KERO DAWASA, Maji yana viambatanisho gani?

KERO DAWASA, Maji yana viambatanisho gani?

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

complex31

JF-Expert Member
Joined
Jun 15, 2016
Posts
578
Reaction score
1,729
Habari,

Kwa takribani miezi miwili kwa vipindi tofauti tofauti maji ya DAWASA upande wa Mbezi Beach yamekuwa yakitoka na rangu nyeusi au yawe machafu ambapo ukikinga kwenye ndoo au tank baada ya muda kuna mchanga/ udongo “una-Settle” kwa chini kwa chombo ulichokikingia.

Mbali na hayo mimi pamoja na familia yangu tulianza kuwashwa baada ya kuoga, nilimuuliza pamoja na baadhi ya jirani zangu na wao pia walitoa malalamiko hayohayo ya kuwashwa na kutokea na vipele vidogovidogo vyekundu, swali langu kwa DAWASA ni haya maji ni safi kwa matumizi ya binadamu?

Kwa wenye hizi changamoto ni kitu gani naweza kutumia au kuweka katika maji kuondokana na hii kadhia? Mtoto wa jirani yangu pia mwenye miaka miwili amekumbwa na hili janga la kuwashwa baada ya kuoga.
 
Ahsante sana, mbadala nimeamua kuweka chlorine mwenyewe pia nina mpango wa kwenda kuulizia filter ni bri gani kwa wataalam wa maji kina Davis & Shirftlife au Merrywater
 
Nafikiri hayajachujwa vizuri.
Wakati huu mvua za masika mto Ruvu kunakuwa na mafuriko yanayo somba tope.
 
Back
Top Bottom