Nakuunga mkono kwa hilo ingawa mashabiki wahafidhina wanamkumbatia De Gea!Ukweli ni kwamba Lindegaard ni bora zaidi.NANI ni mpiganaji ila tatizo lake ni ubinafsi.
Mkuu hali hiyo isikutishe kwani ni kitu cha kawaida kwenye lugha.Hilo ni tatizo la kiotografia.otografia ni utaratibu wa kutumia maandishi kuwakilisha sauti zisikikazo katika lugha.katika otografia ya kiswahili sanifu kuna sauti ambazo huwakilishwa na herufi zaidi ya moja mf:th,sh,mb,mw,nj,ng...
Mkuu hao walimu hewa wameanza leo?hao waheshimiwa wanalijua tatizo tangu zamani,kwa mtazamo wangu hizo pesa zilikuwa zinatafunwa na haohao wakubwa.kama wana ubavu wawachunguze wakurugenzi juu ya upotevu wa pesa hizo ndipo nitakapoamini kwamba wana nia ya dhati ya kulishughulikia suala hili.
pole sana kaka pascal na watanzania wote kwa ujumla.kwa wasikilizaji wa RTD tunawakumbuka vizuri wewe na dada Halima.Binafsi nawakumbuka wakati munatangaza kipindi cha DISCO SHOW kilichokuwa kinarushwa siku ya ijumaa kuanzia saa 5:15 hadi saa 5:45 usiku,hakika mulikuwa munatushika sana vijana...
Ndugu waswahili wenzangu maneno haya yanayohusu wakati nashindwa kuyatumia ipasavyo na mwenye uelewa wa kutosha naomba anielimishe;
alfajiri,asubuhi,mchana,adhuhuri,jioni,alasiri na usiku.kwa mfano nawezaje kutofautisha kati ya alfajiri na asubuhi au mchana na adhuhuri n.k.
Ni sahihi kabisa tunaomba muendelee na zile harakati zenu za kudai pesa ya shoe polish mutasaidia sana vyuo vingine,mukishafanikiwa anzisheni mgomo wa nyongeza ya boom kwa ajili ya sigareti .tehe tehe tehe
Mkuu watumiaji wengi wa neno hilo boreka hutumia kwa maaana ya kuchoka sanjari na neno la kingereza bore.kwa mfano wako wa bora na best,Je kusema X-PASTER ana maisha bora na X-PASTER ana maisha yaliyobestika yote ni sahihi?
Kuna matumizi yasiyo halali ya neno bore ktk lugha kiswahili.Ikumbukwe kwamba neno hilo ni la kiingereza likimaanisha a-kuchosha.cha ajabu ni kuwa neno hilo linaambishwa kwa kuongezewa kiambishi ka ili kuzalisha neno boreka likimaanisha kuchoka.upotoshaji huu wa lugha ya kiswahili hadi lini?
Wana JF chuo kikuu huria Tanzania kinatoa stashahada ya elimu ya msingi ambayo hakuna chuo chochote cha ualimu kinachotoa stashahada hiyo.Aidha ktk wizara ya elimu sijawahi ona tangazo au maelekezo yoyote kuhusiana na stashahada hiyo!Taarifa za uhakika ni kwamba aliyemaliza na kufaulu stashahada...
AROOO!nikisema up lala chini na nikisema down inuka juu.mimi ndiyo afande mwita nimesoma pare sekondari ya jangwani secondary school.tehe tehe tehe tehe.
SCHOOLING IS USELESS BECAUSE SCHOOLS ARE MAKING PEOPLE MORE STUPID AS HOSPITALS ARE MAKING PEOPLE MORE SICK-IVAN ILLICH
(1926-2002)
Baada ya wizara ya elimu kuridhia uanzishaji wa shule za binafsi na kuona utitiri wa shule zisizo na ubora sasa hali hiyo imehamia kwenye vyuo vikuu.sasa hivi kuna vyuo vikuu miundo mbinu yake hamna tofauti na vyoo,wahadhiri hawapo maktaba ndiyo usiseme!aghalabu vyuo hivyo
hutoza ada kubwa...
l
kumbukumbu zaonesha kuwa alimaliza darasa la nne kwenye shule ya kichwele(kwa sasa uhuru mchanganyiko) mwaka 1922 kisha alirudi pangani na hatimaye aliajiriwa kwenye idara ya forodha hapo pangani.si vibaya ukitujuza kama kuna kozi zingine alisoma baada ya ajira hiyo ya mkoloni
Kwa wasiofahamu elimu ya mwandishi wa vitabu vya riwaya na mashairi hayati shaaban Robert ana elimu ya darasa la nne.Unazikumbuka
kazi zake hizi?Kusadikika,kufikirika,Adili na Nduguze n.k.Je hao wasomi wetu wa sasa na phD zao za vitini watamfikia huyu?
Jana wakati waziri wa habari wakati akihitimisha hotuba ya makadirio ya wizara yake alisema bila kutafuna maneno kwamba serikali
itaendelea kuwaunga mkono miss Tanzania na kushadidia kuwa kadri siku zinavyoenda mashindano hayo yataendelea kuboreshwa,
lakini kitu cha ajabu ni kwamba amesiliba...
Wanajamvi katika siku za hivi karibuni nilipata taarifa kwamba Ramsey Noah na kanumba wanafanya movie ya pamoja.sasa nataka
kufahamu kama hiyo movie iko tayari au la.Tafadhali naomba munijuze
Nimekuwa nikifuatillia mijadala kadhaa kuhusiana na ubora wa elimu ktk vyuo vikuu vyetu hapa TZ na wengi wakitoleana maneno
yenye kadhia na wengi wao wanapigia upatu vyuo vya UDOM na UDSM.Vijana wanagombea fito ilhali nyumba ni moja!Mimi ninafikiri watz
wangejadili vile vyuo ambavyo hata...
Hawa jamaa wa TCU hamnazo kabisa!Eti wanasema wanafunzi wasiochaguliwa waombe tena.Swali ni kwamba wanafunzi watajuaje kama wamechaguliwa wakati majina ya waliochaguliwa hayajatolewa?
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.