ACT - Wazalendo waomba kujiunga na UKAWA

ACT - Wazalendo waomba kujiunga na UKAWA

Chama cha ACT-Wazalendo kimeandika barua kwa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi(UKAWA) kikiomba kujua masharti ya kujiunga ili nacho kiwe sehemu yake,imefahamika.

Katibu mkuu was ACT,Maingu Samson Mwigamba,alilithibitishia gazeti hili kwamba chama chake kilituma barua ya kuomba kujiunga UKAWA Jumamosi iliyopita,April 25,2015,kwa vyama vyote vinavyounda UKAWA lakini ile iliyokwenda CHADEMA ilirudi.

"Ni kweli kwamba tuliandika barua kwenda kwa vyama vinne vinavyounda UKAWA. Malengo ya ile barua yalikuwa mawili; moja ni kueleza nia ya kutaka kujiunga na umoja huo na pili ni kuuliza ni utaratibu zipi zinatakiwa kufuatwa kabla ya chama kuruhusiwa kujiunga na umoja huo..."

Chanzo: RAIA MWEMA 29/04/2015
1) Mwenyekiti wa ACT akiwa iringa aliwaambia wananchi na wanachama wake NI MARUFUKU KUSHABIKIA UKAWA.
2. ZITTO KABWE ALISEMA UKAWA NI WASAKA TONGE- kwa hiyo na yeye ni msaka tonge
3.mwigamba yeye akasema wataisambaratisha CUF mikoa ya pwani

Zitto baada ya kuona hali ni ngumu na hata ubunge hawezi kupata ameona mahala pa kujificha ni ukawa. pole sana wewe kijana uliona fedha za ccm tamu sasa zimeanza kuwa chungu
 
"Taifa limevimba. Wakulima Mahindi yanawaozea na Mpunga bei imeporomoka sababu ya mchele kutoka nje na usiolipiwa Kodi. Wahisani wamezuia misaada ( sababu ya kashfa ya #TegetaEscrow ) Kiasi Serikali haiwezi hata kujiendesha. Unapoona wanasiasa wanagawana vyeo katika nyakati kama hizi ujue Taifa halina Viongozi bali wasaka utawala. Wasaka utawala badala ya uongozi ni #WasakaTonge tu"

attachment.php
 
Usaliti unaanza kumtafuna taratibu sasa anataka kuungana na #WasakaTonge. UKAWA hatutafanya makosa ya kumkaribisha msaliti na wasaliti wenzie ambao nia na madhumuni yao makubwa ni kuisambaratisha CHADEMA. Wameona kuisambaratisha CHADEMA ni ndoto za alinacha sasa wanataka kuingia UKAWA ila wakavuruge mshikamano uliokuwepo. UKAWA hatutaki wasaliti wala hatutaki ayatullah.
 
Unajua tuwe wakweli.Ilitumwa na Kurudishwa na nani?

"...........Hats hivyo barua ambazo watu wetu walipeleka katika ofisi za vyama vya NLD,NCCR na CUF zilipokewa na tulipata majibu lakini ile ya Chadema haikupokewa na ilirudishwa kwetu...."

Ben huenda jamaa kaishiwa agenda kwa hiyo anatafuta agenda ya kuzungukia atakaoanza safari kwa mguu au train??
 
Usaliti unaanza kumtafuna taratibu sasa anataka kuungana na #WasakaTonge. UKAWA hatutafanya makosa ya kumkaribisha msaliti na wasaliti wenzie ambao nia na madhumuni yao makubwa ni kuisambaratisha CHADEMA. Wameona kuisambaratisha CHADEMA ni ndoto za alinacha sasa wanataka kuingia UKAWA ila wakavuruge mshikamano uliokuwepo. UKAWA hatutaki wasaliti wala hatutaki ayatullah.
Heshima yako umeandika ukweli kabisa Chadema hakuna nafasi za wasaliti kama ACT labda akaungane na wasaliti wenzake ccm.
 
nyie ndio mnaosema chadema wanaweweseka wanawaogopa inakuaje muombe kuwa nao ?
UKAWA SIO KWA AJILI YA WACHUMIA TUMBO
 
Back
Top Bottom