20m itanifikisha wapi katika ujenzi wakuu?

Isenye

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2024
Posts
1,436
Reaction score
3,862
Habari marafiki.
Mkononi nina kama 20M hivi, kuna kiwanja kama 25×20 nimekipata Morogoro Road, eneo linaitwa Madafu, kwa 3M.

Mkononi nitabakiwa na 17M.

Je, wakuu, naweza kweli kujenga nyumba ya walau room 3 ikafika usawa wa lenta, au niendelee kusubiri kwanza?
 

Renta inafika.
na zile kozi 3 za juu baada ya renta unaweka kabisa.
Inabaki kupaua.
 
Alaf hiyo sehem ni tambarare au ina muinuko?. Udongo mzur?.

Nyumba gharama iko kwenye msingi.
Ila ukishapiga ule mkanda baada ya msingi na kuanza kunyanyua tofali had renta gharama sio kubwa.
 
Ujenzi ni wa kuanza tu Mkuu usisikilize ushahuri wa mtu, utakapoishia hapo hapo, alaf ujenzi Kwa sisi ambao tuna vijipesa za kuja na kupwaa huwa hatumalizi siku Moja itokee tu

Wewe anza utapoishia utamalizia au utaenda mdogo mdogo utakapopata pesa nyingine, jambo la baraka kama hilo huwa lina upepo wake unaweza ukaanza msingi tu wakaja wenye uwezo zaidi wakakwambia wakupe million 100 uwapishe
 
Vyumba 2, choo, jiko, kastoo, ka dinning room na sebule ya 14x15ft^s unahamia.
 
Kama hautaki mbwembwe za ramani ulizoona mbweni, na uwe na idea ya ujenzi angalau kidogo( ili usiokotwe), unang'ata meno unapaua, unapumzika kukusanya nguvu za finishing
 
Room 3 unapaua.
 
Iwapo unauhakika kiwanja hakina shida anza ujenzi,ila usishtuke kwani inaweza isifikie lengo lako la llinta.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…