GE2025 Cecilia Pareso: Awaki alinishawishi nitoke CHADEMA nirudi CCM

GE2025 Cecilia Pareso: Awaki alinishawishi nitoke CHADEMA nirudi CCM

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Wild Flower

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2023
Posts
969
Reaction score
1,939
Aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Arusha, Cecilia Pareso, ambaye pia aligombea Ubunge wa Jimbo la Karatu lakini hakufanikiwa kupata kura za kutosha katika uchaguzi wa ndani uliompa ushindi Daniel Awaki, ameonesha ukomavu wa kisiasa kwa kupanda jukwaani kwa mara ya pili kumuombea Awaki kura kwa wananchi wa Karatu.




Pareso ameeleza kuwa kurejea kwake CCM kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kulitokana na ushawishi wa Awaki. Hivyo, amewataka wananchi wa Karatu kumuunga mkono Awaki ili aendelee kuwa Mbunge wao. Aidha, amesisitiza kuwa ni muhimu wananchi kumpa kura za kutosha Awaki pamoja na Mgombea Urais kupitia CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na wagombea wa nafasi za Udiwani wa CCM.
 
Chadema ilikua inafuga watu wa ajabu sana, nashukuru Lissu kasafisha uchafu wote. Otherwise hata huu uchaguzi kuna wagombea ubunge wangechukua fomu mpaka mgombea urais angepewa fomu na NEC bila hata kamati kuu kuridhia!!
 
Back
Top Bottom