Akiwa katika mahojiano ya kipindi cha Dakika 45 ITV Septema 8, 2025, Professor Kitila Mkumbo alisema haya kuhusu suala la utekaji na ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM)
"ilani ya CCM ina vipaumbele tisa, kwa mfano kipaumbele cha sita ni kudumisha demokrasia na utawala bora, hapa tunazungumzia...
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini kupitia Chama cha ACT Wazalendo, Kiza Mayeye, amesema iwapo wananchi watampa ridhaa ya kuwa Mbunge wao, atahakikisha anapigania maslahi ya wananchi kwa kuhakikisha bajeti zinazopitishwa bungeni zinawagusa moja kwa moja wananchi na si kufujwa kwenye...
Jeshi la Polisi Mkoani Shinyanga limekamata viongozi wa Chadema waliokuwa kwenye Kaburi la Bob Nyanga Makami wakifanya usafi huko Ukenyenge.
Walioshikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoani humo katika kituo cha ukenyenge ni hawa wafuatao;
1. Jackson Mnyawami Mnyawami Katibu wa kanda ya serengeti
2...
Mgombea urais kupitia Chama cha Wakulima (AAFP), Kunje Ngombale Mwiru, ameahidi kununua helikopta kwa kila wilaya nchini zitakazotumika kusaidia shughuli za uokozi kwa Watanzania watakaokumbwa na mafuriko.
Wakazi wa mkoa wa Songwe wameshukuru na kupongeza juhudi za Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kuwakumbuka makatibu wake kwa kuwakabidhi pikipiki mpya, maarufu kama Pikipiki za Mama.
Wakazi hao Wanasema hizo zimeleta mabadiliko makubwa ya kasi na ufanisi katika utendaji wa kazi za chama mashinani...
Mgombea urais wa Chama cha UPDP, Twalib Kadenge amewashangaza wananchi wa Mwanza kwa staili yake ya kampeni ya kucheza muziki kila baada ya kutoa ahadi moja na kuzungumzia sera za chama chake.
Akizungumza amesema, "UPDP ikipewa ridhaa ya wananchi, mtoto kuanzia darasa la 1 mpaka la 7 atasoma...
Prof. Kitila Mkumbo, Mwenyekiti Kamati ndogo iliyoandaa ilani ya CCM, akihojiwa na ITV anukuliwa akisema, "Tunashindana na vyama 17 Watanzania waelewe nchi hii ni ya vyama vingi sio vyama viwili.....huko Marekani ni nchi ya vyama viwili sio Tanzania."
Aliyekuwa Waziri kwa Serikali za awamu tatu na Mbunge wa jimbo la Tanga kwa tiketi ya CCM Ummy Mwalimu, amesema roho yake nyeupe hata kama jina lake limeenguliwa na badala yake ataambatana na aliyeteuliwa kuhakikisha anapata nafasi ya Ubunge ili aweze kuendeleza miradi ya maendeleo aliyoiasisi.
Aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Arusha, Cecilia Pareso, ambaye pia aligombea Ubunge wa Jimbo la Karatu lakini hakufanikiwa kupata kura za kutosha katika uchaguzi wa ndani uliompa ushindi Daniel Awaki, ameonesha ukomavu wa kisiasa kwa kupanda jukwaani kwa mara ya pili kumuombea Awaki...
Mwanasheria mkuu wa CHADEMA, Rugemeleza Nshala amesema Mwenyekiti wa chama hicho, Tundu Lissu amewasilisha mapingamizi mawili Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Dar es Salaam ikiwemo kupinga mwenendo wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Bukoba Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mhandisi Johnston Mtasingwa, aliomba kura kwa wananchi mbele ya mgombea mwenza wa Urais wa chama hicho, Dkt. Emmanuel Nchimbi, katika mkutano wa kampeni uliofanyika jana kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Kashai, mjini Bukoba.
Mgombea wa Kiti cha Urais Zanzibar kupitia chama AAFP, Said Soud alisema hayo tarehe 3/09/2025 wakati anamjibu Mgombea wa Urais Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia tiketi ya Chama Cha ACT wa Wazalendo Othman Masoud Othman anayedaiwa kutoa kauli za kichochezi na kukejeli sheria za uchaguzi...
Kesi ya uhaini dhidi ya Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu Lissu imeahirishwa hadi kesho Septemba 9, 2025 baada ya kuomba muda zaidi kupitia nyaraka za committal proceedings.
Lissu aliwasilisha hoja kuwa nyaraka alizopewa akiwa gerezani zinatofautiana na zile alizokabidhiwa leo na Mahakama Kuu...
Vyombo vya habari na waandishi wa habari wameshauriwa kuepuka kutumia lugha za chuki, uchochezi au zinazoweza kugawa jamii kwa misingi ya ukabila, dini au itikadi katika kipindi hiki cha kuelekea kampeni za uchaguzi.
Soma pia: ZEC: Vyama Visivyosaini Maadili ya Uchaguzi Havitaruhusiwa Kufanya...
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), John Heche amesema Chama hicho hakitokubali kuona Mwenyekiti wao Tundu Lissu anahukumiwa kwa kesi za kutengenezwa.
Heche ameyasema hayo leo Septemba 8 baada ya kuahirishwa kwa kesi ya uhaini inayomkabili Lissu ambaye tayari leo...
Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma inatarajiwa kutoa hukumu ya Shauri Namba 21692 la mwaka 2025 kati ya Bodi ya Wadhamini wa chama cha ACT-Wazalendo na Luhaga Joelson Mpina dhidi ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali siku ya Alhamisi, tarehe 11 Septemba 2025...
Taasisi ya Jamii Mpya Tanzania imetangaza mpango kabambe wa kitaifa wa kuhamasisha wananchi kushiriki Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, ikilenga zaidi vijana na wanawake, huku ikipinga vikali miito ya kisiasa inayotaka wananchi wasusie uchaguzi huo.
Mratibu wa Kitaifa wa taasisi hiyo, Ally...
Katika kampeni zinazoendelea hivi leo mkoa wa Kigoma, Chama cha ACT wazalendo kikiwa katika ufunguzi wa kampeni hizo limeibuka wimbi la wananchi wakimtuhumu Serukamba kuwa ni anatoa rushwa ili apate kura.
Kelele hizo zilisikika mara baada ya Mambo kupanda jukwaani nakuanza kumnadi Kiza Mayeye...
Monicka Ndungulu, mkazi wa Kata ya Mji Mwema katika Halmashauri ya Mji wa Njombe na mwanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), amesema kwamba licha ya chama chake kutojihusisha na uchaguzi, wananchi wa kata hiyo wanapaswa kuchagua kiongozi mwenye maono badala ya kuangalia itikadi...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.