uchaguzi mkuu 2025

No Wikipedia entry exists for this tag
  1. DuaZaMama

    PostGE2025 Jamaa aliyehusishwa na mauaji ya watu wakati wa maandamano akanusha, anadai kuwa yeye ni dereva

    Mwanaume ambaye amekuwa akitrend kwa siku mbili mfululizo baada ya kuhusishwa na kikundi cha watu waliokuwa na silaha na wanaodaiwa kuhusika katika mauaji ya waandamanaji wakati wa maandamano siku ya uchaguzi, amejitokeza na kujitetea kupitia video ambazo kwa sasa zinasambaa kwa kasi mtandaoni...
  2. Just Pray

    GE2025 Video: Polisi wakifuata vijana wa kiume majumbani huko Mara

    Ujumbe uliochapishwa na Mange Kimambi kwenye ukurasa wa Instagram. "Dada Mange moyo wangu unavuja damu, Watanganyika tumekuwa watumwa kwenye nchi yetu wenyewe. Tumekuwa mayatima, hakuna jeshi la kutusaidia, hatuna viongozi tuko wananchi kujipigania wenyewe Hapo ni Nyamongo North Mara. polisi...
  3. Influenza

    GE2025 Wakazi: Tusiiombee Tanzania, tuipiganie. Msije na #PrayforTanzania kama trend tu!

    Msanii Wakazi kupitia Ukurasa wake wa X (twitter) amewasihi Wananchi kuipigania Tanzania yao badala ya kuandia hastags tu kama trends. Amesema hakuna uhalali wowote wa watu kuuawa hata kama kuna vitu viliharibiwa. Anasema; DONT PRAY FOR TANZANIA… FIGHT FOR IT! Hakuna Mtu perfect, na ni kweli...
  4. Black Opal

    PostGE2025 Muhtasari Taarifa ya Awali ya Uchaguzi Mkuu Tanzania 2025 kutoka SADC (SOEM): Uchaguzi haukutimiza Viwango vya Uchaguzi wa Kidemokrasia vya SADC

    Hapa chini ni muhtasari wa taarifa ya awali (final) ya waangalizi wa Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 kutoka SADC (SEOM), uliowasilishwa na Richard Msowoya, Spika wa zamani wa Bunge la Malawi na Mkuu wa Ujumbe wa Waangalizi wa SADC. Upo kwa kifupi na kwa Kiswahili, ukitaka maelezo zaidi pitia...
  5. Keynez

    Muuaji anavaa jezi ya Yanga anaenda kuua mamia ya Watanzania mchana kweupe, halafu Klabu haitoi hata neno la kukemea wala kusikitika

    Hii nchi niliwahi kusema ukielewa how deep hizi timu za Simba na Yanga zinavyotumika kupumbaza na kuumiza Watanzania, wengi mtalia sana. Yule jamaa aliyevaa jezi ya Yanga aliyetoka akaenda na wenzake kumiminia watu risasi za vichwa hakuamka tu akaamaua avae jezi ya Yanga na wala hakushtuliwa tu...
  6. Waufukweni

    GE2025 Prof Tibaijuka: Tuwazike kwa heshima, tuombe toba kuondosha sifa za Taifa letu kwa kutotambua HAKI ndiyo msingi wa yote

    Profesa Anna Tibaijuika ambaye ni Waziri wa zamani wa Ardhi, Nyumba na Makazi katika Serikali ya awamu ya nne chini ya Dr. Jakaya Kikwete, ametuma salamu za pole kwa Watanzania wote waliofikwa na madhara ya maandamano ya October 29 na kushauri kwamba wote waliofariki wazikwe kwa heshima...
  7. PAYE

    GE2025 Kawaida: Video zilirekodiwa na nani, kama waliohamasisha maandamano hawakuwepo barabarani? Swali kwako

    Mwenyekiti wa UVCCM Taifa kupitia ukurasa wake wa Instagram anasema waliohamasisha maandamano hawakuwepo barabarani — lakini video zipo, sauti zipo, nyuso zipo. Kama si wao, ni nani aliyerekodi? Na kwa nini misiba ya waliokufa kwa risasi inageuzwa jukwaa la lawama badala ya tafakari ya Taifa?
  8. Waufukweni

    GE2025 Video: "Hizo risasi hizo" Wananchi wakienda kumzika mwenzao aliyepigwa risasi na Polisi

    Mazishi ya Mwananchi aliyeuawa kikatili kwa kupigwa risasi na polisi yamegeuka kuwa maandamano ya sauti na hisia. Wananchi waimba “Hizo risasi hizo” wakieleza uchungu, hasira, na wito wa uwajibikaji kwa mamlaka.
  9. DuaZaMama

    PostGE2025 Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF)latoa pole na wito wa haki baada ya vurugu na vifo vilivyotokana na Uchaguzi Mkuu 2025

    POLENI WATANZANIA, TUJISAHIHISHE Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) linafuatilia kwa karibu na limepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za vifo vya Watanzania wenzetu, wakiwamo wanahabari na wengine waliojeruhiwa.Siku ya tukio tulipokea taarifa za vifo vya vijana na askari polisi. Baadhi ya...
  10. DuaZaMama

    PostGE2025 Lipumba: Kama CCM na Samia wanapendwa na wananchi kwanini aliapishwa KINYEMELA?

    Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, ameshangazwa na ushindi wa asilimia 97 aliopatikana na mgombea wa urais kupitia CCM, Samia Suluhu Hassan, katika uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 29, 2025. Lipumba amesema kuwa ni ushindi mkubwa ambao haujawahi kutokea tangu...
  11. R

    Steve Nyerere: Ni unafiki Wasanii kufuta picha za kampeni CCM, mnadhani wataacha kuwatukana? Tayari Rais tunaye

    Msanii wa Bongo Movie Steven Nyerere kupitia ukurasa wake wa Mtandao wa Instagram ameandika kuhusiana na Muenendo wa wasanii wengi kufuta picha zao wakiwa katika kampeni za Chama cha Mapinduzi (CCM) akisema ni unafiki na kutokuwa na msimamo "Mstafuuu,....Nimeona Wasanii wengi Wanafuta Picha za...
  12. W

    GE2025 CUF: Matokeo yaliyotangazwa ni matokeo ya kupikwa. Washangazwa Rais Samia kupata kura zaidi ya Nyerere wakati wa chama kimoja

    Akizungumza na waandishi wa habari, Mwenyekiti wa chama hicho Prof. Ibrahim Lipumba kwa niaba ya chama chake cha Civic United Front, amesikitishwa na matokeo hayo yaliyomtangaza mgombea wa CCM kupata kura 97.66%. Prof. Lipumba amesisistiza kuwa matokeo hayo ni ya kupika na hayawakilishi...
  13. DuaZaMama

    PostGE2025 Chama cha Civic United Front (CUF) chataka uwepo wa serikali ya mpito, Uchaguzi uliofanyika ni UBAKWAJI wa DEMOKRASIA

    Chama cha Wananchi (CUF) kimetaka kuundwa kwa Serikali ya Mpito (Caretaker Government) ya Tanzania itakayosimamia mabadiliko ya kikatiba na maandalizi ya uchaguzi huru na wa haki, kikikataa matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 kwa madai kuwa haukuwa huru, wa haki, wala wa kuaminika...
  14. R

    GE2025 Edwin Soko: Waandishi wa habari walijawa hofu ya Sheria za nchi na Maadili kuripoti Matukio Oktoba 29

    Edwin Soko Mwenyekiti wa Taasisi ya Vyombo vya Habari nchi za Kusini mwa Afrika, akizungumza Novemba 5, 2025 katika Mjadala wa Nafasi ya Vyombo vya habari katika Uchaguzi wa Tanzania uliofanyika Oktoba 29, 2025 na kuambatana na vurugu za Maandamano ambapo Vyombo vya habari vilikaa kimya na umma...
  15. R

    GE2025 RPC Maigwa: Hakuna Mwananchi wala Askari aliyeumizwa Oktoba 29 Kilimanjaro

    Jeshi la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro limeeleza kuwa hakuna mwananchi au askari Polisi wa Jeshi hilo Mkoani humo aliyejeruhiwa au kupoteza maisha kutokana na Vurugu zilizotokea siku ya Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro SACP Simon Maigwa ameeleza hayo Novemba 4...
  16. R

    GE2025 Chacha Heche: Viongozi wa CHADEMA wanakamatwa na kupewa kesi ya kuratibu na kuchochea Maandamano ya Oktoba 29

    Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Mara, Chacha Heche akizungumza leo Novemba 5, 2025 katika Mahojiano na Chombo cha habari DW ameeleza hali wanayopitia viongozi wa CHADEMA wakikamatwa kwa kuhusika kupanga na kuhamasiha Maandamano yaliyofanyika Oktoba 29, 2025...
  17. R

    GE2025 James Mbatia: Je, leo hii damu inamwagika kwa ajili ya Madaraka tu? ni laana kwa Taifa

    Mwanasiasa na Mwenyekiti wa zamani wa Chama cha NCCR Mageuzi, James Mbatia akizunguzma leo Novemba 5, 2025 ametoa Pole kwa Taifa kwa vifo vya kikatili vilivyotokea Oktoba 29, 2025 wakati wa Maandamano nchini. Pia amesikitishwa na hali ya kisiasa inayoendelea nchini ambayo imekuwa ya kumwaga...
  18. DuaZaMama

    PostGE2025 Polisi Kilimanjaro yawaachilia huru vijana 300 waliokamatwa kwa kudaiwa kushiriki maandamano ya Oktoba 29

    Jeshi la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro limeeleza kuwa liliwashikilia vijana 300 kutoka maeneo mbalimbali mkoani humo kutokana na kudaiwa kushiriki vurugu zlizotokea siku ya uchaguzi mkuu Oktoba 29,2025. Limesema kuwa baada ya kuwashikilia baadae liliwaachilia huru bila masharti yoyote, kutokana na...
  19. Mkalukungone Mwamba

    GE2025 CHADEMA watangaza siku 7 za maombelezo na bendera kupepea nusu mlingoti kwenye ofisi zao zote

    Mkurugenzi wa mawasiliano na uenezi wa CHADEMA Brenda Rupia amezungumza na watanzania na kutoa pole kwa niaba ya chama na wametangaza maombelezo ya siku 7 na bendera kupepea nusu mlingoti kwenye ofisi zao zote. Nchi yetu ilishuhudia maandamano ya amani yalifanywa na wananchi yalikuwa...
  20. Waufukweni

    GE2025 Baadhi ya Watanzania wanaoishi Uholanzi wameandamana nje ya Mahakama ICC kupinga mauaji ya Watanzania

    Maandamano ya baadhi ya Watanzania wanaoishi Uholanzi yameripotiwa kuanza muda huu nje ya Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) mjini The Hague. Waandamanaji wamebeba mabango wakipinga kile wanachokiita mauaji ya raia nchini Tanzania, na wakitaka uchaguzi ufutwe ili, kwa madai yao, “wananchi...
Back
Top Bottom