Nipo Temeke hapa Maeneo ya Tandika Makaburuni, dumu la maji ni 50 na umeme ni 24/7
Naomba serikali watoe magari yao waje huku wajaze maji na wawasambazie ndugu zetu wa huko pembezoni na mji.
Hapa Temeke visima vipo vingi sana maji ni 24/7
Nimekuwa nikijiuliza, hivi kama Taifa tunakwamia wapi?
Hivi Tanzania ya leo, ndiyo ihangaike kuwatafutia wananchi wake umeme na maji, baada ya kujitawala toka kwa mkoloni miaka 60 iliyopita?
Nchi iliyojaa rasilimali tele, kama vile mito inayotiririka maji mwaka mzima, maziwa matatu makubwa...
Yaani Dada yangu Farhia Middle hivi Waziri wa Maji Awesso kuwa 'Field' kuangalia Changamoto za upatikanaji wa Maji Mkoani Dar es Salaam ndiyo hadi Umsifu mpaka utake hata Kumkufuru Mwenyezi Mungu katika Kipindi chenu Kizuri cha Mazungumzo ya Familia cha leo ukiwa na Pacha wako Aboubakary Sadick...
Ni dhahiri kuwa maneno ya hayati JPM yana ukweli kuwa hujuma ya kufungulia maji ili yasiende kwenye vyanzo vya kuzalisha umeme vya, Kihansi, Kidatu, Mtera na kwingine ndio chanzo cha mgao na tatizo la umeme hapa Bongoland.
Kama raia wa China na muwekezaji alikuwa anachepusha lita Mil moja kwa...
Yaani miaka 60 ya uhuru nchi inaingia kwenye mgao wa maji!! Tena mgao maji yanapatikana siku moja kwa wiki
Bado kuna watu wanajiona eti wao ndio wenye hati miliki ya kuongoza nchi hii. Siku hizi sasa wamechanganyikiwa na kuanza kuvuana nguo hadharani.
Mmoja anaweka jiwe la msingi kujenga...
Tatizo la uongozi liliopo(vaccum of power) ndo linasababu bei ya vitu kupanda na nishati pamoja na maji kukosa. Tusingizie eti sijui awamu ya tano sijui blah blah. Tatizo liliopo sahivi na ndo chazo ya yote haya ni uongozi legelege usiosimamia kinachopaswa kusimamiwa.
Nafikiri kama huu mgao wa umeme ni kweli unasababishwa na vyanzo vya maji kukauka na kupunguza uwezo wa uzalishaji umeme, inabidi kwenda kujifunza kwa wenzetu wanawezaje.
Uganda na Egypt ni nchi ambazo zinategemea kuzalisha umeme kwa hydropower.
Wao wanawezaje pamoja na mabadiliko ya tabia...
Duniani ziwa Tanganyika ni la pili kwa ukubwa baada ya ziwa Baikal. Ziwa Baikal lina ujazo wa kilomita za ujazo 23,000 huku Tanganyika likiwa na 18,900. Nyasa lina 8,500 na Victoria lina 2,500. Ziwa Victoria linaingia kwenye ziwa Tanganyika karibu mara nane.
Ziwa Tanganyika lina asilimia 18.9...
Hakuna watu wanaoteseka na ukosefu wa maji na umeme kama Wanawake, wao ndio wanaohangaika visimani na ndoo kutwa nzima kutafuta maji kwa sababu wewe unayesimama jukwaani na kusema unawapigania umewakatia maji, sielewi hapa ni haki ipi hiyo ya Mwanamke unayoipigania ? Hivi haya mambo huwa...
#HABARI BODI ya Maji Bonde la Wami/Ruvu imemkamata mkulima mkubwa raia wa China anayefanya kilimo cha umwagiliaji Kijiji cha Kidogozelo Kitongoji cha Migudeni wilayani Chalinze akivuta Maji katika Mto Ruvu kwa kutumia mashine yenye uwezo wa kuvuta maji Lita milioni moja kwa saa.
=====...
Nataka niongee kwa hasira kali na leo Mod naomba mnivumilie lugha yangu. Hapa bongo kuna mambo ya kikhanithi yanaendelea sana na matokeo yake wananchi tunapata shida kwa sababu ya ukhanithi wa watu wachache.
Leo Nipashe wametoa taarifa kuwa kuna mchina amekamatwa anachepusha maji ya mto ruvu...
Tunahitaji kubadilisha muonekano wa fedha zetu sasa, hizi zimesha chakaa na zimeshatuchosha.
Kwa miaka zaidi ya kumi tumekuwa na muonekano huo huo hii ni aibu ya taifa.zania Zinahitajika kubadilishwa
Zaidi ya watu Milioni 2 Nchini Somalia wanakabiliwa na uhaba wa Chakula na Maji kutokana na hali mbaya ya ukame, ikielezwa Vyanzo vya Maji vinakauka.
Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa (UN) takriban watu 100,000 wamekimbia makazi yao kutafuta Chakula, Maji na malisho kwa ajili ya mifugo yao.
UN...
Thawabu Za Kutoa Maji Katika Uislamu: Sababu Saba Za Kujenga Kisima cha BURE
Maji ni neema kutoka kwa Mwenyezi Mungu (swt) ambayo mara nyingi tunaichukulia kawaida, lakini wakati wa ukame, kupitia rehema za Mwenyezi Mungu, tunazidi kufahamu shida zinazowakabili wale wasio na maji salama...
Hahahahahaa!! Inabidi nianze uzi kwa kicheko.
Tumepitia kipindi kigumu kama nchi. Licha ya kuwashauri kwa muda mrefu kwa kurudia rudia tukidhani wanatuelewa wakashupaza shingo.
Leo Rais Samia, Makamu wa Rais na makundi yake yote hawawezi kukwepa mdororo huu wa maji na umeme. Tumerudi mwaka...
Kama Tanzania inazalisha umeme kwa 65% gesi na kwa 35% maji, hivyo jumla ni 100%.
Na ghalfla Tanesco akasema uzalishaji umeme umepungua kwa 21% kutokana na kupungua kwa kiwango cha maji;
Je, maji kwenye mabwawa yamepungua kwa asilimia ngapi? Nitatoa jibu baadae kidogo
TANESCO...
Kwa kweli kuna kipindi tulikuwa na maisha mazuri mpaka tukasahau matenki ya maji.
Sasa wale tuliopo na ofisi ambazo vyoo vyetu vya kuflash na plan za ofisi swala la tank la maji hakuna.
Kila mwanadamu lazima kutoa taka mwili. Nipo ofisini mara nasikia hali si nzuri, kwenda chooni hakuna maji...
Kusheherekea kwa Mbwembwe zote miaka 60 ya Uhuru huku Taifa likiwa na Changamoto muhimu za Maji na Umeme huenda Kikatafsiriwa kuwa ni Kielelezo tosha cha Uzuzu ( Ujuha ) mwingi unaopatikana Afrika na kwa Waafrika wengi ( japo siyo Wote )
Sikutegemea kuna mwana JF anaweza kulalamika kuwa kuna mgao wa maji Dar es Salaam.
Sijawahi sikia wakazi wa Temeke, Mbagala au Kigamboni wakiongelea hadithi za mgao wa maji
Kigamboni ni wilaya mpya watu wanaishi wao na visima vyao vya maji
Mbagala na Temeke wao wanaishi na Maji yao ya kununua...
Kuna muda ni lazima ukweli usemwe maana usiposemwa lazima kumbukumbu zitakuwa za upotoshaji Mkubwa
Kwenye Tatizo linaloikumba Tanzania la ukame na ukosefu wa Maji kwa sasa lawama zangu zote nazipeleka kwa watu wafuatao
1. William Lukuvi
Akiwa Waziri wa Ardhi kuanzia Awamu ya Tano, nchi yetu...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.