A living reincarnation, rebirth..!

Mkuu hiyo ni kweli kabisa kwani kwa watu wengine unakuta anafanya kitu lakini anahisi kama hichi kitu amewahi kufanya japo hawezi kukumbuka ni wapi na ni lini japo ni kweli au mwingine roho yake inatoroka na kwenda kwenye matukio ya mbele na kuhifadhi kumbukumbu na baada ya muda yale matukio yanatokea vilevile kwa wale ambao tumeangalia filamu ya final destination tunafahamu hili.
 
Kuna ushuhuda wa dada mmoja hivi ni waajabu sana, huko youtu.

Anasema yeye alizaliwa mwaka 1991, ila hakuishi sana akafa akiwa mtoto, anasema kimwili alikufa ila kiroho alikuwa hajafa kwani alikuwa huko kuzimu. Mwaka 2001 alizaliwa tena duniani ila katika familia nyingine ambayo ndio yuko mpaka sasa.
Sijui hii imekaaje.
 
Kuna ushuhuda wa dada mmoja hivi ni waajabu sana, huko youtu.

Anasema yeye alizaliwa mwaka 1991, ila hakuishi sana akafa akiwa mtoto, anasema kimwili alikufa ila kiroho alikuwa hajafa kwani alikuwa huko kuzimu. Mwaka 2001 alizaliwa tena duniani ila katika familia nyingine ambayo ndio yuko mpaka sasa.
Sijui hii imekaaje.
Living from future... Zipo kesi chache mno lakini zisizo na ithibati za kisayansi zaidi ya shuhuda binafsi kwakuwa ni mambo ya kiroho zaidi
 
Sasa mkuu hayo uliyo ongelea hapo kuna moja huwa linanitokea sana, la kufananishwa na watu kila nitakapokwenda nakua sielewi kama kuna kitu kimejificha ama vp.Je kutokana na kuwa katika hali hiyo vp kuna effect yoyte inaweza kutokea na kuniathiri kimwili au kiroho na katika maisha kiujumla
Nimeshindwa kupata neno zuri la kichwa cha habari kitakachoendana na maudhui hivyo nimeamua kutumia hicho cha kiingereza.... Naomba radhi kwa watakaokwazika...!!!


Kabla sijaendelea naomba nitoe tafsiri ya reincarnation lakini pia nitoe na tafsiri ya rebirth (hizi zote kwa kiswahili ni kuzaliwa tena, ama kuzaliwa mara ya pili)

REINCARNATION ni mchakato wa kuzaliwa tena katika umbo la kiumbe hai kingine kutokana na matendo yako ya nyuma baada ya kufa.... Hii wanaitumia sana waamini wasioamini katika Mungu mmoja bali miungu... Kwao hakuna neno MSAMAHA... ukitenda baya utalipwa baya... Ukitenda jema utalipwa jema... Na hii hutokea ukiwa hai ama ukizaliwa TENA....!!!

REBIRTH ni mchakato wa kuzaliwa mara ya PILI lakini katika mwili ule ule ila likiwa ni tendo la kiroho zaidi... Hii hutumiwa sana na waamini wanaoamini katika Mungu mmoja na maisha ya peponi baada ya kifo kama ukitubu na maisha ya jehanum kama usipotubu na kuungama madhambi yako... Rebirth ni tendo la kuokoka kiroho....

Yote kwa yote kuna mstari mwembamba sana kati ya tafsiri hizi mbili rebirth na reincarnation... Moja ikiwa ni kuzaliwa tena na nyingine ikiwa ni kuzaliwa mara ya pili.... Moja ikiwa ni tendo la kiroho zaidi na nyingine ikiwa ni tendo la kimwili pamoja na kiroho... Mfanano wao ni kwamba zote ni imani!

Turejee kwenye mada yetu sasa..

Kuna usemi maarufu duniani kuwa dunia wawili wawili... Kwamba kuna watu wa kaliba tofauti kabisa.. Nchi tofauti kabisa au maeneo tofauti kabisa lakini wamefanana kama mayai... Naamini umeshawahi kusikia mtu akikwambia kuwa nimemuona mtu anafanana na wewe kabisa... Hii ndio living reincarnation ninayotaka kuijadili hapa

Swala la matunzo ya watoto waliotelekezwa na wazazi wa kiume pamoja na kwamba limekuwa la kisiasa zaidi.. Lakini kiroho lina tafsiri yake pana sana... Tafsiri ya kwamba hapa duniani sura yako si yako pekee mtatofautiana vingine kama kabila umri eneo nk lakini sura ni ile ile.... Kitendo kilichofanywa na baadhi kutaka kuthibitisha madai yao ni kuweka sura za watoto na wababa wanaotuhumiwa kuwa hao ni watoto wao....

Hiki ni kichekesho kwakuwa wengi hawajui kuhusu living reincarnation or rather rebirth... Kwamba kipimo pekee kinachoweza kuthibitisha uhusiano wa mzazi wa kiume na mtoto ni kipimo cha kupima damu cha DNA....!!! hiki ndio kipimo pekee chenye majibu sahihi vingine vyote ni vya kufikirika na kuhisi zaidi kuliko uhalisia....

Lakini vile vile ni mara ngapi huwa tunahisi kuwa sehemu ambayo wala hatujawahi kufika... Saa nyingine tumeona kwenye luninga, gazeti au mitandaoni... Au unafika mahali kwa mara ya kwanza lakini unakuwa na hisia kamili kuwa hapo mahali unapafahamu..

Roho zetu ni kitu kikubwa mno na kilicho huru.. Ni roho zetu hizi hutuhama nje ya ufahamu wetu na kwenda kuzurura kwenye ulimwengu wa roho na hata kuweza kuingia kwenye majumba roho ya mili mingine ama kupita sehemu ambazo hubeba kumbukumbu zake na kurudi nazo kwenye mwili asili..

Kumbukumbu hizo zikihifadhiwa kwenye ubongo hubaki na kutengeneza picha ya uhalisia usio timilifu... Hii hali hupelekea yafuatayo;
  • Kukutana na mtu kwa mara ya kwanza lakini unahis kabisa si mara yenu ya kwanza kukutana.. Basi huishia kusema tu nimekufananisha.
  • Kufika eneo kwa mara ya kwanza lakini ukiwa na fikra kuwa si mara ya kwanza... Jua roho ilikutoroka na kwenda yenyewe.
  • Kufananishwa na mtu ambaye hamfahamiani kabisa na mko mbalimbali
  • Kuwa na fikra ya kukaribia kutokea kitu fulani ambacho kiuhalisia hakijawahi kukutokea
  • Kufanya kitu kipya kabisa huku fikra zikikukumbusha kukifanya kitu hichohicho lakini bila kumbukumbu kamili
Ulimwengu wa roho ni timilifu na huweza kufanya vitu nje ya utashi wa kawaida wa binadamu na kutuletea Kumbukumbu zisisotimia.... Na hii ndio living reincarnation au living rebirth katika uhalisia wake..

Mimi sina mtoto wa kusingiziwa.... Mkioneshwa yeyote tunafanana hata vitabia jueni tu ya kwamba hiyo ni michezo ya roho katika kuvinjari kwake!
 
Sasa mkuu hayo uliyo ongelea hapo kuna moja huwa linanitokea sana, la kufananishwa na watu kila nitakapokwenda nakua sielewi kama kuna kitu kimejificha ama vp.Je kutokana na kuwa katika hali hiyo vp kuna effect yoyte inaweza kutokea na kuniathiri kimwili au kiroho na katika maisha kiujumla
Kiroho hapana ila kimwili ni kama ikatokea hali ukafananishwa na mhalifu fulani ama mtu aliyefanya tukio mahali.... Marekani kuna kesi moja jamaa alifungwa kifungo kirefu kumbe alifananishwa na ikatokea alikuwa sehemu ya tukio
 
.
1.jpeg


Jr
 
Mkuu sipo deep sanaaa katika maswala ya neuroscience ila nitakujibu kadiri ya uwezo wangu ni kuwa katika ubongo kuna system(mfumo) maalum unaohusika katika maswala ya kumbukumbu ambayo kiujumla huitwa LIMBIC SYSTEM ambapo katika lymbic system kumegawanyika sehemu nyingi ila mfano wa hizo ni ( olfactory bulbs, hippocampus, amygdala, anterior thalamic nuclei, fornix n.k) sehemu hizi kama ilivyo kawaida zina mfumo wa neurone kama tunavyojua ubongo una neurons nyingi ambazo zenyewe ndo huwa kama njia ya kusafiririsha tarifa kwa njia ya umeme(electrical impulse) sasa turudi kwenye swali lako ni kuwa katika mfumo huo wa kumbu kumbu huwa kuna kitu wanakiita sensory processor (mchanganuo hisishi) ambao wenyewe huwa unapokea taarifa kwa mfumo wa kemikali(chemicals) au physical vibrations (mawimbi mtikiso) yaani utakapoona tukio ili lihifadhiwe na kwa kumbu kumbu basi mfumo huo utapokea either mabadiliko ya ki kemikali eneo hilo au utapokea mtikisiko maalum ambao utahifadhiwa kipawa chake katika hyppocampus na baada ya hapo kama utakuja kuona tukio hilo hilo basi tukio hilo husababisha utumwaji wa taarifa kama ya awali yenye kipimo (intesity) sawa na kile cha awali basi hapo ubongo wako huweza kupima kiwango cha taarifa kama ni sawa na kile cha awali hii husababisha wewe kupata kumbukumbu:
Mimi ndo hujua hivyo mkuu kwa hiyo kumbu kumbu si invisible bali ni STIMULI ambayo inahifadhiwa kwa mfumo wa chemical change au physical vibrations kwenye ubongo .
Tukimaliza kwenye kumbukumbu,bado tutahoji tena kuwa roho haina sehemu ya kuhifadhi kumbukumbu,iweje basi iwe na macho ya kuona inapoenda....ndipo nitafikia uamuzi wa kusema roho ni roho yenye kila kitu ndani yake
 
Tukimaliza kwenye kumbukumbu,bado tutahoji tena kuwa roho haina sehemu ya kuhifadhi kumbukumbu,iweje basi iwe na macho ya kuona inapoenda....ndipo nitafikia uamuzi wa kusema roho ni roho yenye kila kitu ndani yake
Baada ya roho kutengana na mwili huondoka na memory stick ya ubongo

Jr
 
Nimeshindwa kupata neno zuri la kichwa cha habari kitakachoendana na maudhui hivyo nimeamua kutumia hicho cha kiingereza.... Naomba radhi kwa watakaokwazika...!!!


Kabla sijaendelea naomba nitoe tafsiri ya reincarnation lakini pia nitoe na tafsiri ya rebirth (hizi zote kwa kiswahili ni kuzaliwa tena, ama kuzaliwa mara ya pili)

REINCARNATION ni mchakato wa kuzaliwa tena katika umbo la kiumbe hai kingine kutokana na matendo yako ya nyuma baada ya kufa.... Hii wanaitumia sana waamini wasioamini katika Mungu mmoja bali miungu... Kwao hakuna neno MSAMAHA... ukitenda baya utalipwa baya... Ukitenda jema utalipwa jema... Na hii hutokea ukiwa hai ama ukizaliwa TENA....!!!

REBIRTH ni mchakato wa kuzaliwa mara ya PILI lakini katika mwili ule ule ila likiwa ni tendo la kiroho zaidi... Hii hutumiwa sana na waamini wanaoamini katika Mungu mmoja na maisha ya peponi baada ya kifo kama ukitubu na maisha ya jehanum kama usipotubu na kuungama madhambi yako... Rebirth ni tendo la kuokoka kiroho....

Yote kwa yote kuna mstari mwembamba sana kati ya tafsiri hizi mbili rebirth na reincarnation... Moja ikiwa ni kuzaliwa tena na nyingine ikiwa ni kuzaliwa mara ya pili.... Moja ikiwa ni tendo la kiroho zaidi na nyingine ikiwa ni tendo la kimwili pamoja na kiroho... Mfanano wao ni kwamba zote ni imani!

Turejee kwenye mada yetu sasa..

Kuna usemi maarufu duniani kuwa dunia wawili wawili... Kwamba kuna watu wa kaliba tofauti kabisa.. Nchi tofauti kabisa au maeneo tofauti kabisa lakini wamefanana kama mayai... Naamini umeshawahi kusikia mtu akikwambia kuwa nimemuona mtu anafanana na wewe kabisa... Hii ndio living reincarnation ninayotaka kuijadili hapa

Swala la matunzo ya watoto waliotelekezwa na wazazi wa kiume pamoja na kwamba limekuwa la kisiasa zaidi.. Lakini kiroho lina tafsiri yake pana sana... Tafsiri ya kwamba hapa duniani sura yako si yako pekee mtatofautiana vingine kama kabila umri eneo nk lakini sura ni ile ile.... Kitendo kilichofanywa na baadhi kutaka kuthibitisha madai yao ni kuweka sura za watoto na wababa wanaotuhumiwa kuwa hao ni watoto wao....

Hiki ni kichekesho kwakuwa wengi hawajui kuhusu living reincarnation or rather rebirth... Kwamba kipimo pekee kinachoweza kuthibitisha uhusiano wa mzazi wa kiume na mtoto ni kipimo cha kupima damu cha DNA....!!! hiki ndio kipimo pekee chenye majibu sahihi vingine vyote ni vya kufikirika na kuhisi zaidi kuliko uhalisia....

Lakini vile vile ni mara ngapi huwa tunahisi kuwa sehemu ambayo wala hatujawahi kufika... Saa nyingine tumeona kwenye luninga, gazeti au mitandaoni... Au unafika mahali kwa mara ya kwanza lakini unakuwa na hisia kamili kuwa hapo mahali unapafahamu..

Roho zetu ni kitu kikubwa mno na kilicho huru.. Ni roho zetu hizi hutuhama nje ya ufahamu wetu na kwenda kuzurura kwenye ulimwengu wa roho na hata kuweza kuingia kwenye majumba roho ya mili mingine ama kupita sehemu ambazo hubeba kumbukumbu zake na kurudi nazo kwenye mwili asili..

Kumbukumbu hizo zikihifadhiwa kwenye ubongo hubaki na kutengeneza picha ya uhalisia usio timilifu... Hii hali hupelekea yafuatayo;
  • Kukutana na mtu kwa mara ya kwanza lakini unahis kabisa si mara yenu ya kwanza kukutana.. Basi huishia kusema tu nimekufananisha.
  • Kufika eneo kwa mara ya kwanza lakini ukiwa na fikra kuwa si mara ya kwanza... Jua roho ilikutoroka na kwenda yenyewe.
  • Kufananishwa na mtu ambaye hamfahamiani kabisa na mko mbalimbali
  • Kuwa na fikra ya kukaribia kutokea kitu fulani ambacho kiuhalisia hakijawahi kukutokea
  • Kufanya kitu kipya kabisa huku fikra zikikukumbusha kukifanya kitu hichohicho lakini bila kumbukumbu kamili
Ulimwengu wa roho ni timilifu na huweza kufanya vitu nje ya utashi wa kawaida wa binadamu na kutuletea Kumbukumbu zisisotimia.... Na hii ndio living reincarnation au living rebirth katika uhalisia wake..

Mimi sina mtoto wa kusingiziwa.... Mkioneshwa yeyote tunafanana hata vitabia jueni tu ya kwamba hiyo ni michezo ya roho katika kuvinjari kwake!

Dhana ya 'Utwaaji Upya Mwili' yaani 'Reincarnation' kwa lugha ya kiingereza -- na tena kulingana na imani, maarifa ya kimapokeo na dini -- kama vile Uhindu, Ujaini, Ubuddha n.k; huenda si 'ukweli kamili' juu ya 'kuishi' na 'maisha ya mtu'.

Kwa namna yake, Utwaaji upya mwili, huenda ilikuwa ni tafsiri nyepesi juu ya ukweli wa jambo fulani lililo pana na tata kuhususiana na 'uzima' na 'miili'. Hii ilikuja na 'maona', 'manabii' na 'watu wakuu kiroho'. Kwa maana hawa wote-- iwe kutokea mashariki ama magharibu -- wametuletea nasibu ya habari na visomo kuhusiana na 'mtu','mataifa/kabila/staarabu', 'matukio', 'wakati' na 'hatma' zake.

Yesu, kutokea nchi ya zamani kule Mashariki ya Kati -- kwa mfano, amenukulishwa katika vitabu vya dini, imani na mapokeo kupata kusema "siku za mwisho, maarifa yataongezeka duniani...". Kwamba, yale anayoyafanya, watu wengi wataweza kuyafanya pia hata na zaidi... Sasa, siku za mwisho kwa mfano, ni zipi? Ikiwa mengi aliyopata kuyasema tunayakubali -- na kwa kiasi fulani kushangazwa, ni kwa namna gani aliweza kujua "Mambo ya mbele ya wakati"(?)... Maarifa kuongezeka, Vita na Mabadiliko ya Nchi...

Ni KWELI YESU ALIKUWA NI MWENYE KUWEZA KUONA MATUKIO hata nje ya mzingo wa fahamu zake za mwili wa nyama. Watu wengi tu wamepata kuwa hivyo hivyo; kuwa na 'Jicho la Tatu' -- yeye Yesu, kunukuliwa hili linawezekana pale 'mbili inapofanywa kuwa moja'... Lakini, Je, kuona nje ya mzingo wa wakati ndiyo 'kuwa na maarifa' kama yote? SI LAZIMA... Na hapa tunaweza kutumia kesi hiyo hiyo ya Yesu, kuanza kukadirisha yumkini ya ukweli wa jambo...

Japo kuna 'kanuni ya msababishano' wa vitu na matukio; ndani ya 'mapana ya yote', wakati waweza 'kuchezeshwa' na basi hata kuwa kana 'mwisho wa dunia' usiwe ni 'mwisho' wa dunia... Tunaweza kunasibu kesho iliyo ni tofauti na 'jaala' zetu. Kwenye dini, huzungumzwa 'unafsishi' wa 'Mungu Muweza yote'... Kwamba 'utu' ama 'umma' wenye 'nyoyo safi' na 'Kuishi katika Yeye' huo waweza 'kuepushwa' na lolote 'ovu'... HII NI KWELI; lakini 'Mungu' ni fumbo la Imani...

Katika siku za leo, tunayonafasi ya kujua mambo ilivyo bora kuliko siku za nyuma zilizotuletea dini na mapokeo yanayotawala wengi duniani.

Kati ya vitu ambavyo tutavijua ama kuviandea vyema ili kujua ni 'fumbo la Mungu'; lakini sasa--tunaelekea kujua ukweli kwamba hakuna 'Mungu' hasa, ila kuna 'Uungu'... Vitu vyote, ni 'sifa', 'ishara' na 'utukufu' wa 'kweli' moja iliyo ni 'Mungu'. Lakini ni pale tu tunapoimaizi ama kujinasibu na 'kweli' katika muktadha wa 'Uungu' ndipo tunaweza kujilingania uwezo wa 'kufanyika moja na mawezekano yaliyo makuu'... Ikiwemo kutawala 'Mambo ya Nyakati' na kukadirisha 'Sheria za Madhahirisho' si tu hapa duniani ila ulimwenguni pote. Labda mapokeo ya kidini yangetaja hili kana kusema: 'kuwa Warithi wa Ufalme wa Mbingu -- Mbingu na Nchi'... Ndivyo Yesu alivyoita hasa; kusema baada ya 'Mtu kuzaliwa mara pili'... Mtume Paulo kusema; kuwa 'Mtu Mpya' mwenye nasibu ya 'Nchi Mpya'...

Mshana, 'kweli' ni si hasa --- ama tuseme, haipatikani katika stori stori ama visa vya ajabu ajabu... Kweli ni 'Taji la Imani na Taa' katika ufahamu na katika mtu. Labda mtu mwenye kuiishi njia ya imani ya namna hii anaweza kuwa ni 'mtu wa maarifa'--lakini ikiwa ni hivi, mtu huyu atanasibika 'hekima' na 'busara'. Lakini pia, maarifa si lazima iwe ni maneno... Hata katika ukimya, mapenzi na utumishi, roho ya 'kweli na uzima' inatenda -- wakati wowote na popote; kupitiliza hata 'matukio katika Nyakati'... Watu wa haya ni 'Waamuzi' katika yote yatendekayo--leo, hata kesho katika leo. Katika Uungu hakuna mwanzo wala mwisho, hakuna 'mipaka' wala 'kiasi'...

Basi, humu JF sasa, kipo kizazi cha chipkizi wenye kiu na hamu ya 'kuijua kweli'... Hawa, ndiyo huanza na udadisi, wengine watahoji kuhusu dini na mapokeo, wengine watavutika na mambo yanaonekana kupitiliza kawaida, wengine watakuwa wakanushaji wa yote yaliyoletwa na dini na kuja kuonekana ni kizingiti kwa utanuzi wa fikra, maarifa na upeo. Yote haya ni kheri, Labda pamoja tutajenga 'Hema jipya la Makutanio' katika 'Hesabu' ya watu wa Leo... 'Walawi wa leo' wanamuhitaji Musa wa vilemba vingi -- mkufunzi wa fikizia za kikwantumu, mtaasisi wa maendeleo--mipango na usimamizi, mvumbuzi, mzazi, ndugu na rafiki katika 'safari ya kuhama'; toka kwenye 'utumwa wa kimafikara' kuielekea lulu ya 'uzima na habari za ulele'.

Hmmm.
 
Dhana ya 'Utwaaji Upya Mwili' yaani 'Reincarnation' kwa lugha ya kiingereza -- na tena kulingana na imani, maarifa ya kimapokeo na dini -- kama vile Uhindu, Ujaini, Ubuddha n.k; huenda si 'ukweli kamili' juu ya 'kuishi' na 'maisha ya mtu'.

Kwa namna yake, Utwaaji upya mwili, huenda ilikuwa ni tafsiri nyepesi juu ya ukweli wa jambo fulani lililo pana na tata kuhususiana na 'uzima' na 'miili'. Hii ilikuja na 'maona', 'manabii' na 'watu wakuu kiroho'. Kwa maana hawa wote-- iwe kutokea mashariki ama magharibu -- wametuletea nasibu ya habari na visomo kuhusiana na 'mtu','mataifa/kabila/staarabu', 'matukio', 'wakati' na 'hatma' zake.

Yesu, kutokea nchi ya zamani kule Mashariki ya Kati -- kwa mfano, amenukulishwa katika vitabu vya dini, imani na mapokeo kupata kusema "siku za mwisho, maarifa yataongezeka duniani...". Kwamba, yale anayoyafanya, watu wengi wataweza kuyafanya pia hata na zaidi... Sasa, siku za mwisho kwa mfano, ni zipi? Ikiwa mengi aliyopata kuyasema tunayakubali -- na kwa kiasi fulani kushangazwa, ni kwa namna gani aliweza kujua "Mambo ya mbele ya wakati"(?)... Maarifa kuongezeka, Vita na Mabadiliko ya Nchi...

Ni KWELI YESU ALIKUWA NI MWENYE KUWEZA KUONA MATUKIO hata nje ya mzingo wa fahamu zake za mwili wa nyama. Watu wengi tu wamepata kuwa hivyo hivyo; kuwa na 'Jicho la Tatu' -- yeye Yesu, kunukuliwa hili linawezekana pale 'mbili inapofanywa kuwa moja'... Lakini, Je, kuona nje ya mzingo wa wakati ndiyo 'kuwa na maarifa' kama yote? SI LAZIMA... Na hapa tunaweza kutumia kesi hiyo hiyo ya Yesu, kuanza kukadirisha yumkini ya ukweli wa jambo...

Japo kuna 'kanuni ya msababishano' wa vitu na matukio; ndani ya 'mapana ya yote', wakati waweza 'kuchezeshwa' na basi hata kuwa kana 'mwisho wa dunia' usiwe ni 'mwisho' wa dunia... Tunaweza kunasibu kesho iliyo ni tofauti na 'jaala' zetu. Kwenye dini, huzungumzwa 'unafsishi' wa 'Mungu Muweza yote'... Kwamba 'utu' ama 'umma' wenye 'nyoyo safi' na 'Kuishi katika Yeye' huo waweza 'kuepushwa' na lolote 'ovu'... HII NI KWELI; lakini 'Mungu' ni fumbo la Imani...

Katika siku za leo, tunayonafasi ya kujua mambo ilivyo bora kuliko siku za nyuma zilizotuletea dini na mapokeo yanayotawala wengi duniani.

Kati ya vitu ambavyo tutavijua ama kuviandea vyema ili kujua ni 'fumbo la Mungu'; lakini sasa--tunaelekea kujua ukweli kwamba hakuna 'Mungu' hasa, ila kuna 'Uungu'... Vitu vyote, ni 'sifa', 'ishara' na 'utukufu' wa 'kweli' moja iliyo ni 'Mungu'. Lakini ni pale tu tunapoimaizi ama kujinasibu na 'kweli' katika muktadha wa 'Uungu' ndipo tunaweza kujilingania uwezo wa 'kufanyika moja na mawezekano yaliyo makuu'... Ikiwemo kutawala 'Mambo ya Nyakati' na kukadirisha 'Sheria za Madhahirisho' si tu hapa duniani ila ulimwenguni pote. Labda mapokeo ya kidini yangetaja hili kana kusema: 'kuwa Warithi wa Ufalme wa Mbingu -- Mbingu na Nchi'... Ndivyo Yesu alivyoita hasa; kusema baada ya 'Mtu kuzaliwa mara pili'... Mtume Paulo kusema; kuwa 'Mtu Mpya' mwenye nasibu ya 'Nchi Mpya'...

Mshana, 'kweli' ni si hasa --- ama tuseme, haipatikani katika stori stori ama visa vya ajabu ajabu... Kweli ni 'Taji la Imani na Taa' katika ufahamu na katika mtu. Labda mtu mwenye kuiishi njia ya imani ya namna hii anaweza kuwa ni 'mtu wa maarifa'--lakini ikiwa ni hivi, mtu huyu atanasibika 'hekima' na 'busara'. Lakini pia, maarifa si lazima iwe ni maneno... Hata katika ukimya, mapenzi na utumishi, roho ya 'kweli na uzima' inatenda -- wakati wowote na popote; kupitiliza hata 'matukio katika Nyakati'... Watu wa haya ni 'Waamuzi' katika yote yatendekayo--leo, hata kesho katika leo. Katika Uungu hakuna mwanzo wala mwisho, hakuna 'mipaka' wala 'kiasi'...

Basi, humu JF sasa, kipo kizazi cha chipkizi wenye kiu na hamu ya 'kuijua kweli'... Hawa, ndiyo huanza na udadisi, wengine watahoji kuhusu dini na mapokeo, wengine watavutika na mambo yanaonekana kupitiliza kawaida, wengine watakuwa wakanushaji wa yote yaliyoletwa na dini na kuja kuonekana ni kizingiti kwa utanuzi wa fikra, maarifa na upeo. Yote haya ni kheri, Labda pamoja tutajenga 'Hema jipya la Makutanio' katika 'Hesabu' ya watu wa Leo... 'Walawi wa leo' wanamuhitaji Musa wa vilemba vingi -- mkufunzi wa fikizia za kikwantumu, mtaasisi wa maendeleo--mipango na usimamizi, mvumbuzi, mzazi, ndugu na rafiki katika 'safari ya kuhama'; toka kwenye 'utumwa wa kimafikara' kuielekea lulu ya 'uzima na habari za ulele'.

Hmmm.
@mose Mmh.. hebu sema neno na hapa pia
Maslahi ya kiroho kwenye matokeo tasa ya kimwili yaliyoharibika

Jr
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom