Naona Sheikh anaendelea kujimaliza tu!
Amezungumza kwa namna ya methali sana moja akisema kwamba mbwa hata ukivalisha mkufu atabaki tu kuwa mbwa na mwingine kasema hao mbwa kuna watu wamewapa kiburi cha kukutukana wewe Rais Samia.
Akamalizia kusema mama umewafanyia hisiani na wanajijua wenyewe...
Wakuu,
Mada hii itakuwa na 'Updates' za Uchaguzi Mkuu 2025 kama yanavyotujia kutoka kwenu kutoka mkoa wa Mara. Ukiwa na taarifa yoyote ambayo ni ya eneo hili tafadhali usisite kuweka
Mkoa wa Mara una jumla ya Majimbo ya uchaguzi 10
Jimbo la Musoma Mjini
Jimbo la Musoma Vijijini
Jimbo la Rorya...
Watangazaji wa Radio47 Kenya, Mkamburi na Japhe, wamehoji mwenendo wa uchaguzi unaoendelea nchini Tanzania, wakibainisha kuwa kampeni zimeonekana kutawaliwa na mgombea wa chama kimoja, Samia Suluhu Hassan, huku baadhi ya wapinzani akiwemo Tundu Lissu kuwekwa kizuizini.
Hata hivyo, muenendo wa...
Naibu Katibu wa Chama cha Wamiliki wa Mabasi (TABOA) Issa Nkya, amewatoa hofu wananchi na abiria kuwa hakijatoa tamko la usitishaji huduma za usafiri wa mabasi ya mikoani na nchi jirani hapo kesho, hivyo huduma zipo kama kawaida kwa saa 24, hivyo wananchi wametakiwa kupuuza taarifa za mtandao...
Tume imesema Kwa mujibu wa Ratiba hiyo, mwisho wa kampeni za uchaguzi kwa Tanzania Bara ni tarehe 28 Oktoba, 2025 saa kumi na mbili kamili (12:00) jioni na kwa Tanzania Zanzibar itakuwa tarehe 27 Oktoba, 2025 saa kumi na mbili kamili (12:00) jioni ilI kupisha kura ya mapema. UCHAGUZI WA RAIS...
Baadhi ya wagombewa wa nafasi mbalimbali kupitia chama cha ACT-Wazalendo Zanzibar wametoa tuhuma wakati wa utekelezaji wa zoezi la kura ya mapema ambalo limefanyika leo visiwani Zanzibar
Viongozi hao ambao ni pamoja na Omar Said Shaaban Mgombea Uwakilishi Jimbo la Pangawe pamoja na Mgombea...
Mgombea Udiwani wa Kata ya Kariakoo kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Haji Manara leo Oktoba 28, 2025, amefanya kampeni za kutembea mtaa kwa mtaa (walking campaign ) ndani ya Kata ya Kariakoo, Jijini Dar es Salaam, akiwaombea kura wagombea wa chama hicho katika nafasi mbalimbali.Katika kampeni...
Mgombea Urais wa Tanzania kupitia CCM, Samia Suluhu kwenye kilele cha kampeni za CCM, Mwanza leo Oktoba 28, 2025 amesema; "Nimekutana na makundi ya waangalizi wa uchaguzi waliokuja kuangalia tunavyofanya na yanayotokea katika uchaguzi wetu. Jambo waliloliona kubwa zaidi ya yote ni kuwa nchi...
Wananchi wilaya ya Rungwe Mkoa wa Mbeya wamesema kuwa hawawezi kujihusisha na vitendo vya uvunjifu wa sheria za nchi zenye viashiria vya kuondoa amani ikiwemo maandamano yasiyo na kibali yanayoweza kusababisha vita ambazo zinaendelea baadhi ya Nchi duniani na kuathiri shughuli za kiuchumi...
Askari wa Vikosi vya Ulinzi na Usalama vya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) wakiwa kwenye foleni wakisubiri kupiga kura ya mapema katika kituo cha kupigia kura Sekondari ya Tumekuja Jimbo la Kikwajuni Mkoa wa Mjini Magharibi
Kwa mujibu wa Sheria Namba nne ya Uchaguzi yam waka 2018...
Katibu Mkuu mstaafu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Bashiru Ali amemtaja Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kama kiongozi mwenye ubunifu, uchapakazi na umahiri katika mipango ya kuwatumikia Watanzania.
Dkt. Bashiru amebainisha hayo leo Jumanne Oktoba 28...
Katibu Mwenezi wa CCM Mkoa wa Arusha, Saipulan Ramsey, amewaasa maafisa usafirishaji (bodaboda) kujitokeza kwa wingi katika zoezi la upigaji kura linalotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025.
Ramsey amesema baada ya bodaboda kupiga kura, wanapaswa kuendelea na shughuli zao huku wakihamasisha abiria...
Tamko rasmi la Baraza la Vijana Chadema Taifa (BAVICHA) kuunga mkono maandamano ya vijana wa Gen Z, kesho Oktoba 29,2025.
==
Baraza la Vijana wa Chadema (BAVICHA) limeundwa kwa mujibu wa ibara ya 7.8.2 (a) ya katiba ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ya mwaka 2006 toleo la 2019...
Aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Victoria, Ezekiel Wenje, amesema suala la kwenda kupiga kura si la vyama vya siasa, bali ni la Mtanzania mmoja mmoja kama ilivyoainishwa kwenye Katiba ya Nchi.
Wenje ameyasema hayo leo, Oktoba 28, 2025, katika Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza, wakati...
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mgombea Ubunge wa Jimbo la Karagwe, Innocent Bashungwa, amewahakikishia Watanzania wote kuwa ulinzi na usalama umeimarishwa nchi nzima, hivyo wananchi wajitokeze kwa wingi kushiriki kupiga kura kuwachagua Rais, Wabunge na Madiwani bila hofu yoyote...
Ndugu wanagenzi, ninalo neno juu yenu!
Kuwa makini sana licha ya kwamba umehakikishiwa usalama au utalindwa, usisahau kuwa hao watu wameshachanganyikiwa ukihisiwa tu unasombwa ndani na kutoka mpaka Yesu atakaporudi. Yawezekana ulikuwa una lengo zuri tu la kwenda kupiga kura ila kwasababu tu...
Sasa Sheikh hii dua kweli itakubalika kweli jamani, watu wakitoa maoni au mitazamo yao ni akili mbovu? hata hivyo kwa sasa mnafanya waumini wajenge taswira mpya kuhusu nyinyi viongozi wa dini
-------------
Katika Dua maalum ya kuiombea nchi yetu Tanzania amani,utulivu na uzalendo iliyoandaliwa...
Mohamed Hamis Mohamed, mgombea uwakilishi jimbo la Amani, Zanzibar kupitia chama cha ACT Wazalendo amelalamikia ukiukwaji wa utaratibu wa kupiga kura ya mapema katika kituo chake ya kupigia kura akidai kuwa kuna watu wameletwa kwa mabasi wamewaingiza ndani na kuanza kupiga kura bila uwepo wa...
Msemaji mkuu wa jeshi la polisi nchini DCP Davidi Misime amesema kuwa Jeshi la polisi litawakamata wote waliohamasisha maandamano hatakama utakuja kupiga kura, miseme amesema utaruhusiwa kupiga kura lakini baada ya kumaliza tukio hilo utachukuliwa na jeshi hilo kwa hatua zaidi.
Amesema...
Mgombea ubunge wa jimbo la Arusha Mjini kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Paul Christian Makonda amepongeza mapinduzi makubwa yaliyofanywa na mgombea urais kupitia chama hicho Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika ujenzi wa miundombinu na uendeshaji wa treni na reli ya mwendokasi (SGR).
Aidha...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.