Musiba: Vyama vya upinzani nchini si wa kweli na wanajihusisha moja kwa moja na CCM kwa lengo la kujinufaisha kifedha

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Aug 29, 2022
862
1,744
Mwanaharakati huru Cyprian Musiba amedai kuwa viongozi wengi wa vyama vya upinzani nchini si wa kweli na wanatumia nafasi zao kama chanzo cha kipato badala ya kutetea maslahi ya wananchi.

Akizungumza wakati wa mahojiano na Jambo TV, Musiba amesema vyama vya upinzani vimegeuka kuwa ajira kwa baadhi ya viongozi wake, huku akidai kuwa baadhi yao wanajihusisha moja kwa moja na chama tawala, CCM, kwa lengo la kujinufaisha kifedha.

Aidha, ameeleza kuwa viongozi wa upinzani maarufu kama Profesa Ibrahim Lipumba, John Cheyo, Zitto Kabwe, Seif Sharif Hamad (marehemu), na Freeman Mbowe hawajawa na athari kubwa kwa maisha ya wananchi, akisisitiza kuwa wengi wao wapo kwa maslahi binafsi na ya familia zao.

 
Kaka Musiba waswahili wanasema ukiona vinaelea vimeundwa hyo trend unayoisema bila shaka iliundwa,na kinachoundwa,zaliwa hukua hatimae hukoma kukua huanza kudecline,na mwisho hufa,kinachoendelea Sasa kupitia uchaguzi wa chadema ni ishara kuwa wananchi wamekwisha shituka,huko mbeleni mambo yaweza kuwa tofauti na km waloasisi hyo trend wakin'gang'ania kunaweza kukatokea impact isiyo njema sana kwa nchi yetu.
 
Back
Top Bottom