Hapo ni kweli kabisa; umenena. Kwa hali ya sasa kazi ama biashara ya kujiajiri yenye uhakika wa kesho hakuna, hata hiyo kulima yenyewe mazingira ya hali ya hewa si ya uhakika kabisa.
Masharti tunafuata; kodi kwa wafanyakazi ina afadhali kubwa kuliko wafanyabiashara. Na mfanyakazi yoyote ana uhakika wa kudaka mwisho wa mwezi, tofauti na biashara unapotoka asubuhi; hujui kama biashara itafanyika ama la. Inakuwa bahatisha ndulute.
Tunarudishaje ambacho hamjakinunua? Nunueni kwa faida tulipe tukiwa kama mawakala wa ukusanyaji kodi. Nauli unayolipa kwenye chombo chochote cha usafiri hatujakuwekeni gharama za vipuri; gaharama za faini n.k.
Kama endapo mpo tayari nauli kipanda itapendeza zaidi ili tuweze kukusanya kodi...
Si kwa Tz; mlaji wa mwisho hamkadirii bali wakala mkusanyaji ambaye ni mfanyabiasha. Hawana kuangalia kipato cha mwenye biashara anachoingiza. Wanachanja hadi mtaji na si faida itokanayo na biashara.
Mm nahisi kwa kuwa hawana biashara yoyote; ama wale wafanyakazi wao kutokuwa wafanyabiashara, kunachangia wao kutokujua vyema ugumu wa biashara zenyewe. Ni sawa na mtu anaye fanya jambo kwa nadharia na si vitendo.
Habari zenu wote humu ndani wakuu, nimejaribu kutafakari kwa kina, na kuwaza juu ya ulipaji kodi hapa nchini kwetu, na kubaini wale wafanyakazi karibu wote wa TRA, Na mamlaka nyinginezo za ushuru na kodi. Hawana uzoefu na biashara wanazo toza kodi au mapato.
Nimeona niandike ili nao waweze...
Ilaumiwe serekali; na si Tanesco, wao Tanesco hawafanyi manunuzi ya mitambo bali serekali. Pia umeme ni mgawo ila wamenyimwa kutangaza kwamba ni mgawo.
Mgogoro utaibuka ccm, mtaipata pata. Subirini muone. Kwa CDM walio ondoka, walisha jitambua hawewezi kupata vyeo kule kwa kuwa watu makini CDM ni wengi.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.