Hakuna "Mimi" Wala "Wewe": Spiritual awakening(non-duality)

Hakuna "Mimi" Wala "Wewe": Spiritual awakening(non-duality)

de Gunner

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2021
Posts
11,375
Reaction score
22,568
Kabla sijaanza, nataka niweke wazi kuwa spiritual awakening si sawa na dini. Dini mara nyingi hutufundisha namna ya kumtafuta Mungu nje yetu, lakini spiritual awakening ni safari ya kujitambua ndani yetu. Si kuhusu kubadilisha dini, kuacha imani fulani au kuwa “mtakatifu”… bali ni kuanza kuhoji reality, ego, suffering na true nature yetu ya ndani.

Wengine hupitia hii kupitia dini, maumivu, upweke, meditation, mapenzi, au hata kuvunjika kabisa kiakili na kihisia. Mwisho wa yote, safari hii humrudisha mtu karibu zaidi na essence yake ya kweli.

Leo nataka tupige stori kuhusu hii dhana ya kiroho inayoitwa non-duality (kutokuwa na mgawanyiko wa kweli kati ya “mimi” na “wewe”). Hata kama hujishughulishi sana na spiritual matters, naamini umewahi kusikia kuhusu hii concept! Na kama bado… basi unaweza kuichunguza kidogo maana ni jambo la kuvutia sana.

Tangu nilipoanza safari yangu ya kiroho, imekuwa safari ngumu sana. Mara nyingi huwaambia watu wasikurupuke kuingia kwenye hii njia, maana ukishaingia ndani yake, hakuna kurudi nyuma mpaka upitie kila hatua yake. Na ukweli ni kwamba, inaweza kuwa ya maumivu, kuchanganya na kuvunja kabisa ule uelewa wako wa zamani.

Hatua nne zinazoweza kutokea kwenye spiritual awakening ni hizi:

1: Kutokuwa na ufahamu (Unconsciousness)

Hii ni hatua ambayo ego ndiyo inaongoza maisha yako, na utambulisho wako wote unakuwa umefungwa kwenye mawazo, conditioning na programming ulizokulia nazo.

2: Kifo cha ego (Dark night of the soul)

Hapa ndipo ule mfumo wako wa zamani wa kufikiri unaanza kuvunjika. Reality yako inaanza kubadilika, na hali hii huleta maumivu makubwa kwa sababu vitu vya kimwili vilivyokuwa vinakupa furaha au kukutambulisha vinaanza kuonekana vya uongo au havina maana tena kulingana na uelewa mpya unaochipuka ndani yako.

3: Kutafuta (The search)

Baada ya kupitia mateso na maumivu mengi, unaanza polepole kuingia kwenye ulimwengu usiojulikana. Kuna kitu ndani ya roho yako kinakuvuta kuelekea ukweli ambao bado hujaugundua kikamilifu. Inaweza kuogopesha, lakini ukiendelea mbele kwa imani, utaanza kutembea kwa faith badala ya sight.

4: Kuzaliwa upya (Rebirth)

Baada ya safari ndefu ya kutafuta, siku moja unaweza kupata glimpse ya true nature yako. Ile hali ambayo imekuwa ndani yako tangu ukiwa mtoto mdogo. Itahisi kama kukutana na soulmate wako. Hakuna maneno yanaweza kuelezea hiyo feeling. Utahisi uko nyumbani ndani yako mwenyewe na hata nje yako.

Kwa hizo hatua chache, naamini unaweza kuona jinsi safari ya kiroho ilivyo. Kumbuka, hii si journey yenye mwisho… ni deaths and rebirths zisizoisha. Na mara nyingi hizo hatua zinaweza kutokea kwa wakati mmoja au zisifuate mpangilio kabisa.

Kwa upande wangu, kila baada ya phase fulani ya awakening kwenye maisha yangu, nimekuwa nikihisi hii hali ya non-duality ambapo nahisi hakuna “mimi” wala “wewe”… kila kitu kinaonekana kuunganishwa.

Nafikiri mmegundua pia jinsi watoto wadogo au viumbe wachanga — iwe ni binadamu, ndege au wanyama — wanavyokuwa na hii hali naturally ndani yao.

Nilikuwa naangalia clip moja YouTube siku nyingine nikawaona watoto wa mbwa wakicheza na mtoto mchanga wa kibinadamu, na honestly connection yao ilikuwa beyond words. Pia mmegundua jinsi babies wanavyovutiwa sana na wanyama au hata watu wengine wenye energy fulani ya utulivu na uwepo wa kina?
Naam, hiyo ndiyo essence yetu ya msingi… sisi sote tumeunganishwa.

Kama wewe ni mtu wa kiroho, mara nyingi utaona hata wanyama wanakuwa attracted kwako. Wanaweza kuhisi hiyo pure energy inayotoka ndani ya soul yako.

Ulimwengu umeunganishwa kwenye msingi wake kabisa. Ni miaka ya hivi karibuni tu ambapo hata scientists wameanza kuzungumzia possibilities hizi kupitia quantum mechanics, lakini kwenye spiritual world mambo haya yamekuwa yakizungumziwa kwa maelfu ya miaka.

Kwa hiyo mimi, wewe na kila kitu kingine ni sehemu ya umoja mmoja. Hakuna separation ya kweli.

Ningependa kumalizia na quote niliyosikia kwenye interview ya Gabi Kovalenko. Yeye ni mmoja wa spiritual seekers ninaowapenda sana. Ana YouTube channel ambapo huzungumzia mambo ambayo honestly yanaonekana kuwa beyond her age — na ana miaka 23 tu. Wakati mwingine ni kama anachannel messages kutoka higher realms… lakini baadaye nikagundua kuwa sisi sote tuna uwezo huo, isipokuwa roho zetu zimefungwa na conditioning pamoja na programming za dunia.

Kila mtu anapitia njia yake binafsi, lakini njia ya kurudi nyumbani ni moja kwa wote.” ~ Gabi Kovalenko

So that’s it kwa leo. Wewe unaionaje non-duality? Unaamini ni siri fulani kubwa au ndiyo true nature yetu ya msingi? Umewahi kupitia spiritual awakening? Experience yako ilikuwa vipi?

In love and light ✨
 
andiko lako zuri sana upo sahihi, mimi ni self initiated nina mwaka sasa na practice kabbalah faida ninaziona na sijutii. saturnian work inanisaidia sana kuconfront chaos/distractions kuzigeuza kuwa order nafanyia kazi sana hizi nguzo mbili boaz na jachin.
 
andiko lako zuri sana upo sahihi, mimi ni self initiated nina mwaka sasa na practice kabbalah faida ninaziona na sijutii. saturnian work inanisaidia sana kuconfront chaos/distractions kuzigeuza kuwa order nafanyia kazi sana hizi nguzo mbili boaz na jachin.
Like the kabbalah!!?
images.png

Mimi niliishiaga tu kuisoma, Kwa juu juu tu, ila chakras practice naijua, zile energy centers naskia zinaendana na kabbalah. Na initiation kwangu ilikuwa Kwa njia ya mahusiano nahisi kulikuwa na soul to soul integration na huyo mtu. Nilipitia kipindi kugumu sana.

Hiyo kabbalah unaifanya mwenyewe au?
 
kabbalah ni inner work kama ilivyo meditation tu. kinachotakiwa ni kufocus energy inayotolewa na vitufe(sephirots) mana hvyo vitufe vimepangwa kwenye nguzo tatu kushoto(boaz) katikati(axis mundi) na kulia(jachin), mfn nguzo ya kushoto vina release restrictive energy yaan mtu kuwa na kiasi na kudhibiti tamaa, nidhamu na uvumilivu. nguzo ya kulia ina emit expansive energy hapa ndo kuna usitawi na kuongezeka. pia focus energy inayotoka kwenye zile herufi za kiebrania(hebrew letters) mfn heruf beth(B) ina wakirisha house na inarelate sana na sefirot ya 3 binah(cosmic womb) ambayo ni saturn hii kazi yake ni kubadili fikra(abstract ideas) na kuwa maumbo(form,structure) ko kila kitu kweny tree of life kina energy yake unachotakiwa ni kufocus hizo energy.
 
mfn mtu unapopitia magumu ili kuyashinda unafocuz sefirot ya 3 binah(understanding) inarelate na planet saturn(black) ambayo ni god of time(titan cronos) huyu ni great teacher anafundisha kuwa na discpline, patience. kwa tafsiri nyngne saturn ni kipindi kwny maisha ya m2 ambacho mtu anapitia magumu ili kujifunza na kuwa imara. it is a death indeed.
 
kabbalah ni inner work kama ilivyo meditation tu. kinachotakiwa ni kufocus energy inayotolewa na vitufe(sephirots) mana hvyo vitufe vimepangwa kwenye nguzo tatu kushoto(boaz) katikati(axis mundi) na kulia(jachin), mfn nguzo ya kushoto vina release restrictive energy yaan mtu kuwa na kiasi na kudhibiti tamaa, nidhamu na uvumilivu. nguzo ya kulia ina emit expansive energy hapa ndo kuna usitawi na kuongezeka. pia focus energy inayotoka kwenye zile herufi za kiebrania(hebrew letters) mfn heruf beth(B) ina wakirisha house na inarelate sana na sefirot ya 3 binah(cosmic womb) ambayo ni saturn hii kazi yake ni kubadili fikra(abstract ideas) na kuwa maumbo(form,structure) ko kila kitu kweny tree of life kina energy yake unachotakiwa ni kufocus hizo energy.
Mkuu hii inaonekana ni very complex...
Je Ina link na chakras. Maana unavyo focus hapo si lazima ujue energy center Gani Ina draw hiyo energy.
 
mfn mtu unapopitia magumu ili kuyashinda unafocuz sefirot ya 3 binah(understanding) inarelate na planet saturn(black) ambayo ni god of time(titan cronos) huyu ni great teacher anafundisha kuwa na discpline, patience. kwa tafsiri nyngne saturn ni kipindi kwny maisha ya m2 ambacho mtu anapitia magumu ili kujifunza na kuwa imara. it is a death indeed.
Ngoja nitarudi uongee vizuri. Hapo Kuna astrology pia mambo ya planets sio?
.do you believe in astrology or numerology?
 
ndiyo inauhusiano sana sema tu chakras ni kajisehemu kadogo kutoka kwny tree of life maana inaresemble na nguzo ya katikati yenye vitufe keter(crown), daat(throat), tiferet(heart), yesod na malchut. siyo complex kiivo ukijitoa unaelewa.
 
Yes exactly ushagundua code, hii ndo modern kabbalah inablend sefirots na field zngne kama ulvoztaja astrology, numerology, ukiingia deep kuna angelorogy, demonology, psychology yaan iyo tree of life inamaarifa mengi sana.
 
ndiyo inauhusiano sana sema tu chakras ni kajisehemu kadogo kutoka kwny tree of life maana inaresemble na nguzo ya katikati yenye vitufe keter(crown), daat(throat), tiferet(heart), yesod na malchut. siyo complex kiivo ukijitoa unaelewa.
Je Kuna workshop? Au unafanya mwenyewe?

So you use thought alone? Kudraw energy. Also chakra ziko nyingi. Sio zile 7 tu. Huenda ikawa Ina link na chakras zote. Hizo practice unazifanya hapa hapa bongo? Do you have a guide or guru?
 
naamini sana kwenye astrology ila in kabbalistic perspective sio kama ya hawa manajimu wa mtandaoni wanavochambua. Numerology Sio Sana.
Is that not new age spirituality? Maana kumekuwa na criticism sana kwenye astrology. Numerology mwanzoni kama ilikua Ina make sense ila baadae nikagundua Kuna some sort of fallacies
 
Kabla sijaanza, nataka niweke wazi kuwa spiritual awakening si sawa na dini. Dini mara nyingi hutufundisha namna ya kumtafuta Mungu nje yetu, lakini spiritual awakening ni safari ya kujitambua ndani yetu. Si kuhusu kubadilisha dini, kuacha imani fulani au kuwa “mtakatifu”… bali ni kuanza kuhoji reality, ego, suffering na true nature yetu ya ndani.

Wengine hupitia hii kupitia dini, maumivu, upweke, meditation, mapenzi, au hata kuvunjika kabisa kiakili na kihisia. Mwisho wa yote, safari hii humrudisha mtu karibu zaidi na essence yake ya kweli.

Leo nataka tupige stori kuhusu hii dhana ya kiroho inayoitwa non-duality (kutokuwa na mgawanyiko wa kweli kati ya “mimi” na “wewe”). Hata kama hujishughulishi sana na spiritual matters, naamini umewahi kusikia kuhusu hii concept! Na kama bado… basi unaweza kuichunguza kidogo maana ni jambo la kuvutia sana.

Tangu nilipoanza safari yangu ya kiroho, imekuwa safari ngumu sana. Mara nyingi huwaambia watu wasikurupuke kuingia kwenye hii njia, maana ukishaingia ndani yake, hakuna kurudi nyuma mpaka upitie kila hatua yake. Na ukweli ni kwamba, inaweza kuwa ya maumivu, kuchanganya na kuvunja kabisa ule uelewa wako wa zamani.

Hatua nne zinazoweza kutokea kwenye spiritual awakening ni hizi:

1: Kutokuwa na ufahamu (Unconsciousness)

Hii ni hatua ambayo ego ndiyo inaongoza maisha yako, na utambulisho wako wote unakuwa umefungwa kwenye mawazo, conditioning na programming ulizokulia nazo.

2: Kifo cha ego (Dark night of the soul)

Hapa ndipo ule mfumo wako wa zamani wa kufikiri unaanza kuvunjika. Reality yako inaanza kubadilika, na hali hii huleta maumivu makubwa kwa sababu vitu vya kimwili vilivyokuwa vinakupa furaha au kukutambulisha vinaanza kuonekana vya uongo au havina maana tena kulingana na uelewa mpya unaochipuka ndani yako.

3: Kutafuta (The search)

Baada ya kupitia mateso na maumivu mengi, unaanza polepole kuingia kwenye ulimwengu usiojulikana. Kuna kitu ndani ya roho yako kinakuvuta kuelekea ukweli ambao bado hujaugundua kikamilifu. Inaweza kuogopesha, lakini ukiendelea mbele kwa imani, utaanza kutembea kwa faith badala ya sight.

4: Kuzaliwa upya (Rebirth)

Baada ya safari ndefu ya kutafuta, siku moja unaweza kupata glimpse ya true nature yako. Ile hali ambayo imekuwa ndani yako tangu ukiwa mtoto mdogo. Itahisi kama kukutana na soulmate wako. Hakuna maneno yanaweza kuelezea hiyo feeling. Utahisi uko nyumbani ndani yako mwenyewe na hata nje yako.

Kwa hizo hatua chache, naamini unaweza kuona jinsi safari ya kiroho ilivyo. Kumbuka, hii si journey yenye mwisho… ni deaths and rebirths zisizoisha. Na mara nyingi hizo hatua zinaweza kutokea kwa wakati mmoja au zisifuate mpangilio kabisa.

Kwa upande wangu, kila baada ya phase fulani ya awakening kwenye maisha yangu, nimekuwa nikihisi hii hali ya non-duality ambapo nahisi hakuna “mimi” wala “wewe”… kila kitu kinaonekana kuunganishwa.

Nafikiri mmegundua pia jinsi watoto wadogo au viumbe wachanga — iwe ni binadamu, ndege au wanyama — wanavyokuwa na hii hali naturally ndani yao.

Nilikuwa naangalia clip moja YouTube siku nyingine nikawaona watoto wa mbwa wakicheza na mtoto mchanga wa kibinadamu, na honestly connection yao ilikuwa beyond words. Pia mmegundua jinsi babies wanavyovutiwa sana na wanyama au hata watu wengine wenye energy fulani ya utulivu na uwepo wa kina?
Naam, hiyo ndiyo essence yetu ya msingi… sisi sote tumeunganishwa.

Kama wewe ni mtu wa kiroho, mara nyingi utaona hata wanyama wanakuwa attracted kwako. Wanaweza kuhisi hiyo pure energy inayotoka ndani ya soul yako.

Ulimwengu umeunganishwa kwenye msingi wake kabisa. Ni miaka ya hivi karibuni tu ambapo hata scientists wameanza kuzungumzia possibilities hizi kupitia quantum mechanics, lakini kwenye spiritual world mambo haya yamekuwa yakizungumziwa kwa maelfu ya miaka.

Kwa hiyo mimi, wewe na kila kitu kingine ni sehemu ya umoja mmoja. Hakuna separation ya kweli.

Ningependa kumalizia na quote niliyosikia kwenye interview ya Gabi Kovalenko. Yeye ni mmoja wa spiritual seekers ninaowapenda sana. Ana YouTube channel ambapo huzungumzia mambo ambayo honestly yanaonekana kuwa beyond her age — na ana miaka 23 tu. Wakati mwingine ni kama anachannel messages kutoka higher realms… lakini baadaye nikagundua kuwa sisi sote tuna uwezo huo, isipokuwa roho zetu zimefungwa na conditioning pamoja na programming za dunia.

Kila mtu anapitia njia yake binafsi, lakini njia ya kurudi nyumbani ni moja kwa wote.” ~ Gabi Kovalenko

So that’s it kwa leo. Wewe unaionaje non-duality? Unaamini ni siri fulani kubwa au ndiyo true nature yetu ya msingi? Umewahi kupitia spiritual awakening? Experience yako ilikuwa vipi?

In love and light ✨
Naweka kambi na hapa pia
 
Like the kabbalah!!?
View attachment 3596820
Mimi niliishiaga tu kuisoma, Kwa juu juu tu, ila chakras practice naijua, zile energy centers naskia zinaendana na kabbalah. Na initiation kwangu ilikuwa Kwa njia ya mahusiano nahisi kulikuwa na soul to soul integration na huyo mtu. Nilipitia kipindi kugumu sana.

Hiyo kabbalah unaifanya mwenyewe au?
Hebu nitofautishie hiyo tree of life vs of death inamaanisha what you choose will be responsible for it?
 
Hebu nitofautishie hiyo tree of life vs of death inamaanisha what you choose will be responsible for it?
Mkuu hata Mimi mgeni, huyo mkuu hapo ndo alinikumbusha Kuna kipindi nilipitia hayo mambo juu juu. Tu.

Hapo Kwa ufupi hiyo ni kabbalah. Ni kama practice ya kiroho inayo Fanya kuactivate miwili yetu spiritually just like meditation ila yenyewe unakuwa unafocus kwenye kuiongo au sehem ya mwili mpaka uhisi energy inatembea hapo.

Mfano unafocus kwenye paji la uso, then unajua unahisi kama nishati inazunguka eneo Hilo. So with time sehem hiyo inakuwa more active labda unaanza kufikiria vizuri, unaanza kuona vitu kabla havijatokea and so forth
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom