Inatia shaka kama Watanzania tunajua tulifanyalo.Wakati tunatakiwa kuimarisha upinzani,siye tumekaa kuupiga vita kwa sababu tu ya pesa ndogo za mafisadi.Hivi itatusaidia nini kupokea nipande thelathini vya dhahabu halafu jioni unajinyonga?Majangili,mafisadi,na wala rushwa pamoja na wanaoitwa wawekezaji watazidi kutumaliza na sisi tunawapigia makofi.Inatia hasira na uchungu,halafu wengine wamebaki kuingilia maisha ya watu,Udini,ukabila,ukanda na matusi.
Na mbaya zaidi wanaoanza matusi wakitukanwa wanalamika kwa nini unatukana.Hivi kun faida gani kumuita mtu mwingine mwenye maisha yake MALAYA,na wewe unaita mwenzio MALAYA unausafi gani?
Wanasema hivi...'Usihukumu uisje ukahukumiwa"Tuache tabia chafu za kuchafuana ,tujenge argument zetu kwa hoja tuache kutukana watu haina faida.Tukianza kuwachunguza viongozi wetu wote bila kujali vyama tunaweza kukata tamaa.