Abiria wa Precision Air, Walazimishwa kuacha mizigo Mwanza kwamba ndege imejaa

dubu

JF-Expert Member
Oct 18, 2011
3,496
3,461
Mwanza: Wasafiri ya Ndege ya Precision Air, Wakatazwa kupanda na mizigo yao kwa sababu ya ndege kujaa sana na haina uwezo kwa sababu za kiufundi

Kitendo hicho kimewatia wasiwasi wasafiri wa ndege hiyo ambao imechukua masaa mawili hadi kukubali kupanda ndege hiyo ambayo walitaka maelezo ya kina kwa kuhofia usalama wao.

"Kama ndege inashindwa kubeba mizigo ya kawaida itakuaje usalama wa watu?" alihoji moja ya abiria wa ndege hiyo.

Mamlaka pamoja na kuwakataza kupiga picha wala kuchukua Video kuhusiana na tukio hilo, imewaambia mizigo yao ibaki hapo uwanjani itasafirishwa kwa ndege nyingine.

Hadi sasa hakuna taarifa rasmi kutoka kwa Wasimamizi wa safari wala Mamlaka husika ili kujua nini hasa kimefanya watu waache mizigo yao kinyume na taratibu au mazoea.

Namba za ndege ni 5H-PWG ambayo operator wake ni Precision Air. Aircraft ni ATR 72-500, type code ni AT75. Safari ilikuwa Mwanza kwenda Dar.
 
TCAA muanze kuwa makini kwakweli hizi si dalili nzuri
Vinginevyo oneni jinsi mnaweza wasaidia hawa watu
 
Binafsi nawapongeza precision Kwa kuchukua tahadhari mapema...

Wakichukua tahadhari tunalalamika ........

Likitokea la kutokea tunalalamika zaidi ....
sijui tunataka nini aisee🙌 Nature yetu waTz ni kulalamika kweli aloo....🙌
 
Hili shirika la ndege la Precission air kuna haja yakuangaliwa kwa jicho kali maana siku za karibuni limekuwa na matukio yenye kuleta shaka..

Tusisubiri majanga maana kwa hizi trends maana yake kiusalama ni kitu kikubwa kinakuja.....

Serikali iangalie issue za maintenance operations na safety kwenye hili shirika kwa akili yangu nahisi kuna shida kubwa na mambo mengi ni kienyeji na mazoea.
 
Shirika hili kwa sasa nadhani lina ndege kuukuu sana.Mamlaka ya anga ongezeni safari za anga kwa airTanzania,au waiteni wale jamaa wa 70,000/=
 
Binafsi nawapongeza precision Kwa kuchukua tahadhari mapema...

Wakichukua tahadhari tunalalamika ........

Likitokea la kutokea tunalalamika zaidi ....
sijui tunataka nini aisee🙌 Nature yetu waTz ni kulalamika kweli aloo....🙌
Ndo useme ndege haina uwezo kwa sababu za Kiufundi? Ndege inajaa sana kwani kuna wasafiri wanakosa viti kwamba wanasimama?
 
Mwanza: Wasafiri ya Ndege ya Precision Air, Wakatazwa kupanda na mizigo yao kwa sababu ya ndege kujaa sana na haina uwezo kwa sababu za kiufundi

Kitendo hicho kimewatia wasiwasi wasafiri wa ndege hiyo ambao imechukua masaa mawili hadi kukubali kupanda ndege hiyo ambayo walitaka maelezo ya kina kwa kuhofia usalama wao.

"Kama ndege inashindwa kubeba mizigo ya kawaida itakuaje usalama wa watu?" alihoji moja ya abiria wa ndege hiyo.

Mamlaka pamoja na kuwakataza kupiga picha wala kuchukua Video kuhusiana na tukio hilo, imewaambia mizigo yao ibaki hapo uwanjani itasafirishwa kwa ndege nyingine.

Hadi sasa hakuna taarifa rasmi kutoka kwa Wasimamizi wa safari wala Mamlaka husika ili kujua nini hasa kimefanya watu waache mizigo yao kinyume na taratibu au mazoea.

Namba za ndege ni 5H-PWG ambayo operator wake ni Precision Air. Aircraft ni ATR 72-500, type code ni AT75. Safari ilikuwa Mwanza kwenda Dar.
View attachment 2522990
Kwanini watu wanataka kupanda ndege hiyo.
 
Shirika lina changamoto ya ukwasi ambayo inapelekea hata maintance ya ndege iwe changamoto nyingine. Waiting for the investigation report on their aircraft which dived in the lake Victoria and killed a number of people.
 
Mwanza: Wasafiri ya Ndege ya Precision Air, Wakatazwa kupanda na mizigo yao kwa sababu ya ndege kujaa sana na haina uwezo kwa sababu za kiufundi

Kitendo hicho kimewatia wasiwasi wasafiri wa ndege hiyo ambao imechukua masaa mawili hadi kukubali kupanda ndege hiyo ambayo walitaka maelezo ya kina kwa kuhofia usalama wao.

"Kama ndege inashindwa kubeba mizigo ya kawaida itakuaje usalama wa watu?" alihoji moja ya abiria wa ndege hiyo.

Mamlaka pamoja na kuwakataza kupiga picha wala kuchukua Video kuhusiana na tukio hilo, imewaambia mizigo yao ibaki hapo uwanjani itasafirishwa kwa ndege nyingine.

Hadi sasa hakuna taarifa rasmi kutoka kwa Wasimamizi wa safari wala Mamlaka husika ili kujua nini hasa kimefanya watu waache mizigo yao kinyume na taratibu au mazoea.

Namba za ndege ni 5H-PWG ambayo operator wake ni Precision Air. Aircraft ni ATR 72-500, type code ni AT75. Safari ilikuwa Mwanza kwenda Dar.
View attachment 2522990
Serikali inasubiri nini kusitisha safari za precision kubeba abria?ndani ya tanzania?
 
Ndo useme ndege haina uwezo kwa sababu za Kiufundi? Ndege inajaa sana kwani kuna wasafiri wanakosa viti kwamba wanasimama?

nyie tangulieni Tu na hiyo ndege nyingine mfike salama mshkuru Mungu mkuu..
hiyo mizigo mkaingoje huko huko iletwe.

Note: sijawah panda ndege ila uhai muhimu.
 
nadhani mamlaka husika zianze kuchukua hatua mapema kabla hatujapata madhara makubwa, hawa precision air wana matatizo maana hata ndege iliyokuwa iondoke saa 17:45 toka dar es salaam kuelekea kilimanjaro ndiyo inaondoka muda huu baada ya abiria kufaulishwa kwenye ndege inayoelekea nairobi.
 
Back
Top Bottom