A living reincarnation, rebirth..!

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,606
696,720
Nimeshindwa kupata neno zuri la kichwa cha habari kitakachoendana na maudhui hivyo nimeamua kutumia hicho cha kiingereza.... Naomba radhi kwa watakaokwazika...!!!


Kabla sijaendelea naomba nitoe tafsiri ya reincarnation lakini pia nitoe na tafsiri ya rebirth (hizi zote kwa kiswahili ni kuzaliwa tena, ama kuzaliwa mara ya pili)

REINCARNATION ni mchakato wa kuzaliwa tena katika umbo la kiumbe hai kingine kutokana na matendo yako ya nyuma baada ya kufa.... Hii wanaitumia sana waamini wasioamini katika Mungu mmoja bali miungu... Kwao hakuna neno MSAMAHA... ukitenda baya utalipwa baya... Ukitenda jema utalipwa jema... Na hii hutokea ukiwa hai ama ukizaliwa TENA....!!!

REBIRTH ni mchakato wa kuzaliwa mara ya PILI lakini katika mwili ule ule ila likiwa ni tendo la kiroho zaidi... Hii hutumiwa sana na waamini wanaoamini katika Mungu mmoja na maisha ya peponi baada ya kifo kama ukitubu na maisha ya jehanum kama usipotubu na kuungama madhambi yako... Rebirth ni tendo la kuokoka kiroho....

Yote kwa yote kuna mstari mwembamba sana kati ya tafsiri hizi mbili rebirth na reincarnation... Moja ikiwa ni kuzaliwa tena na nyingine ikiwa ni kuzaliwa mara ya pili.... Moja ikiwa ni tendo la kiroho zaidi na nyingine ikiwa ni tendo la kimwili pamoja na kiroho... Mfanano wao ni kwamba zote ni imani!

Turejee kwenye mada yetu sasa..

Kuna usemi maarufu duniani kuwa dunia wawili wawili... Kwamba kuna watu wa kaliba tofauti kabisa.. Nchi tofauti kabisa au maeneo tofauti kabisa lakini wamefanana kama mayai... Naamini umeshawahi kusikia mtu akikwambia kuwa nimemuona mtu anafanana na wewe kabisa... Hii ndio living reincarnation ninayotaka kuijadili hapa

Swala la matunzo ya watoto waliotelekezwa na wazazi wa kiume pamoja na kwamba limekuwa la kisiasa zaidi.. Lakini kiroho lina tafsiri yake pana sana... Tafsiri ya kwamba hapa duniani sura yako si yako pekee mtatofautiana vingine kama kabila umri eneo nk lakini sura ni ile ile.... Kitendo kilichofanywa na baadhi kutaka kuthibitisha madai yao ni kuweka sura za watoto na wababa wanaotuhumiwa kuwa hao ni watoto wao....

Hiki ni kichekesho kwakuwa wengi hawajui kuhusu living reincarnation or rather rebirth... Kwamba kipimo pekee kinachoweza kuthibitisha uhusiano wa mzazi wa kiume na mtoto ni kipimo cha kupima damu cha DNA....!!! hiki ndio kipimo pekee chenye majibu sahihi vingine vyote ni vya kufikirika na kuhisi zaidi kuliko uhalisia....

Lakini vile vile ni mara ngapi huwa tunahisi kuwa sehemu ambayo wala hatujawahi kufika... Saa nyingine tumeona kwenye luninga, gazeti au mitandaoni... Au unafika mahali kwa mara ya kwanza lakini unakuwa na hisia kamili kuwa hapo mahali unapafahamu..

Roho zetu ni kitu kikubwa mno na kilicho huru.. Ni roho zetu hizi hutuhama nje ya ufahamu wetu na kwenda kuzurura kwenye ulimwengu wa roho na hata kuweza kuingia kwenye majumba roho ya mili mingine ama kupita sehemu ambazo hubeba kumbukumbu zake na kurudi nazo kwenye mwili asili..

Kumbukumbu hizo zikihifadhiwa kwenye ubongo hubaki na kutengeneza picha ya uhalisia usio timilifu... Hii hali hupelekea yafuatayo;
  • Kukutana na mtu kwa mara ya kwanza lakini unahis kabisa si mara yenu ya kwanza kukutana.. Basi huishia kusema tu nimekufananisha.
  • Kufika eneo kwa mara ya kwanza lakini ukiwa na fikra kuwa si mara ya kwanza... Jua roho ilikutoroka na kwenda yenyewe.
  • Kufananishwa na mtu ambaye hamfahamiani kabisa na mko mbalimbali
  • Kuwa na fikra ya kukaribia kutokea kitu fulani ambacho kiuhalisia hakijawahi kukutokea
  • Kufanya kitu kipya kabisa huku fikra zikikukumbusha kukifanya kitu hichohicho lakini bila kumbukumbu kamili
Ulimwengu wa roho ni timilifu na huweza kufanya vitu nje ya utashi wa kawaida wa binadamu na kutuletea Kumbukumbu zisisotimia.... Na hii ndio living reincarnation au living rebirth katika uhalisia wake..

Mimi sina mtoto wa kusingiziwa.... Mkioneshwa yeyote tunafanana hata vitabia jueni tu ya kwamba hiyo ni michezo ya roho katika kuvinjari kwake!
 
Haya mambo sometime ukiyafatilia Na kama una
Stress za Barcelona or Madrid huwez elewa
Pia ukisema uko centratt kwenye haya mambo ukiwa Na mawazo ya madereva Na Makonda
Unaweza changanyikiwa
 
Inaweza kuwa kweli kuna kipindi nikiwa secondary mwalimu aliuliza swali akampoint mtu wa kwanza akashidwa kujibu, akampoint wa pili ghafla nikakumbuka ni kama kitu kimewahi kutokea nikamwambia rafiki yangu pembeni akitoka huyo atamuuliza mdada flani then ataishia kwangu na kweli ilitokea hivyo, Jamaa alishangaa sana nimejuaje.
Hiyo hali mpaka leo ninayo ya kuhisi kitu flani kilishatokea kitatokea hapa na kikatokea kweli.
 
Bora mimi simfuatilii huyo Bashite maana ningechanganya mambo hapa
Limetokea kwa sababu... Tunaweza kuliangalia kwa jicho la kisiasa lakini hili ni la kiroho na limetokea kwa sababu zake, kwa muda wake na kwa maana yake.... Kwakuwa tumefumbwa ufahamu ni ngumu kujua yajayo lakini hitimisho linaweza kukupa mrejesho wa kushangaza sana
 
Limetokea kwa sababu... Tunaweza kuliangalia kwa jicho la kisiasa lakini hili ni la kiroho na limetokea kwa sababu zake, kwa muda wake na kwa maana yake.... Kwakuwa tumefumbwa ufahamu ni ngumu kujua yajayo lakini hitimisho linaweza kukupa mrejesho wa kushangaza sana
Nakuelewaga sana

Avache
 
Inaweza kuwa kweli kuna kipindi nikiwa secondary mwalimu aliuliza swali akampoint mtu wa kwanza akashidwa kujibu, akampoint wa pili ghafla nikakumbuka ni kama kitu kimewahi kutokea nikamwambia rafiki yangu pembeni akitoka huyo atamuuliza mdada flani then ataishia kwangu na kweli ilitokea hivyo, Jamaa alishangaa sana nimejuaje.
Hiyo hali mpaka leo ninayo ya kuhisi kitu flani kilishatokea kitatokea hapa na kikatokea kweli.
Kuna baadhi ya taarifa na kumbukumbu huanzia ndotoni usiku.. Unaletewa picha kamili jinsi kitu kitakavyotokea... Hapa machale pia huingilia maamuzi
Unajiona kabisa ukinusurika ajali ama Ukipata ajali na kuumia ama kupoteza vitu vyako... Unayaona yajayo live... Halafu kuna roho inakwambia nenda tu utapata ajali lakini hutaumia au nyingine inakukataza kabisa usiende.. Ukikaidi.......!!!!!
 
Tunapata ujumbe gani hapa!? Angalia kushoto kuna nini na kulia kuna nini... Angalia chini kuna nini... Vipi kuhusu juu!?
Tukijaaliwa kuamka salama.... Tukutane kwa ajili ya uchambuzi na ufafanuzi wa kina zaidi.... Dhana ya kuzaliwa tena na kuzaliwa mara ya pili... Dhana ya kumbukumbu ya mahali tusipowahi kufika kabla na matukio yake.... Dhana ya kufanana na kufananishwa
Reincarnation_746_460_80_c1.jpg
IMG-20180411-WA0077.jpg
 
Kuhama kwa roho tukiwa usingizini usiku ni jambo la kawaida (temporal shift) na roho huenda kutangatanga huko na huko na hatimaye kurejea mwilini salama.. Kipindi chote hiki. Mwili unakuwa kwenye hali tuli (dormance state) lakini pia roho huhama hata wakati mwili ukiwa live (partial discharge) na kuwa na uwezo wa kujigawa huku unakotoka na kule uendako!

Hujawahi kupata hali hii!? Au hujawahi kusikia wengine wakimuuliza mtu hivi wewe leo ukoje! Ama hujawahi kusikia mtu akisema mbona kama sijielewi elewi!? Mbona kama sio mimi!?

Ni katika kipindi hiki ujue roho yako haiko kamili nawe na kuna mahali inafanya kolabo
Ni kolabo hii huzalisha mfanano wa kisura ama hata kitabia... Na ndio maana kuna watu hufanya vitu nasi kuishia kusema kuwa ile haikuwa akili yake..

Tunamjua vema ile haikuwa akili yake... Ama wewe mwenyewe kuishia kujilaumu kwa kitu kibaya ama cha kipuuzi ulichofanya kwa kusema kuwa haikuwa akili yako
 

Similar Discussions

26 Reactions
Reply
Back
Top Bottom