Taliban yaruhusu wanawake kupigwa ila wasivunjwe mifupa au kupata majeraha

Taliban yaruhusu wanawake kupigwa ila wasivunjwe mifupa au kupata majeraha

Traxtion

JF-Expert Member
Joined
Dec 10, 2021
Posts
6,164
Reaction score
12,492
Kiongozi mkuu wa Taliban, Hibatullah Akhundzada amesaini sheria mpya ya adhabu nchini Afghanistan ambayo inaruhusu wanaume kuwapiga wake na watoto wao, isipo kuwa vipigo hivyo havisababishi kuvunjika kwa mifupa kwenye miili yao.

Aidha mazingira ya kisheria kwa wanawake yamezidi kuwa magumu, ambapo sasa mwanamke anaweza kufungwa hadi miezi mitatu gerezani ikiwa atatembelea ndugu zake bila ruhusa ya mumewe.

Vile vile mwanamke anapodai kufanyiwa ukatili mahakamani, analazimika kuleta ushahidi akiwa amejifunika mwili mzima na akiwa ameambatana na mlezi wa kiume Shirika la kutetea haki za binadamu la Rawadari limetoa wito kwa Umoja wa Mataifa (UN) kuingilia kati mara moja.
1771514387509.jpg

Source 1: Chazy Media
Source 2: ‘Harsh Beatings, No Broken Bones': Taliban’s New Law Allows Men To Physically Punish Their Wives Amid Ongoing Women’s Rights Crackdown- What We Know
 
Wakikaidi
ah, sawa
Ila Taliban treatment zao kwa wanawake nawakubali sana mambo ya haki sawa haya ndio yamefanya ndoa ziwe ngumu sana huko ulaya huku Africa wanaanza kuota mapembe taratibu.

Mwanamke anatakiwa apelekwe mchakamchaka.
kwahio wahenga walikosea kusema mwanamke hapigwi ngumi anapigwa na kanga.
 
Kiongozi mkuu wa Taliban, Hibatullah Akhundzada amesaini sheria mpya ya adhabu nchini Afghanistan ambayo inaruhusu wanaume kuwapiga wake na watoto wao, isipo kuwa vipigo hivyo havisababishi kuvunjika kwa mifupa kwenye miili yao.

Aidha mazingira ya kisheria kwa wanawake yamezidi kuwa magumu, ambapo sasa mwanamke anaweza kufungwa hadi miezi mitatu gerezani ikiwa atatembelea ndugu zake bila ruhusa ya mumewe.

Vile vile mwanamke anapodai kufanyiwa ukatili mahakamani, analazimika kuleta ushahidi akiwa amejifunika mwili mzima na akiwa ameambatana na mlezi wa kiume Shirika la kutetea haki za binadamu la Rawadari limetoa wito kwa Umoja wa Mataifa (UN) kuingilia kati mara moja.
1771515981355.jpg
 
Kiongozi mkuu wa Taliban, Hibatullah Akhundzada, amesaini sheria mpya ya adhabu nchini Afghanistan ambayo inaruhusu wanaume kuwapiga wake na watoto wao, mradi tu vipigo hivyo havisababishi kuvunjika kwa mifupa au majeraha ya wazi mwilini.

Sheria hiyo ambayo imezua taharuki kimataifa, haikuishia hapo, bali imegawanya jamii katika madaraja ya kijamii, ambapo adhabu hutofautiana kulingana na hadhi ya mkosaji.

Kulingana na kituo cha habari cha FirstPost, chini ya mfumo huu mpya, wasomi wa dini hupewa ushauri pekee wanapokosea, watu wa daraja la chini hukabiliwa na vifungo vya gerezani au adhabu za viboko.

Mazingira ya kisheria kwa wanawake yamezidi kuwa magumu, ambapo sasa mwanamke anaweza kufungwa hadi miezi mitatu gerezani ikiwa atatembelea ndugu zake bila ruhusa ya mumewe.

Aidha, mwanamke anapodai kufanyiwa ukatili mahakamani, analazimika kuleta ushahidi akiwa amejifunika mwili mzima na akiwa ameambatana na mlezi wa kiume.

Takbiiiiiiir😁😁😁😁.
 
Back
Top Bottom