Hunyu
JF-Expert Member
- Aug 19, 2014
- 4,775
- 4,316
Nakushauri, fanya nae kikao. Umueleze jinsi unavompenda na jinsi ungetamani maisha yenu yawe na ya mtoto wenu.Ktk hali ya hasira, lakini si mara ya kwanza kurudia kauli kama hizo. Amekuwa akirudia mara kwa mara sana.
Baada ya hapo mweleze kwa upole kabisa na kwa upendo jinsi ulivyoumizwa na kauli yake ya kuwa anakuchukia sana toka moyoni.
Mwisho: mwambie kuwa hakuna haja ya yeye kuendelea kukuchukia wakati uamuzi anao yeye. Mwambie atoe yaliyomoyoni mwake kwamba ili aache kukuchukia angetamani uweje au ufanye nini. Pia mpe uhuru wa kuamua hatima ya maisha yake hapo hapo kuliko kuendelea kukuchukia.
Kwa maana nyingine, usiwe chanzo cha familia yako kusambaratika wala kuachana. Mwachie yeye mwenyewe afanye chochote anachotaka kwa usalama wako, wake na wa mtoto wenu.
Nina imani, kama ataamua kuondoka huo utakuwa mwanzo wa yeye kuhangaika na kujitaftia msaibu ambayo kwa sasa hako nayo. Miaka inayokuja atarudi kwako kwa magoti na kulia.
Kumbuka usalama wako kwanza.