Kabila gani linaweza thubutu kudai ndio wazawa wa asili wa TZ? Hakuna. Tunadanganywa na hawa waliosoma masomo ya ujanja ujanja na rahisi ya historia, lugha, utamaduni, nk na bahati mbaya wengi wamejipenyeza kwenye siasa na utawala. Tuheshimiane. Kabila letu kwa sasa sisi ni Watz au ukipenda...
Hapana Brigit86, hakuna dhambi au uovu ambao Bwana Yesu kristo hawezi kusamehe, Yeye anasamehe dhambi na uovu wa aina yote. Wala kwake hakuna dhambi kubwa au ndogo. Tena kwake hakuna dhambi ya kawaida na au isiyo ya kawaida. Usiogope huo ni mzigo kuna pa kuutua na maisha yakaendelea (Mathayo...
Hapana siyo kweli ndugu yangu Sky Eclat. Bwana Yesu halisi hakuacha picha wala taswira ya sura yake ya namna yoyote ile. Tena taswira za inayodaiwa kuwa ni ya Bwana Yesu ni janja ya shetani kuwaingiza watu kwenye Ibada ya sanamu (Habakuki 2:18). Jihadhari hizi ni siku za mwisho ni siku za...
Iwapo umebabatika kufika ktk maeneo walikopatiwa makazi wakimbizi hususani kutoka Burundi, hali ya usalama ni mbaya utafikiri si Tz. Watz wenzetu wanauawa na wakimbizi hawa, we acha tu. Jamaa hawa jirani zetu walikwishakata tamaa hivyo roho ya utu ilikwishawatoka. Wanachinja ndugu zetu Waha kama...
Jengo la msikiti ukiliona limefikia hatua kubwa na litakuwa limechukuwa muda mrefu hadi kufikia hapo. Kwa vyovyote Serikali kupitia Idara zake ilihusika na hasa Ardhi, majengo na mipango miji. Kelele? Mbona watu wa imani zote hapa Tz hata S'wanga bila shaka wanaelewa baadhi ya taratibu za...
Napoleon, pole sana! Kwa TZ ukitaka ku - win ajira nzuri yenye future soma lugha, saikolojia, sheria, human management, policy making, ubalozi. Kwa jumla haya masomo ya nadharia ambayo ili kujitutumua wanaita pia sayansi ili angalau kuyapa uzito na heshima. Uliyesoma utabibu, kilimo, uandisi nk...
Inasemekana na kukadiriwa kuwa 50% au zaidi ya watawala wetu kwa sasa ni walimu, wanatoka kwenye ualimu wa shule za msingi, sekondari. Walihitimu 'O' level daraja la IV au la III wakawa walimu wetu wa shule za msingi. Wakatengeneza vyeti (through QT) wakasoma kidato cha V na VI kwa njia ya posta...
Ndugu yangu Nyani, wamekukwaza kwa kweli unastahili kughadhibika. Pole sana. Binafsi mie nakukubali na kupitia michango yako nilikwisha gundua kuwa wewe ni mchangiaji huru. Huna upande. Wanakuongopea. Akutukanaye. Hata hivyo, kama tunataka kuiimarisha Forum yetu tujitahidi kujenga hoja zenye...
Hapana kwa tulopita jeshini, wewe lisikie tu shambulio la kushtukizwa (ambush). Ni balaa! Hata mtoto mdogo anakupiga anavyotaka. Yaliyosemwa na UN juu ya udhaifu wa MONUSCO naunga mkono. Hawako vizuri ktk mafunzo ya kukabiliana na matukio ya ambush. Watu wanakabiliana na ambushers muda wote ule...
Ndugu kisingi niambie! Kuna watumishi wanaomba kustaafu kwa hiari kufuatia tetesi kuwa muswada umesainiwa na Bunge wa wastaafu kuwa watakuwa wakilipwa 38% ya kiinua mgongo na zinazosalia kulipwa kwa mwezi. Imewatisha na kuwavunja moyo watumishi wengi wa Serikali hususani waliobakiza miaka 10 -...
Hapana ndugu, watoto tunapaswa kuwategemeza wazazi wanapokuwa wameanza kuishiwa uwezo wa kufanya kazi. Huu ni utamaduni na desturi yetu nzuri na yenye kufaa Watanzania tulirithishwa na mababu zetu vizazi na vizazi. Hata mwenyezi Mungu anatufundisha na kutuhimiza juu ya hili. Ni wajibu...
Ndugu MSIMISEKI S... ulilosema hapa nalikubali. JF ukichunguza baadhi ya articles watu wanaandika uongo. Haitosaidia. Sana itatujengea mazoea na baadaye tabia ya kuwa watu waongo na wazushi. Tabia mbaya. Jambo kama hili kabla ya kuwahabarisha wana JF wenzio hakikisha umefanya uchunguzi wa kina...
Katika Kitabu cha Mathayo 11:28 Bwana Yesu kristo anakualika uende kwake atalikomesha hilo tatizo lako. Ni dogo sana Kwake. Wewe na mkeo wote mnaendeshwa na mapepo ya uzinzi na uasherati. Tafuteni Kanisa la Kipentekoste, mtaombewa, demons hao watapigwa kwa moto wa Roho Mtakatifu na watakimbia na...
Kunradhi, Reucherau, wewe ni muumini ktk imani gani zilizopo hapa Tz. Iwapo ni Mkristo, Je, waweza kuwa hujui kwa nini Israel mpaka leo ni Taifa teule na Takatifu kwa Mungu Yesu Kristo, Mungu aliye hai aliyeumba mbingu na nchi na vitu vyote vilivyomo? Kwani mkono wako kunajisika kwa kuchafuliwa...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.