Mwanaume ambaye amekuwa akitrend kwa siku mbili mfululizo baada ya kuhusishwa na kikundi cha watu waliokuwa na silaha na wanaodaiwa kuhusika katika mauaji ya waandamanaji wakati wa maandamano siku ya uchaguzi, amejitokeza na kujitetea kupitia video ambazo kwa sasa zinasambaa kwa kasi mtandaoni...
Ujumbe uliochapishwa na Mange Kimambi kwenye ukurasa wa Instagram.
"Dada Mange moyo wangu unavuja damu, Watanganyika tumekuwa watumwa kwenye nchi yetu wenyewe. Tumekuwa mayatima, hakuna jeshi la kutusaidia, hatuna viongozi tuko wananchi kujipigania wenyewe
Hapo ni Nyamongo North Mara. polisi...
Msanii Wakazi kupitia Ukurasa wake wa X (twitter) amewasihi Wananchi kuipigania Tanzania yao badala ya kuandia hastags tu kama trends. Amesema hakuna uhalali wowote wa watu kuuawa hata kama kuna vitu viliharibiwa.
Anasema;
DONT PRAY FOR TANZANIA… FIGHT FOR IT!
Hakuna Mtu perfect, na ni kweli...
Hapa chini ni muhtasari wa taarifa ya awali (final) ya waangalizi wa Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 kutoka SADC (SEOM), uliowasilishwa na Richard Msowoya, Spika wa zamani wa Bunge la Malawi na Mkuu wa Ujumbe wa Waangalizi wa SADC.
Upo kwa kifupi na kwa Kiswahili, ukitaka maelezo zaidi pitia...
Hii nchi niliwahi kusema ukielewa how deep hizi timu za Simba na Yanga zinavyotumika kupumbaza na kuumiza Watanzania, wengi mtalia sana.
Yule jamaa aliyevaa jezi ya Yanga aliyetoka akaenda na wenzake kumiminia watu risasi za vichwa hakuamka tu akaamaua avae jezi ya Yanga na wala hakushtuliwa tu...
Profesa Anna Tibaijuika ambaye ni Waziri wa zamani wa Ardhi, Nyumba na Makazi katika Serikali ya awamu ya nne chini ya Dr. Jakaya Kikwete, ametuma salamu za pole kwa Watanzania wote waliofikwa na madhara ya maandamano ya October 29 na kushauri kwamba wote waliofariki wazikwe kwa heshima...
Mwenyekiti wa UVCCM Taifa kupitia ukurasa wake wa Instagram anasema waliohamasisha maandamano hawakuwepo barabarani — lakini video zipo, sauti zipo, nyuso zipo. Kama si wao, ni nani aliyerekodi?
Na kwa nini misiba ya waliokufa kwa risasi inageuzwa jukwaa la lawama badala ya tafakari ya Taifa?
Mazishi ya Mwananchi aliyeuawa kikatili kwa kupigwa risasi na polisi yamegeuka kuwa maandamano ya sauti na hisia.
Wananchi waimba “Hizo risasi hizo” wakieleza uchungu, hasira, na wito wa uwajibikaji kwa mamlaka.
POLENI WATANZANIA, TUJISAHIHISHE
Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) linafuatilia kwa karibu na limepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za vifo vya Watanzania wenzetu, wakiwamo wanahabari na wengine waliojeruhiwa.Siku ya tukio tulipokea taarifa za vifo vya vijana na askari polisi. Baadhi ya...
Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, ameshangazwa na ushindi wa asilimia 97 aliopatikana na mgombea wa urais kupitia CCM, Samia Suluhu Hassan, katika uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 29, 2025. Lipumba amesema kuwa ni ushindi mkubwa ambao haujawahi kutokea tangu...
Msanii wa Bongo Movie Steven Nyerere kupitia ukurasa wake wa Mtandao wa Instagram ameandika kuhusiana na Muenendo wa wasanii wengi kufuta picha zao wakiwa katika kampeni za Chama cha Mapinduzi (CCM) akisema ni unafiki na kutokuwa na msimamo
"Mstafuuu,....Nimeona Wasanii wengi Wanafuta Picha za...
Akizungumza na waandishi wa habari, Mwenyekiti wa chama hicho Prof. Ibrahim Lipumba kwa niaba ya chama chake cha Civic United Front, amesikitishwa na matokeo hayo yaliyomtangaza mgombea wa CCM kupata kura 97.66%.
Prof. Lipumba amesisistiza kuwa matokeo hayo ni ya kupika na hayawakilishi...
Chama cha Wananchi (CUF) kimetaka kuundwa kwa Serikali ya Mpito (Caretaker Government) ya Tanzania itakayosimamia mabadiliko ya kikatiba na maandalizi ya uchaguzi huru na wa haki, kikikataa matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 kwa madai kuwa haukuwa huru, wa haki, wala wa kuaminika...
Edwin Soko Mwenyekiti wa Taasisi ya Vyombo vya Habari nchi za Kusini mwa Afrika, akizungumza Novemba 5, 2025 katika Mjadala wa Nafasi ya Vyombo vya habari katika Uchaguzi wa Tanzania uliofanyika Oktoba 29, 2025 na kuambatana na vurugu za Maandamano ambapo Vyombo vya habari vilikaa kimya na umma...
Jeshi la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro limeeleza kuwa hakuna mwananchi au askari Polisi wa Jeshi hilo Mkoani humo aliyejeruhiwa au kupoteza maisha kutokana na Vurugu zilizotokea siku ya Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro SACP Simon Maigwa ameeleza hayo Novemba 4...
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Mara, Chacha Heche akizungumza leo Novemba 5, 2025 katika Mahojiano na Chombo cha habari DW ameeleza hali wanayopitia viongozi wa CHADEMA wakikamatwa kwa kuhusika kupanga na kuhamasiha Maandamano yaliyofanyika Oktoba 29, 2025...
Mwanasiasa na Mwenyekiti wa zamani wa Chama cha NCCR Mageuzi, James Mbatia akizunguzma leo Novemba 5, 2025 ametoa Pole kwa Taifa kwa vifo vya kikatili vilivyotokea Oktoba 29, 2025 wakati wa Maandamano nchini.
Pia amesikitishwa na hali ya kisiasa inayoendelea nchini ambayo imekuwa ya kumwaga...
Jeshi la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro limeeleza kuwa liliwashikilia vijana 300 kutoka maeneo mbalimbali mkoani humo kutokana na kudaiwa kushiriki vurugu zlizotokea siku ya uchaguzi mkuu Oktoba 29,2025.
Limesema kuwa baada ya kuwashikilia baadae liliwaachilia huru bila masharti yoyote, kutokana na...
Mkurugenzi wa mawasiliano na uenezi wa CHADEMA Brenda Rupia amezungumza na watanzania na kutoa pole kwa niaba ya chama na wametangaza maombelezo ya siku 7 na bendera kupepea nusu mlingoti kwenye ofisi zao zote.
Nchi yetu ilishuhudia maandamano ya amani yalifanywa na wananchi yalikuwa...
Maandamano ya baadhi ya Watanzania wanaoishi Uholanzi yameripotiwa kuanza muda huu nje ya Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) mjini The Hague. Waandamanaji wamebeba mabango wakipinga kile wanachokiita mauaji ya raia nchini Tanzania, na wakitaka uchaguzi ufutwe ili, kwa madai yao, “wananchi...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.