Tuna matatizo makubwa sana kama chama, hili lipo wazi kabisa.
Mpaka sasa uongozi ni kama haupo kabisa maana kila kitu kimekwenda mrama.
Mwenyekiti yupo jela kama mahabusu. Makamu mwenyekiti yupo Ubelgiji na inaonekana hana mpango wa kurudi bongo.
Sasa ni kama kuna ombwe la uongozi maana kama...
Kichwa cha habari chajitosheleza
Yaani uwe mshtaki au mshtakiwa bila fedha husikilizwi wala kusaidiwa. Tena ukiwaambia unajua haki zako ndio kabsaa.
Umewatibua, watakutenga na hawatajali malalamiko yako. Huu ni ndio ukweli halisi nendankwenye vituo vyao kazi ukajionee, mara lete elfu arobaini...
Huku sio kuchafuana au kupakana matope bali ni kukosa busara za kisiasa. Maana huwezi kusema kuwa ni Chadema yetu au Ccm yao itachafuka kwa upuuzi wa kutunga mitandaoni.
Hili ni tukio baya la kuterrorise maisha ya watu kama lingekuwa motivated na chama cha siasa asingekwenda mtuhumiwa mmoja...
Kazi ya IGP imekuwa kama vile kazi ya siasa siku hizi. IGP ndiyo kiongozi wa kubambikiza kesi, kutesa wapinzani, kuzuia katiba isitekelezwe, kuongoza mauaji kama watu kupotea na kupigwa risasi.
Lakini kwasababu hii IGP mfano Sirro imefikia wakati ana dharau mawaziri kwasababu ya mila zake za...
Straightly forward, kuna mgogoro wa kisiasa nchini au hakuna? Kama kuna migogoro ya kisiasa tinajengaje uchumi wa nchi? Umewahi kuona wapi inawezekana hiyo?
Kama hakuna mgogoro wa kisiasa ni kwanini kiongozi wa Chama kikuu cha upinzani nchini yupo ndani hadi sasa? Ni kwanini wanachama wake...
Mtafanya nini zaidi ya kuacha mafarakano? Maana taifa lina hitaji amani na mshikamano.
Sheria imefuata mkondo, mwamba yupo mahabusu. Hapa ni kusubiri sheria ifuate mkondo.
Hakuna haja ya kuwa na vinyongo, ungeni juhudi ili taifa lipate maendeleo. Hii ina maanisha kuwa mkubali matokeo na kuacha...
Askofu Gwajima siku zinavyozidi kwenda anazidi kuwaaminishia watanzania kuwa yeye si mtu wa kuyumbishwa yumbishwa na wachumia tumbo hata kama yupo chama cha CCM , ana uwezo wa kumpinga Mwenyekiti wake pamoja na viongozi wote wa CCM kama sehemu ya misimamo yake pamoja na imani yake. Nguvu hii...
Kwa lugha nyepesi tu au kwa maana nyingine hapa nasema kuwa tujitahidi mno kabla hatujateuliwa nafasi yoyote au hata tukiteuliwa tu tuache Kuwatendea mabaya Watu kwani Mungu aliyekuumba Wewe ndiyo huyo huyo kawaumba na Wao.
Kuna mahala fulani hivi nimemuona Israeli kama vile anataka Kuondoka na...
Msimamo wa Rais Samia kuhusu demokrasia ya kisiasa, fujo za kisiasa na fujo za kidini ni wa kujadiliwa kwa kina kusudi watu wengi wauelewe na kuukubali.
Tayari kuna maoni kadhaa yametolewa tangu alipofanya mahojiano yake na BBC, na kuuweka bayana.
Kuna maoni ya Askofu Bagonza, Kauli za...
Watanzania wengi wanachanganywa sana na wanasiasa wanatumia maneno bila kuyaelezea vizuri au kutoa ushahidi. Polisi, CCM na Rais wa Tanzania kwa wao mkutano wa aina yeyote kama wa katiba au kuita Watanzania kujadili kitu chochote kama sio CCM wanaita fujo! au uvunjaji wa amani!. Yaani umeita...
Kama tutakuwa na mifumo yakuwapitisha Viongozi wa ngazi za juu kutuongoza bila kuwa na mifumo ya kuwandaa kiuongozi ni kurudisha taifa nyuma.
Kumekuwa na kasumba ya vyama vya siasa kupachikana kwenye vyeo nyeti na muhimu kwa kutumia bidii ya ushiriki kwenye kampeni.
Katiba mpya iweke vipengele...
Mtu yeyote mwenye kujua sheria anapoona tu kichwa cha thread hii, atasema sio sahihi, Rais Samia hapaswi kuingilia kati suala la mashitaka ya Mbowe ya Ugaidi kwa kuwa hapaswi kuingilia kati mhimili wa Mahakama. Ni kweli.
Lakini pia, Watanzania wengi sana wanaamini kwa dhati kwamba kesi ya...
Wembe ni uleule, CCM ipo kutatua kero za wananchi na kuwaletea maendeleo wananchi.
Habari kuwa kuna wanasiasa walibaguliwa na kutengwa wakati wa utawala wa Hayati Magufuli ni kuleta porojo ambazo hazina mashiko.
Ni Mtanzania gani anataka umoja na wanasiasa ambao hawalitaki mema taifa lao kwa...
Kwa wanasiasa wazuri kila kitu kinachomkumba mtu ni mtaji wa kisiasa kiwe cha heli au Shari.
Mfano Zitto umaarufu wake ulikuwa Sana baada ya kufukuzwa bungeni. Tisheti zikachapwa, Kanga na Mabango Mengi kuelewesha umma nini hasa alichopigania. Nyimbo zikaimbwa za kutoa ELIMU na kumsifu. Hata...
Huyu mzee ametoka kuzika ndugu zake wawili wa damu ndani ya mda mfupi.
Anapitia nyakati ngumu mno pengne kuliko mpinzani yeyote ndani ya nchi hii.
Anakabiliwa na kesi lukuki, uchumi wake binafsi umeporomoka, usalama wake u shakani.nk
Ana miaka 60.
endapo mwelekeo utakuwa ni huu sijui tu.
Kwa...
Ndugu zangu nimekuwa na nyie hapa kwa zaidi ya miaka 7 sasa.
Kulingana na mwenendo wa siasa za nchi hii naomba niachane kabisa na siasa, ni kujipa presha na usumbufu usio na faida.
Mwanzo nilifikiri tatizo ni Marais wanaotawala hii nchi kumbe tatizo sio Marais wanaotawala hii nchi bali ni...
Nimetafakari sana kuwa ni nani zaidi kati ya CCM na Chadema katika kubadilisha msimamo kijamii, kisiasa na kiuchumi? Kwa mfano CCM walikuwa na msimamo kuhusu katiba mpya haki kuanzisha mchakati uliopelekea kukusanya maoni ya wananchi.
Pia ilikuwa na msimamo kuwa Corona haipo Tanzania kwa...
Baada ya ufafanuzi mzuri wa kisayansi uliotolewa na Mkurugenzi mkuu wa NIMR Profesa Yunus Mgaya kupitia Clouds tv sitashangaa kumuona Askofu Gwajima akibadili mawazo na kutimba Ikulu kupata chanjo hapo kesho.
Prof Yunus Mgaya amesema chanjo ya Johnson & Johson inaweza kuwaathiri watu 4 tu...
Mtangazaji: Tuanze na suala la chanjo, tumepata taarifa kesho Rais Samia Suluhu atazindua utaratibu wa chanjo na yeye atachanjwa. Utaratibu utakuwaje kama umeshawekwa na Serikali?
Msigwa: Baada ya kuwasili dozi za chanjo zaidi ya milioni 1, kesho asubuhi mheshimiwa Rais atazindua zoezi la...
Tanzania sio kisiwa, kila tunachokifanya kwenye mapambano dhidi ya Covid 19 kinavuka mipaka na kuonekana duniani kote.
Ni wazi kuwa sasa tumekubaliana kuwa maambukizi ya COVID-19 yapo hata Tanzania, na kuna wenzetu wameugua, wanaugua na waliokufa na wanaokufa kwa ugonjwa huu. Katika hali hiyo...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.