Mfanyabiashara Nassor Hamdan Seif, Maarufu kama Mzee NBS, Mmiliki wa Mabasi ya NBS Tabora, amefariki leo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam
Mwili wa Marehemu Mzee NBS utasafirishwa kuelekea Tabora kwa Mazishi yake.
Apumzike kwa Amani
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu -TAMISEMI, Prof. Riziki Shemdoe amesema Serikali imetoa Shilingi Milioni 675 kutekeleza mradi wa ujenzi na upanuzi wa Kituo cha Afya Mailimoja cha Manispaa ya Tabora, ili kuboresha huduma za utoaji tiba kwa wananchi zaidi 45,107 wa kata ya Ipuli katika...
Kwa muda sasa hatupatiwi call allowance,, Extra duty allowance hali inayopelekea kukosa morali ya kazi.
Mara ya mwisho kulipwa ilikuwa mwezi wa 10/2025 nayo hayo malipo yalikuwa ya extra duty na call allowance za mwezi wa 03/2025.
Hivyo hadi sasa tunadai extra na call allowance za miezi...
Binti aliyejulikana kwa jina la Tatu Mgeta (23), mwanafunzi wa Chuo cha Tabora Polytechnic College, amefariki dunia huku dereva wa bodaboda akijeruhiwa kufuatia ajali iliyotokea wakati walipokuwa wamepakizana kuelekea chuoni,kugongana na treni ya abiria iliyokuwa ikitokea mkoani Tabora kuelekea...
Serikali kupitia Shirika la Reli Tanzania (TRC) imeanza zoezi la kulipa fidia ya Shilingi bn 3.66 kwa wananchi 2,471 wa Mikoa ya Simiyu ,Mwanza, Shinyanga na Tabora, ambao maeneo yao yametwaliwa kupisha Umeme wa msongo mkubwa utakaotumika katika mradi wa SGR kipande cha 5 (Isaka-Mwanza)...
Jeshi la polisi mkoani Tabora limewahakikishia wananchi ulinzi na usalama katika sherehe za Krisimasi na Mwakampya..
Akizungumza na Waandishi wa habari leo Disemba 24, 2025 Kamanda wa polisi mkoa wa Tabora,Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa polisi, Richard Abwao amesema jeshi la polisi litaendesha...
Mamlaka ya hali ya hewa kanda ya Magharibi- Tabora imesema hali ya ukavu iliyojitokeza kwa wiki mbili katika mkoa wa Tabora ni mabadiliko ya kawaida ya hali ya hewa ambayo hutokea katikati ya msimu wa masika. Akizungumza na CG FM Menena wa mamlaka ya hali ya hewa kanda ya Magharibi Tabora...
Kandarasi wa Mkoa wa Tabora aliyefanya ubadhilifu wa zaidi ya 100ml akumbwa na kadhia kubwa ya aibu na adhabu kali baada ya kushtukizwa na mamlaka za ukaguzi wa miradi nakupelekea kupewa adhabu kali na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mh Paulo Chacha kwa makosa ya ubadhilifu wa fedha za mradi wa soko...
Kituo kipya cha abiria katika Uwanja wa Ndege wa Tabora kimekamilika kwa asilimia 98 na kimekusudiwa kuanza kufanya kazi, ikiwa ni maendeleo muhimu katika miundombinu ya usafirishaji wa mkoa.
Waziri wa Usafirishaji Prof. Makame Mbarawa alikagua na kutembelea kituo hicho, akionyesha kuridhishwa...
Jeshi la Polisi Mkoa wa Tabora limewakamata na kuwashikilia watu watano kwa tuhuma za kupanga njama za kuleta vurugu ikiwemo kuchoma moto vituo vya mafuta, vituo vya mabasi, ofisi za CCM na nyumba za watumishi wa serikali mkoani humo siku ya uchaguzi uliofanyika Oktoba 29, 2025.
Taarifa hiyo...
Maafisa wa Jeshi la Polisi mkoa wa Tabora wakiongozwa na SACP Richard Abwao, Kamanda wa Polisi mkoani humo wamefanya mazoezi ya kawaida ya mwendo wa pole na haraka katika viunga vya Manispaa ya Tabora yakilenga kujiweka tayari kulinda amani na usalama kwa wananchi hususani kuelekea uchaguzi mkuu...
Mgombea Udiwani kata ya Cheyo Manispaa ya Tabora Yusuph Kitumbo amewaahidi Wananchi wa kata hiyo kutatua kero ya Barabara mara baada ya kuachaguliwa kuwa Diwani wa kata hiyo.
Kitumbo ameyasema hayo leo October 4,2025 wakati wa uzinduzi wa Kampeni katika kata hiyo uliofanyika Katika viwanja vya...
Mgombea Ubunge Jimbo la Tabora mjini kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Hawa Mwaifunga leo Septemba 25,2025 ameendelea na mikutano ya Kampeni kuomba ridhaa ya Wananchi wa Jimbo la Tabora mjini kumchagua.
Akiwa katika kata ya Mwinyi Mgombea Ubunge huyo amewaahidi wananchi wa kata hiyo kutatua...
Aliyekuwa Mstahiki Meya wa Manispaa ya Tabora ambaye kwa sasa ni Mgombe wa nafasi ya udiwani Kata ya Isevya kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Ramadhani Kapela amezindua rasmi kampeni ya kuomba ridhaa kwa wakazi wa kata hiyo
Akizungumza na kumuombea kura Rais na Mgombea Ubunge Jimbo la...
Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe, amesema serikali inajenga kiwanda kikubwa cha kuchakata zao la Tumbaku mkoani Tabora, huku maandalizi yakiendelea kwa ujenzi wa kiwanda kingine cha kuzalisha mbolea ya zao hilo, ikiwa ni mkakati wa kuongeza uzalishaji na ubora wa Tumbaku ya Tanzania kwenye...
Kwangu mimi nachofahamu mamlaka ya mapato tanzania (TRA) kazi yake kubwa ni ukusanyaji wa kodi ambazo kodi hizo hupelekwa kwenye miradi ya maendeleo na kulipa watumishi katika taasisi mbalimbali
Fedha hizo za uwekezaji kwenye mpira zimetoka wapi siyo kwamba ni njia ya utakatishaji fedha!
Au...
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imeibua mjadala mkali baada ya kutangaza rasmi umiliki wa timu ya soka ya Tabora United na kuibadilisha jina kuwa TRA United Sports Club. Kwa maneno yao wamedai kuwa hatua hii, inalenga kuhamasisha ulipaji wa kodi wa hiari na kuimarisha uwajibikaji wa kijamii...
Mgombea Ubunge Jimbo la Nzega mjini na Waziri wa Kilimo Hussein Bashe leo Septemba 19,2025 akiwa katika mkutano wa Kampeni kata ya Gongoni Jimbo la Tabora mjini amemlisha kiapo cha kuwatumikia Wananchi Mgombea Ubunge Jimbo la Tabora mjini Hawa Mwaifunga mbele ya wananchi waliohudhuria mkutano...
Mkurugenzi wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima Nchini Professa Philipo Sanga amesema Mkoa wa Tabora ni kinara kwa asilimia kubwa ya watu wasiojua kusoma na kuandika katika mikoa mitano nchini ambayo bado ina changamoto hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari katika viwanja vya maonesho ya...
Umoja wa Wataalamu wa Tiba za asili, pamoja na viongozi wa mila ambao ni Machifu, Watemi na Watwale kutoka mkoa wa Tabora wamekusanyika katika eneo la matambiko ya asili lililopo Izimbili kata ya Kalunde Manispaa ya Tabora na kufanya matambiko ya kimila wakiombea uchaguzi mkuu wa oktoba 29...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.