Miaka 50 ya Reli ya TAZARA: Safari ya ushirikiano kati ya China na Afrika

Miaka 50 ya Reli ya TAZARA: Safari ya ushirikiano kati ya China na Afrika

Yoyo Zhou

Senior Member
Joined
Jun 16, 2020
Posts
189
Reaction score
314
VCG31N1717009890.jpg
Huu ni mwaka wa 50 tangu kuzinduliwa rasimi wa Reli ya TAZARA. Reli hiyo inayopita Bonde la Ufa la Afrika Mashariki ni ushuhuda wa urafiki kati ya China na Afrika. Nusu karne iliyopita, wahandisi na mafundi wa China walifanya kazi bega kwa bega na ndugu zao wa Afrika, kukamilisha mradi wa TAZARA “uliokuwa mgumu kutekelezeka”. Hivi leo, reli hiyo inayohuishwa ni kama pingu za kiroho zinazounganisha China na Afrika zenye mustakabali wa pamoja.

Katika miaka ya 1960, Zambia ambayo ni mzalishaji wa tatu wa shaba duniani, ilikabiliwa na changamoto ya mauzo ya nje ya shaba kutokana na vizuizi vilivyowekwa na serikali za kikoloni za nchi jirani. Mwalimu Juliusi Nyerere wa Tanzania aliomba msaada kwa jamii ya kimataifa, nchi za magharibi zilikataa bila ya kusita, ila China, ambayo wakati ule ilikuwa inakabiliwa na changamoto mbalimbali za kiuchumi ilikubali kutoa msaada.

Mwaka 1965, aliyekuwa rais wa China Mao Zedong alimwambia Nyerere, “Tutasaidia kujenga reli hiyo hata kama tukilazimika kuacha kujenga reli nyumbani.” Halafu China ilitoa fedha na kupeleka makumi ya elfu ya wahandisi na mafundi wa China kujenga reli hiyo. Walifanya kazi ngumu kwa kushirikiana na wenzao wa Tanzania na Zambia kwa miaka sita, mpaka kukamilisha reli hiyo yenye urefu wa kilomita 1,860.

Mwaka 2024, China, Tanzania, na Zambia zilisaini Mkataba wa Makubaliano kuhusu Mradi wa Uhuishaji wa Reli ya TAZARA, zikiamua kuirekebisha kikamilifu reli hiyo. Mwaka 2025, mradi huo ulianza rasmi, na makampuni ya China yakishirikiana na makampuni ya Tanzania na Zambia yataunganisha reli hiyo na mtandao wa reli wa kikanda, na kuunda mfumo mpya wa “usafirishaji wa reli na bandari” na Bandari ya Dar es Salaam. Mara tu mradi huo utakapokamilika, Reli ya TAZARA inatarajiwa kuongeza mara tatu uwezo wake wa usafirishaji wa kila mwaka.

Baada ya miaka 50, moyo wa Reli ya TAZARA umepata uhai mpya katika ushirikiano wa China na Afrika. Katika miaka ya hivi karibuni, reli nyingine nyingi zilizojengwa na China ikiwemo reli ya SGR inayounganisha Nairobi na Mombasa na reli inayounganisha Addis Ababa na Djibouti, zilizinduliwa barani Afrika. Ushirikiano kati ya China na Afrika unastawi katika nyanja mbalimbali kama vile uchumi wa kidijitali, maendeleo ya kijani, juhudi za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, na huduma za elimu na afya.

Pendekezo la China la “Ukanda Mmoja, Njia Moja” linaendana na Ajenda ya Afrika ya 2063. China imeendelea kuwa mshirika mkubwa zaidi wa kibiashara wa Afrika kwa miaka 17 mfululizo. China na Afrika zimeinua kiwango cha uhusiano wao kuwa Jumuiya yenye Hatma ya Pamoja katika Enzi Mpya.

Safari ya miaka 50 ya Reli ya TAZARA imeshuhudia uhusiano wa kirafiki wa China na Afrika. Hadi leo, moyo wa reli hiyo wa usawa, kuheshimiana, na kunufaishana bado ni moyo wa ushirikiano wa China na Afrika. Wakati dunia inapokabiliana na mabadiliko makubwa ambayo hajawahi kutokea katika miaka 100 iliyopita, China itaendelea kushirikiana na nchi za Afrika kusukuma mbele ujenzi wa jumuiya yenye hatma ya pamoja ya pande hizo mbili
 
Tazara is the whitest of the white elephant projects ever established in this country.
 
Serikali inapotaka kuaanzisha jambo, basi ni lazima wananchi katika sectors mbalimbali wajumuishwe. Kuanzia implementation mpaka uendeshaji.

Sasa ivi , copper zinasafirishwa kwa malori na kuiacha tazara, ni Kwa sababu tazara Haina mafuaa kwa wa TZ wafanya Biashara ya usafirishaji

Kama wa TZ wazawa wenye companies za usafirishaji wangepewa ubia kwenye tazara, basi tungeona hili shirika likukuwa
 
sOMO!
Tazara irudishwe Kwa wachina mana bado raslimali watu hawapo (experts)
Washarudishiwa kwa mkataba wa miaka makumi naa,lakini chakustajabisha mali zote za Tazara upande wa Dar kuanzia Viwanja,maeneo ya wazi,nyumba za watumishi/Maghorofa na kota ya pale Temeke Vetinary na kule Mchicha zimeuzwa vyote kwa wakina Lake Oil na Oil Com. Sasa sijui huyo mchina akitaka kufufua shirika wafanyakazi watakaa wapi.
 
Shirika linaongoza kwa madeni kuanzia kwa watumishi wake mpaka kwa watoa huduma wa nje. Wafanyakazi wanadai mishahara miaka kwa miaka. Ile treni daladala aka Mwakyembe tuu imewashinda kuendesha,madeni kibao ya diesel.
 
Washarudishiwa kwa mkataba wa miaka makumi naa,lakini chakustajabisha mali zote za Tazara upande wa Dar kuanzia Viwanja,maeneo ya wazi,nyumba za watumishi/Maghorofa na kota ya pale Temeke Vetinary na kule Mchicha zimeuzwa vyote kwa wakina Lake Oil na Oil Com. Sasa sijui huyo mchina akitaka kufufua shirika wafanyakazi watakaa wapi.
Uchafu mavikunuka uliopo tazara usikiage tu afadhari ,mana nilikua nahisi yalikuwa maneno tu karatasini
 
Washarudishiwa kwa mkataba wa miaka makumi naa,lakini chakustajabisha mali zote za Tazara upande wa Dar kuanzia Viwanja,maeneo ya wazi,nyumba za watumishi/Maghorofa na kota ya pale Temeke Vetinary na kule Mchicha zimeuzwa vyote kwa wakina Lake Oil na Oil Com. Sasa sijui huyo mchina akitaka kufufua shirika wafanyakazi watakaa wapi.
Mchina anaangalia TU 😂, kusafirisha mizigo yake kutumia tazara kwenda corridor ya huko kusini
 
Back
Top Bottom