ACT - Wazalendo waomba kujiunga na UKAWA

ACT - Wazalendo waomba kujiunga na UKAWA

Walikuwa wapi wakati bunge maalumu la katiba?
 
Mkuu tuliwaambia kuwa chadema wamezidi ubaguzi wao wanataka kupewa kila kitu hivi ulishaona wapi wao wanataka kutoa mgombea urais ,watoe waziri mkuu halafu Cuf eti watoe makamu wa rais lakini NCCR hawajapewa nafasi hata moja.

Lakini jambo baya zaidi wanataka majimbo ya dar yote waachiwe chadema sasa nani atakubali ujinga kama huo.

Ukiongea hivi ndo unawatia hasira ukawa za kuiondoa magambas we shauri yako
 
Mkuu tuliwaambia kuwa chadema wamezidi ubaguzi wao wanataka kupewa kila kitu hivi ulishaona wapi wao wanataka kutoa mgombea urais ,watoe waziri mkuu halafu Cuf eti watoe makamu wa rais lakini NCCR hawajapewa nafasi hata moja.

Lakini jambo baya zaidi wanataka majimbo ya dar yote waachiwe chadema sasa nani atakubali ujinga kama huo.

kumbagua msaliti sio kosa
 
Usaliti unaanza kumtafuna taratibu sasa anataka kuungana na #WasakaTonge. UKAWA hatutafanya makosa ya kumkaribisha msaliti na wasaliti wenzie ambao nia na madhumuni yao makubwa ni kuisambaratisha CHADEMA. Wameona kuisambaratisha CHADEMA ni ndoto za alinacha sasa wanataka kuingia UKAWA ila wakavuruge mshikamano uliokuwepo. UKAWA hatutaki wasaliti wala hatutaki ayatullah.

Ukiona adui yako anaomba urafiki wa ghafla na wewe inabidi utafakari kwa jicho la nne kulikoni?

Shtuka!!
 
Kitu gani maalum sana ACT wanakiona ni muhimu wakipate ndani ya UKAWA? Kwa mtazamo wangu bado ni chama kichanga kiumri na kinahitaji sana kujijenga ili kiwe na mfumo mzuri wa kisiasa na uendeshaji kabla ya kufikiria kujiunga kwenye ushirikiano wowote ule. Wanahitaji kujipambanua ndani ya jamii na Watanzania, wawe na mfumo na mtandao wa chama chao, waaminike na wawe na uwezo wa kuendesha mambo yao kwa kujisimamia wao wenyewe kwanza.

Kwa hisia za usaliti wanazotuhumiwa nazo na baadhi ya wanaUKAWA ni sababu tosha kuwa wanahitaji kushughulikia chama chao ili kuwaaminisha Watanzania kuwa yanayozungumzwa dhidi yao si sahihi hiyo itawasaidia kupata huruma ya Watanzania na pengine kuchaguliwa vyema wakati wa uchaguzi.

Binafsi sijashawishika kama wanayo dhamira ya kweli ya kuwa chama cha siasa, ukiachilia mbali harakati za mikutano waliyofanya hivi karibuni ambayo bahati nzuri ilipata nafasi kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii. Ukiondoa hilo ACT haijafanya sana katika siasa za upinzani. Kujiunga na UKAWA ni kujimeza na watakosa 'identity' kwani wao ni tofauti sana na hivyo vyama vingine kama CUF. NCCR, CDM ambavyo historia zao zinaeleweka na vimeshapitia misukosuko mingi ya kisiasa na NLD ambacho haina cha kupoteza katika umoja huo hata ukisambaratika.


Kukataliwa na CHADEMA ichukuliwe kama chachu ya kufanya kazi na kuondoa doa la usaliti inalotuhumiwa nalo, kung'ang'ania kutamaanisha kuwa hisia za usaliti zina ukweli. Hawakuwepo katika harakati za kuunda huo umoja hadi hapo ulipofika, sioni sababu kwa nini sasa walazimishe hata kama hawakubaliwi na mmoja tu kati ya waundaji wa UKAWA yaani CDM.

Ikumbukwe kuwa wenzao wameshafika mbali sana katika harakati za kuimarisha ushirikiano huo, inawezekana kuwakubalia wao itamaanisha kurudi nyuma hatua kadhaa na kulazimika kurekebisha baadhi ya taratibu za umoja wao. Nawashauri ACT wawaache wenzao waendelee na mipango yao.


Sitaki kuamini kuwa ACT haiwezi kufanya kazi bila UKAWA. Wakiendelea watasababisha UKAWA kutingishika na kusababisha mpasuko au mgawanyiko. Tuhuma zote zitawaangukia wao ACT na wataadhibiwa na Watanzania. Wajipambanue kama chama cha siasa ambacho kilisajiliwa ili kifanye siasa bila kutegemea nguvu ya kutoka nje ya wao wenyewe. Wasimame katika dhana ya kuwa wanaweza kuendesha siasa zao kama ilivyo kwa TLP, UDP na wengine ambao hawamo ndani ya UKAWA.

Nice analysis actual hapa naona Yale madai ya kusema ACT imetumwa kupunguza kura za UKAWA yamekufa namshauri Zitto atuliehoja yao muhimu wameishaipangua wenyewe kweli jamaa ni genius yani kawalazimisha kula matapishi yao
 
Mimi barua yao ACT Wanafiki samahani WAZALENDO niliiona inakwenda CCM ni yakuomba kuongezewa fedha za mikutano yao awamu ya pili siya kujiunga na UKAWA.
 
Mkuu wangu Ngongo , hebu tuambie lini CUF iliacha kuwa CCM B?

Hapo sasa, ndio maana wahenga walisema njia ya muongo ni fupi!

Chadema wanachekesha sana wanasema Zitto ni CCM wakati ndani ya UKAWA kuna mteule wa Mwenyekiti wa CCM, Mbatia.

Wakati huo wapo na CUF ambao ni washirika wa CCM.

Ukawa ni vituko vitupu.

Kila shetani na mbuyu wake zitto na mbowe watajuana wenyewe kivyao.

Wana Ukumbi,.

Katika gazeti la changamoto katika ukurasa wake wa kwanza unasomeka "Zitto azidi kuwaumiza CHADEMA" na habari hiyo ukiifuatilia ndani inaeleza kuhusu kauli ya mwenyekiti wa CHADEMA, mhe Mbowe na jinsi Zitto alivyoipokea.

Kwa mujibu wa gazeti hilo ni kwamba, Zitto hakutarajia mtu ambae yeye anamuheshimu katika siasa kuwa na misimamo isiyo tanguliza maslahi ya taifa mbele na badala yake kushikilia matatizo yao yaliyojitokeza huko nyuma ambayo kimsingi yalihusu nafasi za kiuongozi.

Zitto alieleza kuwa kwa sasa hayupo tayari kujibizana na viongozi tena kwa kuwa amekuwa akisema hivyo kila mahali anapokwenda kufanya mikutano yake na amewekeza nguvu nyingi katika kukitangaza chama chake kipya. Pamoja na malengo hayo, ila kwa kauli ile ya jana ameona hana budi kuitolea maelezo!

Zitto alisisitiza kuwa matatizo yake binafsi na viongozi wa chama chake cha zamani yasipewe kipaumbele kuliko maslahi ya taifa. Ameeleza kuwa mara kadhaa ameomba chama chake kijiunge na UKAWA lakini CHADEMA wamekuwa wakigoma. Kauli ile ya jana sio ngeni masikioni pangu. Alieleza Zitto.

Zitto aliongezea kuwa, "kama ni matatizo basi ni kati yangu na viongozi wa CHADEMA na yasifanywe ya taifa zima. ACT-Wazalendo tuna nia ya dhati ya kuwaondoa CCM madarakani. Pia UKAWA wana nia hiyo hiyo. Kwa hali hiyo hatuna budi kushirikiana kummaliza CCM na hilo litafanyika kama kweli tumetanguliza utaifa mbele badala ya matatizo yetu binafsi na viongozi wa chama changu cha zamani."

My Take,

Zitto amekomaa kisiasa na ana ngozi ngumu sana. Pamoja na mihasira ya Mbowe na maneno yake ya ovyo kuhusu Zitto kisa tu uenyekiti wa CHADEMA, lakini kijana Zitto amemjibu kistaarabu sana na bado ameonyesha nia ya kutaka ushirikiano na UKAWA. Kudos.
Kinachonishangaza wengi wa hawa wanaoshinikiza Zitto na chama chake wajiunge na UKAWA, ni watu ambao wamethibitika humu JF kuwa ni wana CCM damu.

Hao wote niliowanukuu hapo juu ni watetezi wa CCM na wapiga propaganda wa CCM aka team lumumba.

Swali ambalo mtu yoyote mwenye kufikiri vizuri anajiuliza, ni kuwa: Je ni kweli hawa wana CCM wanaipangia UKAWA kikosi ya kujipanga kuiondoa CCM madarakani wakiwa na nia ya dhati au ndio mikakati ya kupandikiza virusi vyao???!!!

Tena wanashinikiza mikakati ya UKAWA kuiondoa CCM madarakani iwe kadiri wana CCM wenyewe wanavyotaka.

Huhitaji PhD kuona hisia za U P A N D I K I Z I na unaweza kuwelewa sasa kwa nini CHADEMA wanakataa, hofu ya U S A L I T I , ambao umeshaleta madhara CHADEMA.
 
Ukweli ni kwamba zitto angekua mwanamke angekua na wanaume wengi, maana anawashwa sana huyu binti
 
Teh teh teh Lipumba alimsaidia kikwete kwenda ilkulu leo agizo la ukawa cuf na nccr mliwakataa mchana kweupe kwamba ccm b leo kulikoni mshawahi kutangazia umma kwamba zile kauli sio za kweli ili tuwaelewe?

Chama kikiwa ndani ya UKAWA kimekuwa kipya. Ya kale yamepita, tazama, yamekuwa UKAWA.

Ndio maana hata Alliance for Cowards and Traitors aka Agizo la Chama Tawala (angalia mahali walipofanyia mkutano wao kule Arusha) nao wanataka kujiunga ili usaliti uwe umepita. Lakini kwa bahati mbaya hata huo ulaghai wa kujiunga ni ili wanaendeleze usaliti wao. Bado wako kazini. Hawataki ya kale yaishe bali wanataka wende nayo UKAWA. Wameshindwa! Nilishawaambia tangu awali kuwa hiyo (ACT) ngoma ya kitoto, haikeshi! Utaona.

Salama yao ACT ni kujiunga rasmi na hadharani (sio kufanya sirini) na Umoja wa Katiba ya Chenge (UKACHE) pamwe na wenzi wao CCM, TLP, UMD, nk.
 
Chama kikiwa ndani ya UKAWA kimekuwa kipya. Ya kale yamepita, tazama, yamekuwa UKAWA.

Ndio maana hata Alliance for Cowards and Traitors aka Agizo la Chama Tawala (angalia mahali walipofanyia mkutano wao kule Arusha) nao wanataka kujiunga ili usaliti uwe umepita. Lakini kwa bahati mbaya hata huo ulaghai wa kujiunga ni ili wanaendeleze usaliti wao. Bado wako kazini. Hawataki ya kale yaishe bali wanataka wende nayo UKAWA. Wameshindwa! Nilishawaambia tangu awali kuwa hiyo (ACT) ngoma ya kitoto, haikeshi! Utaona.

Salama yao ACT ni kujiunga rasmi na hadharani (sio kufanya sirini) na Umoja wa Katiba ya Chenge (UKACHE) pamwe na wenzi wao CCM, TLP, UMD, nk.

Cuf na nccr sio ccm b na kafulila sio msaliti leo hii.
 
Zitto alinukuliwa akisema ACT iko tayari kujiunga na chama chochote ili mradi Umoja huo usiwe na malengo ya kugawana vyeo, lakini pia alitoa masharti kwamba lazima viendane na itikadi ya ACT. Nachujua mimi Ukawa havina sera za kijamaa. Ila nafahamu pia Zitto anaweza kuvishawishi vyama vya ADC, TLP, UPDP, DP, NRA, TFP, Jahazi Asilia, CCK kufuata itikadi ya kijamaa ili waungane pamoja
 
Zitto alinukuliwa akisema ACT iko tayari kujiunga na chama chochote ili mradi Umoja huo usiwe na malengo ya kugawana vyeo, lakini pia alitoa masharti kwamba lazima viendane na itikadi ya ACT. Nachujua mimi Ukawa havina sera za kijamaa. Ila nafahamu pia Zitto anaweza kuvishawishi vyama vya ADC, TLP, UPDP, DP, NRA, TFP, Jahazi Asilia, CCK kufuata itikadi ya kijamaa ili waungane pamoja

Kwa wenye akili zilizopevuka,wanaelewa kabisa kwamba huyu zzk anaiga siasa kwa kufukiri atafanana na kina Mahattima Gandh n.k. Si Mara moja kujipambanua na kuidanganya nafsi yake kwamba yuko hivo.Kama hataki kugawana vyeo basis iweje alikwenda mahakamani na hadi leo analalamikia kuvuliwa nyadhifa ndani ya Chadema? Iweje zzk afike tu katika chama na kuwa CEO? Hivi kwa mini ametaka kuwa amirijeshi mkuu wa chama au hajui maana ya cheo chake? Asikwambie MTU huyu do go anataka kuwa juu ya kila mtu na kila kitu. Anataka yeye ndo aonekane siku zote.
 
Zitto apiga hodi Chadema










Mwandishi Wetu

Toleo la 403
29 Apr 2015










zitto_0.jpg






CHAMA cha ACT-Wazalendo kimeandika barua kwa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kikiomba kujua masharti ya kujiunga ili nacho kiwe sehemu yake, imefahamika.
Hata hivyo, wakati vyama vitatu miongoni mwa vinne vinavyounda umoja huo vikiwa tayari vimepelekewa barua hiyo, Raia Mwema limeambiwa kwamba vitatu vimepokea barua husika huku kimoja kikikataa kuipokea.
Kwa mujibu wa vyanzo vya gazeti hili, vyama ambavyo viliipokea barua ya ACT inayoongozwa na Naibu Katibu Mkuu wa zamani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Zitto Kabwe ni National League for Democracy (NLD), National Convention for Construction and Reform (NCCR-Mageuzi) na Chama cha Wananchi (CUF), huku Chadema kikidaiwa kutopokea barua hiyo.
Katibu Mkuu wa ACT, Maingu Samson Mwigamba, alilithibitishia gazeti hili kwamba chama chake kilituma barua ya kuomba kujiunga Ukawa Jumamosi iliyopita, Aprili 25, 2015, kwa vyama vyote vinavyounda Ukawa lakini ile iliyokwenda Chadema ilirudi.
“Ni kweli kwamba tuliandika barua kwenda kwa vyama vinne vinavyounda Ukawa. Malengo ya ile barua yalikuwa mawili; moja ni kueleza nia ya kutaka kujiunga na umoja huo na pili ni kuuliza ni taratibu zipi zinatakiwa kufuatwa kabla ya chama kuruhusiwa kujiunga na umoja huo.
“Hii ni kwa sababu, kama tulivyoeleza huko nyuma, sisi nia yetu ni kuunda upinzani ambao lengo lake kuu ni kuing’oa CCM madarakani. Tulipoeleza kuhusu nia yetu hiyo, wapo viongozi wa Ukawa waliosema kwamba tunatakiwa kuandika barua na tumefanya hivyo.
“Hata hivyo, barua ambazo watu wetu walipeleka katika ofisi za vyama vya NLD, NCCR na CUF zilipokewa na tulipata majibu lakini ile ya Chadema haikupokewa na ilirudishwa kwetu. Waliokataa kuzipokea hawakutoa sababu lakini nadhani katika watu wanne asipopokea mmoja si mbaya sana ili mradi tumetekeleza mojawapo ya matakwa ya kutaka kuingia Ukawa,” alisema.
Viongozi wote wa ngazi za juu wa Chadema akiwamo Mwenyekiti, Freeman Mbowe na manaibu wake, John Mnyika na Salum Mwalimu wako mikoani katika ziara mbalimbali za kisiasa zenye lengo la kujenga chama hicho.
Juhudi za kuwapata wote kuzungumzia suala hilo hazikuweza kufanikiwa hadi tunakwenda mitamboni juzi Jumatatu.
Ndani ya Ukawa
Wakati huo huo, gazeti hili limearifiwa kwamba viongozi wa juu wa Ukawa walikuwa wanatarajiwa kukutana Jumanne wiki hii, kwa kikao maalumu ambacho kazi yake kubwa ni kutafuta namna ya kukubaliana kuhusu mgombea mmoja wa urais wa Tanzania, katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.
Hadi sasa, Ukawa hawajakubaliana katika suala hilo huku karibu vyama vyote vinavyounda umoja, ukiondoa NLD vikiwa na viongozi wanaoweza kukubalika kuwania urais endapo watapitishwa.
Wafuasi wa CUF wanaamini kwamba Mwenyekiti wao, Profesa Ibrahim Lipumba, ndiye anayestahili kubeba bendera ya Ukawa kwenye uchaguzi huo kutokana na uzoefu wake katika jambo hilo, usomi wake pamoja na uwezo wake wa uongozi.
Chadema nao wanaamini kwamba Katibu Mkuu wake, Dk. Wilbrod Slaa, anatakiwa kubeba bendera ya Ukawa kwenye uchaguzi huo kutokana na wingi wa kura alioupata katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 ambao alipata kura nyingi kuliko mgombea yeyote wa nafasi hiyo kupitia upinzani, katika historia ya Tanzania.
Wiki iliyopita, NCCR - Mageuzi kupitia kwa Mkurugenzi wake wa Uchaguzi, Faustine Sungura, ilisema kwamba mgombea anayefaa kubeba bendera ya Ukawa ni Mwenyekiti wa chama hicho, Dk. George Kahangwa, kutokana na ujana wake, wakiweka sharti kwamba anayefaa ni yule aliyezaliwa baada ya Uhuru wa Tanganyika, Desemba 9, 1961. Dk. Kahangwa ni mhadhiri.
Ingawa hakusema moja kwa moja, kauli kwamba mgombea wa Ukawa anatakiwa kuwa amezaliwa baada ya Uhuru wa Tanganyika, yaani mwaka 1961, ilimaanisha kwamba Lipumba na Slaa ambao walizaliwa kabla, hawana sifa na Kahangwa, ambaye alizaliwa baada ya Uhuru, ndiye anayefaa.
Miongoni mwa changamoto kubwa ambazo Ukawa inakabiliana nazo kwenye nafasi hiyo ya urais ni ukweli kwamba kwa mujibu wa sheria zilizopo, chama kinachotoa mgombea urais ndicho hicho kinachotakiwa kutoa mgombea mwenza.
Hii maana yake ni kwamba, itabidi mojawapo ya vyama hivyo kikubali mmoja wa wanachama wake achukue kadi ya uanachama ya chama kingine ili awe na sifa ya kuwania na hadi sasa hakuna chama kilichoonyesha moja kwa moja dhamira ya kukubali chama chake kikose nafasi hiyo.
Kikwazo kingine cha Ukawa ni sheria za uchaguzi za Tanzania zinazotaka vyama vipate ruzuku kubwa kutokana na wingi wa kura ambazo mgombea wake wa ngazi ya urais na wabunge wamepata.
“Hii maana yake ni kwamba, kama Chadema kitatoa mgombea urais na si CUF au NCCR, maana yake ni kwamba wao watapata ruzuku kubwa zaidi baada ya uchaguzi na hivyo watakuwa na nguvu zaidi kuliko vyama vingine. Ni lazima itengenezwe namna ambayo mgawanyo huu wa ruzuku utakuwa sawia,” alisema mmoja wa viongozi wa CUF aliyezungumza na gazeti hili wiki kwa masharti ya kutotajwa jina kwa maelezo kuwa si msemaji wa chama hicho.
Raia Mwema limeelezwa kwamba kutokana na uzoefu kilioupata kwenye miaka ya nyuma wakati kilipokuwa hakisimamishi mgombea urais, NCCR – Mageuzi hakitakuwa tayari kurudia kosa hilo kwa kutokuwa na mgombea kwenye ngazi hiyo.

Source: Raia Mwema, 29.04.2015










 
Back
Top Bottom