2030: Wimbo mpya ya Roma Mkatoliki

Roma ni msanii mzuri sana lakini inabidi abadilike.Ana style na mistari mikali tuu.Tatizo linakuja pale ngoma zake zote zinafanana kimidundo na kimaudhui.Chorus tu ndo tofauti!Hata kama producer ni mmoja lakini sio lazima ngoma zote zifuate the same pattern.

Inabidi ajifunze kubadilisha maudhui na midundo halafu ile identity yake ya "Uroma" akaendelea kuimaintain(If you know what am talking about).Sasa hivi ukichukua miziki yake yote na ukafuta chorus zote ukaanza kusikiliza,hautajua kama ilikuwa miziki tofauti.

Otherwise he is doing good.
 
kweliiiiiiiiiiiiiii!

Yani kila siku uwa nabishana na watu kwa kuwambia roma rhymes zake ni direct sana kitu kinachozifanya ziwe kawaida sana.
Halafu style na mambo anayoyaongelea ni yale yale na kwa style ile ile na beats zake ni zile zile yani sioni utofauti wa nyimbo zake.
Kwa upande wangu simkubari ila kuna wimbo alishirikishwa na kala jeremayah verse ya roma niliipenda sana wimbo wenyewe unaitwa wosia
 
Mimi sio Roma. ni shabiki tu nilieamua kuusikiliza na kuuchambua...

na wewe unaruhusiwa kuchambua iwe kwa mema au mabaya
 
Aiseeeeeeee babayangu hiyo ngoma bado haijafika hiku kwetu mkuu rombo kijiijini
wapenda haki naomba mwiweke humu jf niweze kuinyoja nitaitwanga kama dozi ya marelya yani kutwa mara 3 asubui mchana na jion

na tena vile jirani yagu ni gamba ataweka pamba masikion
 
Kasikilize Miss Tanzania na Homa ya dunia za Solo Thang ndo utaelewa mkuu sixgates alikuwa anamaanisha kitu gani.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums

kaka homa ya dunia ushaulizwa unajua alikokopi mistar? labda gemu ya bongo umeanza ckiliza juzi, hukuwepo enzi hizo, kuna kitabu kinaitwa homa ya Dunia, ndiko alikokopi mashairi na mwenye kitabu alimfikisha mahakamani solo thang...na kama kumbukumbi zangu ziko poa, solo alilipa faini baada ya kikiri, kitabu cha homa ya Dunia kiliandikwa na mchungaji mmoja wa kisabato akiitwa Nyagori, hv sasa ni marehemu.

nikiacha taarifa hiyo, kuhusu roma niseme ukitoa ujumbe beat is poor tena nikopi ya nyimbo zake za awali, then is static habadiliki, yani hata kama mtu anastyle inayomtbulisha , ua roma ina bore maana kama alivosema mdau mmoja hapa, ukiunganisha nyimbo zake ukatoa chorus, hutofautishi...otherwise meseji imefika.
 
Ukikamshifu roma utakuwa safarini kwenda mirembe,tukutakie safari njema.Kaza buti bb Roma wenye shida na dhiki zilizoletwa na hao akina ben na mrisho tuko nawe mia mia.KOMAA TUPA NDONGA
 
Mi naamini kama kweli tunasikiliza ujumbe katika Nyimbo basi.KWA TANZANIA SASA HAKUNA MSANII WA HIPHOP MWENYE MASHAIRI YANAYOIGUDA JAMII MOJA KWA MOJA KAMA ROMA.

''Wanasema Tuzo sikustahili kwani tuzo ina sarafu ya nani?? vya kaisari Mpeni kaisari''
 
sie wanafki.. Msanii akibadilika napo anapondwa... Mfano ni prof jay alipotoa single na marko chali... Watu walimponda sana..

Well said,ukiisoma ngano ya punda binadamu hawezi kukusumbua kwa longolongo zake na hata mwanamziki wa zamani alishaimba "Binadamu hatosheki hata umpe nini milele hatoridhika" kama Hamuijui Simulizi ya Ngano ya Punda Just quote or mention me"
 
sie wanafki.. Msanii akibadilika napo anapondwa... Mfano ni prof jay alipotoa single na marko chali... Watu walimponda sana..

Mkuu tunaposema kubadirika hatuna maana aimbe takeu au miziki ya akina bob jr, tunamaanisha kuwepo na tofauti kati ya track zake hata ukisikiliza ukiwa mbali ujue hii ni track flani na ile ni flani.
Nyimbo za roma zinafanana. kila mtu ana style yake ya kushusha mistari lakini haimaanishi track zake zitafanana.
Mfano ukisikiliza nyimbo za darasa usikate tamaa na nishike mkono japo flow ni ile ile lakini utazitofautisha tu.
Any way ni mtazamo tu the kid is still doing good
 
Mwimbaji wa mziki kwa Jina al-maaarufu " ROMA MKATOLIKI " ni zaidi ya Baadhi ya wabunge wengi saana wa Tanzania .

Kwa kuaangali ujumbe anaofikisha Roma katika jamii juu ya machafu yanayofanywa hapa nchini,ROMA atabaki kuwa Positive kwa Kulinganisha na Baadhi ya wabunge wanaojifanya Wanauchungu na ukombozi wa Tanzania kumbe ni Wabunge Maslai tu na Wanafiki wanaohudhuria vikao vya bunge kungoja Posho na Mishahara Iongezwe wapige Makofi.

ROMA ni zaidi ya wabunge 20. Kutoka vyama vyote ( kwa uwezo wa kufikitia )

BIG UP ... ROMA.
 
Roma ajawai kutoa ngoma mpya,sijaona kipya kabisa hapo,ukisikiliza tangia anatoka hadi sasa anaimba kitu kilekile na flow ni ileile ya makelele..zaidi ni muendelezo wa kutumia majina ya watu maharufu kuyataja negatively ili apate atenshen...labda kipya ni kawachana waislam which is so bad.

huyu Roma anataka sifa za kijinga sana sana....me pia sijawahi one kitu kipya kwake zaidi ya theme ile ile na kutaja majina ya watu maharufu apate sifa za kizushi! kwani nyimbo haiewezi kuhit bila kumtaja riz, jk au slaa?? mbona hamtaji Slaa anayechukua wake za watu au Mbowe aliyemjaza mimba mwanachama wa chadema? au yule boya wa Mwanga aliyebaka mtoto wa miaka 17 mbona hawataji humo???? dogo atapotezwa sana yani kawasema vibaya sana waislamu ngoja wazee wa uamsho wampate
 
Tupia shairi hizo mwana!

Song: Wazo La Leo
Artist: Stamina Feat Fid Q
Studio: Bongo Records
Producer: P funk Majani
Song Writters: Stamina (verses) & Fid Q
(chorus)
Intro...
U know what majani??nice to meet you
homie
Its moro town baby,,,shorobwenzi
Verse 1. (Stamina)
Elimika nyangema, maisha
hayaendeshwi na nguo
Pesa ni vazi la mgema, haliwezi kuwa
na mpasuo
Vaa uaminifu,tupa boksi la kondomu
Hip hop haijengwi na
bifu,underground usijaze fomu
Maisha ni kujipanga, mganga usigawe
irizi
Viongozi msizuie ganja, huku
mnachukua ushuru wa rizz
Ridhiki ina kamba, ivute ili ikupe noti
Mkulima rudi shamba,dec mbegu siku
hizi hazioti
Maisha njia panda,mtembezi chagua
pa kwenda
Uchumi vazi la bwanga,ukishuka uvishe
suspenda
Shiba kwa nia,ukiwa mlafi wa malengo
Usikufuru we shukuru ukifaulu kila
tendo
Punguza pupa,mpendaji uingie ndoani
Mapenzi yamevaa bukta,uswazi mapaja
hadharani
Usilale kijinga,kwenye kitanda cha
ushamba
Unaweza kuwa shabiki wa samba,na
ukaishi mwembe yanga
Chorus. (Fid Q)
Hiki kijiko unachokiona,baada ya kula
kwa mkono
Ndomu usiyoiona,mpaka ukishafanya
ngono
Neno la kuponya,lilokosa mdomo
Na hili bonge la ngoma,kwenu kwangu
ni kama somo
{Hilo ndo wazo la leo}-inshu usingizi
wa furaha,mzinzi jenga kibanda cha
angaza utoe nasaha.
{hilo ndo wazo la leo}-usiishi kwa
vikwazo,weka wazo kwenye vyanzo
vyako-{hilo ndo wazo}
Verse 2. (Stamina)
Underground panga tenzi,ustar hauji
kwa promo
Hakuna tajiri wa mapenzi,kapuku
punguza ngono
Bora uitwe mfalme jua,kwenye utawala
wa kishamba
Mapenzi yakikusumbua,tafuta daktari
wa kitanga
Vazi unaloishi,mwenyezi yeye ndio
disegner
Shetani akikushawishi, mvute kwake
kama dayna
Dunia duara,jitahidi uizunguke
Mla bata starehe hasara,,wekeza hadhi
isishuke
Huna undugu na bakhersa,niaje aje
unakula unga
Mateja wanahitaji sensa,taifa la kesho
linavunda
Dogo jifunze,heshima sio upaparazi
Mwambie na dada ajitunze,mlango
wake asiuache wazi
Kama unajijua ni mchoyo,basi usingoje
kupewa
Tafuta pesa kwa moyo,sio kwa ushindi
wa ngekewa
Sharo mpe salamu,the great braza
kanumba
Mwambie bongo sio tamu,na lulu
bado wamemfunga
Chorus(fid q)
Hiki kijiko unachokiona,baada ya kula
kwa mkono
Ndomu usiyoiona,mpaka ukishafanya
ngono
Neno la kuponya,lilokosa mdomo
Na hili bonge la ngoma,kwenu kwangu
ni kama somo
{Hilo ndo wazo la leo}-inshu usingizi
wa furaha,mzinzi jenga kibanda cha
angaza utoe nasaha.
{hilo ndo wazo la leo}-usiishi kwa
vikwazo,weka wazo kwenye vyanzo
vyako-{hilo ndo wazo}
Verse 3. (Stamina)
Utamu wa ndafu ya harusi,sio wa ndoa
we kilaza
Mbuzi atabaki mbuzi,hata mle hadi
mkasaza
Nchi tayari imekonda,mwananchi
tafuta ulaji
Life ngumu hadi omba omba,kidonda
anafanya mtaji
ukipata mazuri,jipange kuikwepa
hasara
kijana vazi la msuli,haliwezi kukuvisha
busara
ukiishi kwa hisia,kila stone litakubanza
cha msingi ni kuweka nia,ujivue kuwa
mtanza
kata ya kijiji,haibebi maji ya maendeleo
katibu tunza mkwiji,msuli ukishuka
kimeo
uchumi umeshika tama,kwenye shavu
la mlanguzi
raia usilaumu chama,shiriki kwenye
uchaguzi
unaweza ukavaa kinga,ila ukafa kwa
uaminifu
mzinzi usigawe ujinga,sambaza
ujumbe wasifu
hakuna snitch kama pesa,ukiwa nae
fanya vya maana
akiondoka atakutesa,utamsaka usiku
na mchana
Chorus. (Fid Q)
Hiki kijiko unachokiona,baada ya kula
kwa mkono
Ndomu usiyoiona,mpaka ukishafanya
ngono
Neno la kuponya,lilokosa mdomo
Na hili bonge la ngoma,kwenu kwangu
ni kama somo
{Hilo ndo wazo la leo}-inshu usingizi
wa furaha,mzinzi jenga kibanda cha
angaza utoe nasaha.
{hilo ndo wazo la leo}-usiishi kwa
vikwazo,weka wazo kwenye vyanzo
vyako-{hilo ndo wazo}
 
Back
Top Bottom