ushuru

  1. Mi mi

    China yatangaza nyongeza ya asilimia 84% ya ushuru kwa bidhaa za Marekani

    Kazi bado inaendelea ni vuta nikuvute kati ya utawala wa Trump na nchi ya China katika vita vya ushuru. BREAKING: 🇨🇳🇺🇸 China announces additional 84% tariff on US goods. https://x.com/WatcherGuru/status/1909925306560885110?t=-ienhln5-MyLFFrJ4DBwBQ&s=19
  2. Sir John Deere

    Kwanini katika nchi zote Trump alizozipandishia ushuru Russia haipo?

    Kwa anayejua Tafadhali katika mkeka alioutoa Bwana Trumpet ameorodhesha nchi zote lakini Russia haipo je kulikoni? Hebu mwenye ufahamu aje atueleze hapa.
  3. X

    Alichosema Trump baada ya Marekani kuiongezea ushuru China kufikia 104%: Tunasubiri simu zao

    "Tunasubiri simu zao" hivyo ndivyo Trump alivyopost kwenye akaunti yake baada ya Marekani kuongeza ushuru kwa China kufikia 104% Tangu mwanzoni kabisa Trump alipoanza kuiongezea ushuru China, serikali ya China ilishasema; China itapambana hii vita mpaka mwisho. Trump aache kuwazia eti kuna...
  4. L

    China yaitikia vita ya ushuru ya Marekani ili kutetea haki

    Katika kipindi muhimu cha ufufuaji wa uchumi wa dunia, Marekani imetumia tena rungu la ushuru, ikiamua kutoza ushuru ambao inauita "sambamba" kwa washirika wake wote wa biashara duniani, ambapo ushuru wa bidhaa kutoka China utafika hadi 34%. Ikikabiliana na hatua hii ya kimabavu ya wazi, China...
  5. Tman900

    Ushuru wa Gari, TRA ni 80% Hadi 100% na zaidi

    Ushuru wa kuingiza Gari Tanzania uko Juu sana Kuliko Zanzibar, pia Kumiliki gari kama Anasa,ila kiuhalisia gari sio Jambo la anasa Gari ni Chombo Cha usafiri kukutoa Sehemu Moja kwenda Sehemu nyingine. Kua na ushuru mkubwa sababu ni Nini.
  6. Mwanongwa

    Mbeya: Baada ya mgomo wa daladala kutolipa ushuru, hatimaye Stendi ya Nanenane yaanza kurekebishwa

    Baada ya malalamiko ya muda mrefu na baadae kusababisha madereva kugoma kulipa ushuru , hatimaye halmashauri ya Jiji la Mbeya imeanza kurekebisha barabara za stand hiyo. Ni muda mrefu Sasa stand hiyo na Nanenane imekuwa na miundombinu mibovu ya Barabara. Halmashauri ya jiji jitahidi kufanya...
  7. Mi mi

    Wakulima wa Kimarekani walalamikia majibu ya China ya nyongeza ya ushuru wa 15% kwa bidhaa

    Baada ya China kujibu mapigo kwa nyongeza ya ushuru wa 15% kwa bidhaa za kimarekani baada ya serikali ya Donald Trump kuiwekea ushuru kwa bidhaa za China zinazo ingia marekani athari za majibizano ya nyongeza za ushuru kati ya serikali ya Washington na Beijing za wakumba wakulima wa kimarekani...
  8. Carlos The Jackal

    Baada ya Canada kulipiza Kwa kuweka ushuru wa 25% kwenye Umeme , Trump kaongeza Ushuru kutoka 25% Hadi 50% Kwa Chuma na Aluminum ya Canada

    Na Mwamba ndo kwanza anazidi kutoa Onyo!! Inawezekana kwa Trump, Dunia yote ikapigishwa Magoti.
  9. Ritz

    Trump anasema ataiwekea Urusi vikwazo vikubwa, vya ushuru kumaliza vita vya Ukraine.

    Wanaukumbi. Machi 7 (Reuters) - Rais wa Marekani, Donald Trump alisema Ijumaa "anazingatia sana" kuweka vikwazo vikali, vikiwemo vile vya benki, na ushuru kwa Urusi hadi makubaliano ya kusitisha mapigano na amani yafikiwe na Ukraine. Trump pia amesitisha usaidizi wa kijeshi na ushirikiano wa...
  10. L

    Ni upuuzi kwa Marekani kuongeza ushuru kwa nchi nyingine kwa kisingizio cha Fentanyl!

    Wiki hii, serikali ya Trump ilitangaza tena kuongeza ushuru wa 10% kwa bidhaa za China zinazouzwa Marekani kwa kisingizio cha suala la Fentanyl na mengineyo, huku pia ikiongeza ushuru wa 25% kwa bidhaa kutoka Canada na Mexico. Hatua hii sio tu kwamba ilisababisha pingamizi kutoka kwa China na...
  11. Lycaon pictus

    Ushuru wa USA kwa Canada, Mexico na China vimeanza kufanya kazi rasmi

    Baada yakusitisha kwa mwezi mmoja, Trump kasema Canada na Mexico hawajafanya lolote kuboresha hali ya mipakani. Basi ushuru wa 25 percent kwa bidhaa kutoka Canada na Mexico umeanza kufanya kazi rasmi. China imeongezewa ushuru kufikia asilimia 20, toka 10. Waziri mkuu wa Canada ameongea na...
  12. P

    Ushuru wa magari na online TRA calculator

    Mimi binafsi napotaka kuagiza gari, nachukua details za ile gari halafu nakuja kukadiria bei ya ushuru kupitia Calculator ya TRA, tuseme napata Mil 12,355,000 kama ushuru. Unaagiza gari baada ya wiki tatu ushuru unaongozeka kidogo hadi mil 13+ kawaida kabisa kutoka na value ya USD KUPANDA NA...
  13. Mad Max

    Battle la Compact SUV: Mazda CX-3 vs Honda Vezel. CIF karibia zipo sawa, ila Ushuru wa TRA mmoja amedabo!

    Kwa wapenzi wa compact SUV kuna haya magari mawili, Mazda CX-3 na Honda Vezel. Ingawa ni taste mbili tofauti, lakini yanaweza kufananishwa ata kwa udogo. Mazda CX-3 yeye ana sifa zifuatazo: Engine: 1.5L SkyActiv-D diesel engine, inatoa power ya 105 hp Transmission: 6-speed manual au...
  14. K

    Msaada: Makisio ya kodi na ushuru bandarini

    Wakuu wazima? Katika process za kutoa kontena bandarini, naomba mwenye uelewa anifungue macho hapa. Ni kodi zipi na asilimia ngapi hulipwa kwa kontena la 40HQ, mzigo ni machines za kiwandani, rawmaterials na packages. Itapendeza kama nikipata mchanganuo wa gharama zote. Natanguliza shukrani..
  15. kwisha

    Canada yakataa kusalimu amri kwa Rais Trump kuhusu ushuru wa 25%

    Rais wa Marekani, Donald Trump, alitangaza kuwa anapanga kuweka ushuru wa 25% kwa bidhaa kutoka Canada na Mexico, pamoja na ushuru wa 10% kwa bidhaa kutoka China. Trump alieleza kuwa hatua hii inafanywa kama njia ya kulinda mipaka ya Marekani dhidi ya uhamiaji haramu na madawa ya kulevya ambayo...
  16. Chaz Joe

    Nahitaji kufahamu gharama za ushuru wa TOYOTA NOAH bandarini zikoje?

    Habari wapendwa, nahitaji kumiliki gari aina ya Toyota Noah. Naona ndiyo inayonifaa kwaajili ya kuendesha mishemishe zangu. Ningependa kwa yeyote ambae anafaham chochote kuhusu gharama za kuagiza hiyo gari na kodi zote tafadhali nijuze
  17. Offshore Seamen

    Ukiagiza bidhaa au gari na ukakwama ushuru ni vyema baada ya gari kufika ukapeleka Bonded Warehouse

    Kama umeagiza gari au bidhaa na ikawa imefika Kwenye Bandari na wakati huo pesa ya ushuru umepungukiwa,kukwama au hukuwa na taarifa sahihi za ushuru na makadirio ya kodi yamekuja zaidi ya kiwango ulichopanga njia sahihi ni kumwambia wakala wa Forodha(Clearing Agent) afanye maombi (TRA) ya...
  18. Mtukutu Mkuu

    TUPENI ABC Kwa sisi tunaotaka kuagiza laptop Zanzibar ushuru ukoje

    Kama Kichwa kinavyojieleza hapo nataka kuagiza laptop Zanzibar au naweza kwenda mwenyewe nikabeba kwenye begi Je Bei ya ushuru ipoje na kama mzigo nimeweka kwenye begi bado nitatozwa ushuru Nawasalisha Kama Upo Zanzibar/Pemba tafadhari karibu dm
  19. S

    Trump aziambia nchi za umoja wa ulaya zinunue gesi na mafuta zaidi kutoka Marekani au ataongeza ushuru kwa bidhaa za kutoka jumuiya hiyo

    Rais mteule wa Marekani Donald Trump ameonya kuongeza ushuru kwa bidhaa za jumuiya ya Ulaya zinazoingia Marekani endapo jumuiya hiyo haitaongeza viwango vya mafuta na gesi inavyonunua kutoka Marekani. Trump alitoa taarifa hiyo kupitia post katika mtandao wa Truth aliyoichapisha Alhamisi usiku...
  20. L

    Ushuru wa Trump kwa nchi washirika wake wa kibiashara huenda ukaifanya Marekani iishie kujipiga risasi yenyewe mguuni

    Rais mteule wa Marekani Donald Trump akiwa sasa yupo kwenye maandilizi ya kurejea tena kushika usukani na kuliongoza taifa la Marekani Januari mwaka 2025, ameanza kujenga uhasama na nchi washirika wake wa kibiashara kwa kutoa vitisho kwa nchi mbalimbali duniani, huku akitilia mkazo sera ya...
Back
Top Bottom