52 weeks saving Challenge... Hivi watanzania Tuna Shida gani?

52 weeks saving Challenge... Hivi watanzania Tuna Shida gani?

Kuweka akiba inawezekana sana,ila kama una pesa kidogo haisaidii.Maana pesa yetu haitabiriki.Leo unaweka laki na nusu kwenye kibubu,ambayo ungeweza kununua baiskeli ikupunguzie gharama za usafiri,mwakani unaichukua uitumie unakuta baiskeli inauzwa laki mbili,sasa huu utakuwa ujanja ama uzwazwa?
Wakati mwingine,huwa nawashangaa sana wasomi wengi kwa kutoa elimu kutokana na theory zilizotengenezwa na wazungu.Wazungu wao pesa yao ni stable sana wanaweza kuweka akiba na ikawa na maana.
Unakuta jitu linasoma marekani,linakuja na Sera za kufuta fao la kujitoa,kisa, wazungu wanafanya hivyo!!Yaani unaona kabisa jinsi akili zilivyo za kikenge
 
Kusema Ukweli mie huwa Sinaga Mood kabisa na Hizi Tips and Tricks za Kusave na Kusaidiana zinazoibuka kila mara maana Nyingi naonaga kama Ni za Watu ambao hawakukaa Chini kufikiria ila Walikurupuka Tu

Naona Haka kamtindo kameanza Mdogo Mdogo (52 weeks saving) yaani Kila Week uwe una Deposit kiasi fulani cha Pesa Kwenye Kibubu chako. Na wahanga wengi watakuwa tena wakina Mama.. Kama Michezo ya Vikoba na Kusaidiana

1704ef7b023da7df8b4261787371f775.jpg


Sijaona Mantiki ya Hii Kitu na Kwangu ni kama Impossible kwa Maisha Yetu haya Ya Kubangaiza Bangaiza. Leo hii mtu anakuambia et kila week weka Kiasi fulani cha Pesa...

Chukulia Mfano kwa week 40 mpk 43 hapo juu haiwezekani mtu kwa week Moja Aingize Tsh laki 400000 halafu week ya pili pia Aingize laki 410000 halafu week ya tatu aingize 420000 na Ya nne Aingize 430000 which makes 1660000 per month.

Hii itawezekana kwa Watu wenye biashara kubwa na Waliofanikiwa Tayari ila kama Wewe ni mfanyakazi wa Serikali wa laki 4-7 per month bado hujalipa Kodi... Madeni.... Watoto..na biashara zetu ndogo ndogo.n.k hii kitu ni Impossible
Umekuwa bias kuizungumzia ya f10 wakati zipo chat cha hadi 1000 kwa wiki ila wewe ulitaka uzungumzie kilicho kushinda. Mimi ninacho cha f5 na nimeamua kujiwekea kila ninapopata hata mara mbili hadi tatu kwa wiki kadri nipatavyo. Mpaka sasa niko wiki ya 10
 
Umekuwa bias kuizungumzia ya f10 wakati zipo chat cha hadi 1000 kwa wiki ila wewe ulitaka uzungumzie kilicho kushinda. Mimi ninacho cha f5 na nimeamua kujiwekea kila ninapopata hata mara mbili hadi tatu kwa wiki kadri nipatavyo. Mpaka sasa niko wiki ya 10
Sawa ukifika Week za Mbele Uje Tena ... Hizo week za Mwanzo hata Mwanafunzi wa chuo anaweza fika ..... Endelea Week za Mbele ambazo Zitakuhitaji Kila Week uwe unapata Laki 4 ndo utajua It is an impossible thing kila week upate laki 4
 
Kuweka akiba inawezekana sana,ila kama una pesa kidogo haisaidii.Maana pesa yetu haitabiriki.Leo unaweka laki na nusu kwenye kibubu,ambayo ungeweza kununua baiskeli ikupunguzie gharama za usafiri,mwakani unaichukua uitumie unakuta baiskeli inauzwa laki mbili,sasa huu utakuwa ujanja ama uzwazwa?
Wakati mwingine,huwa nawashangaa sana wasomi wengi kwa kutoa elimu kutokana na theory zilizotengenezwa na wazungu.Wazungu wao pesa yao ni stable sana wanaweza kuweka akiba na ikawa na maana.
Unakuta jitu linasoma marekani,linakuja na Sera za kufuta fao la kujitoa,kisa, wazungu wanafanya hivyo!!Yaani unaona kabisa jinsi akili zilivyo za kikenge
Bora wewe... Kuna watu humu wapo kama Wale wa Forex.... Wanadhani hiyo Chat Ni Simple kuifuta..
 
Sawa ukifika Week za Mbele Uje Tena ... Hizo week za Mwanzo hata Mwanafunzi wa chuo anaweza fika ..... Endelea Week za Mbele ambazo Zitakuhitaji Kila Week uwe unapata Laki 4 ndo utajua It is an impossible thing kila week upate laki 4
Wiki ya 52 nitatakiwa ku-save 260,000 nayo mahela mengi hata wakati unayaweka unajionea tamaa
 
Wiki ya 52 nitatakiwa ku-save 260,000 nayo mahela mengi hata wakati unayaweka unajionea tamaa
Week ya 52-260000
Week ya 51-255000
Week ya 50-250000
Week ya 49-245000

Hizo week unatakuwa uwe na Kipato cha 1,010,000.(million moja na Kumi) kwa Mwezi....ndo maana Nikasema Kama Wewe si Mfabiashara ni mtu wa Kawaida tu hutoweza.. Hizo chat ni ngumu... Na Walizonazo ni wenye vipato vidogo wakitegemea kwa Week watapata laki 2 wakati Mshahara wake kwa mwezi haufiki laki 5
 
  • Thanks
Reactions: 314
Asante....hili ndilo lengo hasa...mie binti yangu kila jumamosi nampeleka benk akaweke akiba minimum tzs 5000. Ana 8 years....na anapenda sana kazi hyo maana nishimwambia anatunza hela ya sikukuuu....wazo kuu hapa ni kwamba hapo baadae hii itakuwa ni tabia yake....kuweka akiba hata kama ana kidogo.

Basi Mada Yangu Ni Nje Ya Mnachokijadili hata Mie nina Weka Akiba pia.. ila Angalieni Lengo la Akiba Ya Hiyo Chat.. hapo juu

Umetoa mfano Mzuri kwamba Kila Jumamos unampa Mwanao Elfu 5 . Sasa Kuna mmoja humu Yeye anafuata Huo huo Mtindo wako wa Elfu 5 ila Kwa Chati hiyo hapo Juu. Sasa Yeye Anatakuwa Kila Week Aongeze Elfu Tano yaani kila Jumamos uwe unampa Mwanao Kiasi hicho cha Nyongeza ya Sh Elfu 5 mpka Week 52 zitimie.

Maana Yake Itakapofika
jumamosi ya Kwanza Utampa 5000
Jumamosi ya pili utampa 10000
Jumamos ya tatu utampa 15000
Jumamosi ya nne utampa 20000
Jumamosi ya tano utampa 25000
Jumamosi ya sita utampa 30000

Hizo Jumamos za Kwanza Unaweza Ukajibana Ukampa Maana Ni Rahisi

Maana yake Utakapo fika Jumamosi ya 49 utatakiwa kumpa Mwanao 245,000 kwa Week na Jumamos ya 50 inayofuata Utatakiwa Kumpa Mwanao tena 250000 kwa Week hiyo. Jumamosi inayofuata ya 51 unatakiwa kumpa Mwanao 255000 na Jumamos ya 52 unatakiwa Kumpa Mwanao tena 260000. Which makes 1,010,000 kwa Mwezi mzima..

JE UTAWEZA KUMPATIA MWANAO Shilingi za kitanzania Milioni moja na elfu kumi kwa Mwezi wakati wewe Mshahara wako ni Laki 5 kwa Mwezi... ?
Asante....hili ndilo lengo hasa...mie binti yangu kila jumamosi nampeleka benk akaweke akiba minimum tzs 5000. Ana 8 years....na anapenda sana kazi hyo maana nishimwambia anatunza hela ya sikukuuu....wazo kuu hapa ni kwamba hapo baadae hii itakuwa ni tabia yake....kuweka akiba hata kama ana kidogo.
 
Hilo shindano hakutapeli mtu, ni mchezo unaocheza mwenyewe nyumbani kwako, na siyo lazima kiwango kiwe hicho kilichotajwa....mnaweza kuanza na 500 au 1000...tena hiyo inaweza kuwa bora kuliko upatu
Ni wapi Nimesema kwamba Watu wanatapeliwa?
 
Unaweza pia ukaweka kiasi kisichobadilika kilicho ndani ya uwezo wako.
Sawa Tatizo la Hiyo Chat inakuhitaji Uweke Kiasi Cha Nyongeza kila Week...

Yaani Tuseme leo tarehe 3 uweke 250000 baada ya Siku saba yaani tarehe 10 uweke 260000 baada ya siku saba tena yaani tarehe 17 uweke 270000 mana Yake Kuanzia Leo tarehe 3 mpaka tarehe 17 mwezi Huu uwe umeweka Tsh 780,000 . Je kwa Kawaida Mwenye Mshahara Duni Ataweza
 
Usifananishe vicoba na hiyo. Kwanza ni hela yako unasave kwanini uone haiwezekani?
 
Usifananishe vicoba na hiyo. Kwanza ni hela yako unasave kwanini uone haiwezekani?
Ma dia vitu vingine vinawezekana kwa kuandika tu na kuongea ila ukija kwenye vitendo na uhalisia haviwezekani hapo labda inawezekana kwa kina mengi sie tunaosubiri laki moja tarehe 32 hadi tarehe 32 kiuhalisia hiyo ni NGUMU
 
Ma dia vitu vingine vinawezekana kwa kuandika tu na kuongea ila ukija kwenye vitendo na uhalisia haviwezekani hapo labda inawezekana kwa kina mengi sie tunaosubiri laki moja tarehe 32 hadi tarehe 32 kiuhalisia hiyo ni NGUMU
Ndo wengine hatuwez ila wapo wanaoweza. Kwa mfano mimi ningesave week tu ningevunja kibubu nikaila hiyo hela [emoji2][emoji2]
 
Sawa ukifika Week za Mbele Uje Tena ... Hizo week za Mwanzo hata Mwanafunzi wa chuo anaweza fika ..... Endelea Week za Mbele ambazo Zitakuhitaji Kila Week uwe unapata Laki 4 ndo utajua It is an impossible thing kila week upate laki 4
Hawajakuelewa ila wakipitia hii point watakuelewa kuna vitu huwa theoretically inawezekana ila kiutendaji ni ngumu ni bora wangewwka fixed amount lkn hapo wanaonyesha kuwa kipato chako kinakua kila mwezi au una kipato kikubwa sana unajifunza kuweka akiba
 
Ndo wengine hatuwez ila wapo wanaoweza. Kwa mfano mimi ningesave week tu ningevunja kibubu nikaila hiyo hela [emoji2][emoji2]
ha ha ha ha ha kwamba ungevunja mie kusave naweza ila si kwa kiwango cha hiyo chart.
 
ha ha ha ha ha kwamba ungevunja mie kusave naweza ila si kwa kiwango cha hiyo chart.
Aah ningevunja. Nasave kwenye vicoba na michezo miwili ya upatu inatosha. Siwezi kuona nina hela ndani halafu kuna jambo linakwama nisiitumie.
 
Back
Top Bottom