Academics &Professional CV ya Deogratius Nalimi Kisandu

Academics &Professional CV ya Deogratius Nalimi Kisandu

Unapodeal na watu dizaini ya Deo humu kwenye mitandao inabidi uwe na umakini wa ziada
 
Kwahiyo unataka tufanyeje CV yenyewe ya kuunga unga?

You are putting yourself under the firing squad halafu unakuja kwa ID nyingine kulalamika umenyanyapaliwa. Nini kimekuvuruga haswa?
 
What is going on mr.kisandu
But cv yako iko vzr ingawaje badoo kjn big up bro.kisandu shadaut to mkolani high school love it soo much
 
Hii ndio Biograph ya Deogratius Kisandu.

Kuzaliwa: 28 Juni 1980. Siku ya Jumamosi.

1990-1994: Shule ya msingi Sunge, kata ya Busoka, Kahama, Shinyanga. Darasa la i-v.

1995-1996: Shule la msingi kahama, kahama, Shinyanga. Darasa la vi-vii.

1997: Kidato cha kwanza, Magu sekondari, Magu, Mwanza.(Evening Class-ODL).Niliishia Form one tu.

July 1998-April 1999: Mtawa shirika la Ndugu wadogo wa Afrika, Morogoro. Niliishia hatua ya Uaspiranti tu(Utakaji) hivyo sikutunukiwa cheti zaidi ya Kitambulisho.


April 1999-2002: Form i-iv, Kishimba sekondari, Kahama, Shinyanga.(Evening classes-ODL).

Desemba 2002-2003: ASTASHAHADA ya Uandishi wa habari, Chuo cha Royal College of Journalism, Dar es Salaàm.

2004: Mwandishi wa habari wa kujitegemea.

2007: Ku attend mtihani wa Kidato cha sita katika kituo cha kufanyia mtihani cha sekondari ya wasichana Tabora.(Cheti cha kidato cha sita)

April 2007-Juni 2007: Induction course for secondary school Teachers, Chuo cha ualimu Tabora(Leseni ya kufundishia 2007-2012).

2007-2012: Mwalimu, Shule ya sekondari Mwamala, Nzega, Tabora.

2008: Kurudia mtihani wa kidato cha sita (resitter), Kahama sekondari.

2008: Msimamizi Mkuu, mtihani kidato cha Pili, Mogwa sekondari, Nzenga.

April 2009: Msahihishaji wa Mitihani ya Mock kidato cha NNE, kanda ya Magharibi, Tabora.(Somo la kiswahili).

2009-2012: Shahada ya Elimu Maalum(Ndani yake nimesoma Political Science and Public Administration), Chuo Kikuu kishiriki cha Tumaini Makumira cha Sebastian Kolowa(SEKUCo), kwasasa SEKOMU.

2013 up to date: Mwalimu, Shule ya sekondari Mkolani, Mwanza.

2013: Mafunzo maalum ya Gesi asilia na madini, Mwanza, TEITI.

2014: Muwezeshaji Kongamano la KATIBA Mpya, Mwanza.

April 2014: Mafunzo maalum ya mahusiano ya Ndoa na Uchumba, JRC, Mwanza.

2016: Semina ya kusimamia mtihani na kusahisha kidato cha sita, Mwanza.

2016: Msimamizi wa mitihani kidato cha sita, Ngaza sekondari, Mwanza.

2016: Mafunzo maalum ya Imani Takatifu ndani ya Kanisa Katoliki(KATEKESI), Mwanza.

2012-2016: Nimeshiriki semina zote za JUKWAA LA KATIBA kupitia taasisi yetu ya JUKWAA la Mwalimu na Wanafunzi Tanzania (Teachers and Students Forum Tanzania).

Niliposahau nitaleta mwendelezo,

Wenu wa karibu:

Deogratius Nalimi Kisandu.
Tunalaumu watoto wetu bure baada ya kufeli.We nawe ni mwl wa sekondary kwa induction course ya wiki 8 na unasaihihisha mitihani ya A level.Naona nitakuwa mwehu badala yako nikiendelea kutafakari cv yako.
 
Deogratratius Nalimi Kisandu mbona familia yenu yote mlikuwa CCM,miaka na miaka kipi kilichokupeleka upinzani.
 
Deo nimetokea kukubali kila thread yako lazima niifungue nione jinsi gani binadamu tuko diverse especially kwenye kufikiria
 
Sijaelewa lengo la CV yake ni nini? Ila nilikiona vijana wanafeli kwa kusahihishwa na watu kama hawa. Kaunga unga shule harafu anakuja kusahihisha mtihani wa form six. Kama point ni 6 kufuatana na marking scheme alipewa we ya kwanza umeweka ya sita utafeli. Nakumbuka kipindi nikiwa darasa la 3 tunasahihishwa na darasa LA 7
 
Ulizaliwa 1980 na 2015 ulitaka kugombea urais..

Kazi kwelikweli!
 
Back
Top Bottom