kwa sababu walitumia maliasili zao kujiimarisha kiuchumi, kisiasa na kijamii.

Wakoloni wameiba mpaka mfumo wa elimu ambao waanzilishi ni Wamisri achilia mbali malighafi na wakahakikisha wanafanya kila linalowezekana ili hata wenye elimu wasinufaike.

Nchi za kiafrika haziendelei kwa sababu wakoloni wameasisi na wanamiliki dhana ya resource curse!
 
Wewe sky katawaliwe wewe mwenyewe. Najua unataka kuilinganisha marekani na tz. Marekani ina umri wa miaka 400 na sisi tuna umri wa kiaka 50+ sasa tafuta picha za taifa hilo 350 yrs ago then angali ulinganishe na sisi leo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwani kabla ya wakoloni tulikuwa tunaishi vipi?

Wakoloni wamedidimiza maisha ya wananchi waliowatawala kwa sababu walitumia maliasili zao kujiimarisha kiuchumi, kisiasa na kijamii.

Wakoloni wameiba mpaka mfumo wa elimu ambao waanzilishi ni Wamisri achilia mbali malighafi na wakahakikisha wanafanya kila linalowezekana ili hata wenye elimu wasinufaike.

Nchi za kiafrika haziendelei kwa sababu wakoloni wameasisi na wanamiliki dhana ya resource curse!
Wakoloni waliwezaje kututawala?
Kwanza walikuja na bunduki wakati sisi tulikuwa na majeshi ya upinde na mshale pamoja na mikuki.

kama wakoloni waliwwza kunufaika na rasilimali zetu mbona sisi hazitunufaishi?
 
Wakoloni waliwezaje kututawala?
Kwanza walikuja na bunduki wakati sisi tulikuwa na majeshi ya upinde na mshale pamoja na mikuki.

kama wakoloni waliwwza kunufaika na rasilimali zetu mbona sisi hazitunufaishi?
Nadhani umesoma angalizo langu lakini hukulielewa vizuri!

Nimeandika, wakoloni wameasisi dhana ya resource curse ambayo wanaitumia kuhakikisha rasilimali haziwanufaishi Waafrika.
 
Miaka karibia 60 baada ya uhuru 50% ya raia hawana uhakika wa huduma za jamii. Kuna vijiji huko unasafiri siku mbili kabla hujafika kituo chako cha karibu cha polisi. Mtu akifariki kama ni kifo chenye mashaka inabidi maiti ikae siku mbili ndani kabla polisi hajafika.

Elimu, Afya, Maji hali ya huduma ni hivyo hivyo. Huduma za jamii zimekua mtaji wa siasa. Wananchi wanaahidiwa, serikalili inaingia madarakani na baada ya miaka mitano mnaomba mambo yale yale.

Katika harakati za siasa, TANU ilipaswa kuhimiza watu wapate elimu. Wengi wangeelimika wangesukuma maendeleo. Kukosa elimu watu wanafikiri wanapata huduma za jamii kwa hisani ya serikali. Hawafikirii kuwa Hii ni kodi wanayolipa na huduma ni jukumu la serikali si hisani.
Soma hii...

 
Wewe sky katawaliwe wewe mwenyewe. Najua unataka kuilinganisha marekani na tz. Marekani ina umri wa miaka 400 na sisi tuna umri wa kiaka 50+ sasa tafuta picha za taifa hilo 350 yrs ago then angali ulinganishe na sisi leo

Sent using Jamii Forums mobile app
Hapana ninasngalia maisha wakati wa utawala wa Mjerumsni, alianzisha commercial farming za katani, pampa, tumbaku, kahawa na chai. Alituchapa viboko ni lazima uende kazini na ulipe kodi.

sasa hivi ardhi tunayo lakini hakuna commercial farming, watu hawana ajira.
 
Nadhani umesoma angalizo langu lakini hukulielewa vizuri!

Nimeandika, wakoloni wameasisi dhana ya resource curse ambayo wanaitumia kuhakikisha rasilimali haziwanufaishi Waafrika.
Kutambua tatizo ni nusu ya kulitatua. Sasa kama tumejua issue is a curse what are we doing about it?
 
Kutambua tatizo ni nusu ya kulitatua. Sasa kama tumejua issue is a curse what are we doing about it?
Tatizo tumelitambua ndio maana tunapiga hatua kidogo kidogo huku tukipambana nalo!

Kwa hatua hizo ndogo ndogo, Tanzania ya 50yrs ago ni tofauti na Tanzania ya leo!
 
Miaka karibia 60 baada ya uhuru 50% ya raia hawana uhakika wa huduma za jamii. Kuna vijiji huko unasafiri siku mbili kabla hujafika kituo chako cha karibu cha polisi. Mtu akifariki kama ni kifo chenye mashaka inabidi maiti ikae siku mbili ndani kabla polisi hajafika.

Elimu, Afya, Maji hali ya huduma ni hivyo hivyo. Huduma za jamii zimekua mtaji wa siasa. Wananchi wanaahidiwa, serikalili inaingia madarakani na baada ya miaka mitano mnaomba mambo yale yale.

Katika harakati za siasa, TANU ilipaswa kuhimiza watu wapate elimu. Wengi wangeelimika wangesukuma maendeleo. Kukosa elimu watu wanafikiri wanapata huduma za jamii kwa hisani ya serikali. Hawafikirii kuwa Hii ni kodi wanayolipa na huduma ni jukumu la serikali si hisani.
Sasa hivi tunatawaliwa na chama tena kwa mabavu, maneno kebekebe yaliyojaa kejeli kwa kutoka kwa viongozi wake.
Mtawala tu amebadilika, bora tungeendelea kutawaliwa na hao watawala wa zamani
 
Miaka karibia 60 baada ya uhuru 50% ya raia hawana uhakika wa huduma za jamii. Kuna vijiji huko unasafiri siku mbili kabla hujafika kituo chako cha karibu cha polisi. Mtu akifariki kama ni kifo chenye mashaka inabidi maiti ikae siku mbili ndani kabla polisi hajafika.

Elimu, Afya, Maji hali ya huduma ni hivyo hivyo. Huduma za jamii zimekua mtaji wa siasa. Wananchi wanaahidiwa, serikalili inaingia madarakani na baada ya miaka mitano mnaomba mambo yale yale.

Katika harakati za siasa, TANU ilipaswa kuhimiza watu wapate elimu. Wengi wangeelimika wangesukuma maendeleo. Kukosa elimu watu wanafikiri wanapata huduma za jamii kwa hisani ya serikali. Hawafikirii kuwa Hii ni kodi wanayolipa na huduma ni jukumu la serikali si hisani.

Tulikimbilia uhuru ili kuondokana mateso ya kikoloni ya manyanyaso na kuwekwa ndani hovyo hovyo! Kitu ambacho naona bado kinaendelea, bora tungeendelea tu kuwa kwenye ukoloni for sure!

Hatukujipanga kwa mengine, tulijipanga na kukimbia mateso basi! Thus why haya mengine ya maendeleo, afya na malazi yemekuwa mzigo sana kwetu.
 
Hapana ninasngalia maisha wakati wa utawala wa Mjerumsni, alianzisha commercial farming za katani, pampa, tumbaku, kahawa na chai. Alituchapa viboko ni lazima uende kazini na ulipe kodi.

sasa hivi ardhi tunayo lakini hakuna commercial farming, watu hawana ajira.
Commercial farming aliziua Nyerere baada ya kuwanyanga wakulima wa kizungu na kuzitaifisha NAFCO.
Tuseme Nyerere alikurupuka kabla ya kuandaa vyema NAFCO.
Kukurupuka,africanization,Roho mbaya,UFISADI ,ndio uliangusha mataifa ya Kiafrika baada ya kupata uhuru.
 
Back
Top Bottom