My point is satelite zao zimeshindwa kuhuduMia watu 19,000 tu kiasi ambacho minara miwili tu inahudumia bila shida, itawezaje kukomboa watu milioni 60 wakati 19,000 imeshindwa?
Na Elon hawezi kukuletea satelite 7000 ni matrilioni ya hela, kwake yeye ni faida zaidi kununua mitandao yote ya Tanzania kuliko kuleta hizo satelite.
Hapo hujaelewa kitu mzee..
Satellite moja ya starlink inaweza hudumia watu hadi 5000 na zaidi kwa wakati mmoja...
Nimekuelezea hapo kwamba bado starlink hawajaweka ground stations za kutosha, Africa nzima kuna ground stations mbili tu , moja ipo Nigeria nyingine Nairobi.. hizo ndizo zinahudumia Africa yote...
Tatizo sio satellite, tatizo hapo ni ground stations....
Kama huku mnavyopambana na kujenga minara toka 1990s, starlink ya juzi hapa inaendelea kujenga ground stations , Nigeria sasa wanaendelea na ujenzi katika miji mitatu Lagos, Ogun, na Port Harcourt.
Mwezi march hapo Msumbiji wametengeneza kituo hapo Msumbiji kwa ajili ya ku feed connection Kusini mwa Jangwa la Sahara, hasa kwa nchi jirani kama Zambia na Zimbabwe..
Kama starlink wana satellite zaidi ya 7578... hawashindwi kutengeneza ground stations(PoP) za kutosha hapa East Africa..
Hadi sasa kuna Point of Presence mbili tu Africa kote, moja ni Nigeria na nyingine ni Kenya...
Gharama moja ya kutengeneza satellite ya starlink v2 mini ya kisasa ni dola $200,000–$300,000 kwa satelaiti moja.. ikiwa ni pamoja na ujenzi, majaribio, na urushaji...
Starlink inarushwa kwa kutumia roketi za Falcon 9 kutoka SpaceX, kwa gharama ya karibu $67 milioni kwa roketi moja, inayobeba satelaiti kati ya 22–60.
Tuje kwenye gharama ya ground stations...
Kituo cha PoP cha Starlink, ground station yenye dishes kubwa, fiber connection na data center ndogo hugharimu Takribani $50,000 hadi $250,000 kutegemeana na eneo...
Hapo Gharama ni ya kujenga, kuweka vifaa, na kuunganisha na fiber kwenye internet backbone...
Hivyo elewa Satelaiti ya Starlink ni ghali zaidi kutengeneza na kurusha kuliko PoP ya ardhini lakini bado angani wana satellite 7578, watashindwa kusambaza hizo PoPs bara la Africa?