Tena basi, hata huku fbook, tumeona mashambulizi mengi karibu ya mwezi wa Ramadhan na ndani ya Ramadhan. Hakika chuki zao zinapofusha uwezo wao wa kufikiri.Story inaeleza kuwa hata Hussein kajeruhiwa,wao hawalioni hilo. Allah Atuhifadhi na Atuongoze sisi na wao.
Maelezo yanasema tukio limetokea saa 1.20 USIKU. Aidha maelezo yanaonyesha akiwa anatokomea baada ya tukio tajwa, alimjeruhi mtu mwingine, aitwaye........HUSSEIN.
Kuwashindisha na njaa watumishi wa ndani wasio Waislamu sio sahihi,kwa kuwa sharti la kwanza la kufunga funga ya Ramadhan ni kuwa Muislam. Wanaofanya hivyo wajirekebishe.
Naomba nifahamishwe, endapo Viongozi wa Chama cha siasa wanahitaji kukutana na watendaji wa Serikali,kama vile Halmashauri kama hiyo ya Monduli, utaratibu wa kuwasiliana nao kupitia kwa Mkurugenzi ambaye ndiye mkuu wao wa kazi,unapaswa uwe vipi?
Sina hakika kama mtoa maoni haya ni Muislam, lakini kwa vyovyote iwavyo,kila anayetaka kuujua Uislam anayo fursa ya kujifunza kutoka vyanzo vikuu viwili vilivyo muhimu,navyo ni Qur-an na Sunnah. Historia ya Mtume Muhammad SAW inashuhudiwa kuwa mmoja wa wake zake, Maria alikuwa ni...
Uislamu unaruhusu kuwepo kwa wasio Waislamu,na jambo hilo ni mashuhuri hata wakati wa Mtume Muhammad SAW, pale Madinah walikuwepo Wayahudi na Wakristo wakiwa chini ya himaya ya Uislamu. Huo ndio Uislamu unaozingatia kuwepo kwa watu na uhuru wao wa kuabudu wanachokiamini wao wenyewe.
Hapa kwetu Tanzania, na katika nchi nyinginezo adhabu ya kifo hutekelezwa. Katika shariah ya Kiislamu,adhabu ya kifo pia ipo. Tujadili kwa hoja, kuna tatizo lipi hasa? Kuuawa hadharani au kwa kuwa adhabu hiyo imetolewa katika nchi yenye Waislamu wengi?
Tanga-Pangani Road wakati mwingine huwa na matatizo pale Mgwisha-Tongoni na katika madaraja ya Kirare hasa mvua zikizidi mno. Hali ikoje siku hizi.tunataka kuja Pangani!
Imesimuliwa kutoka kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.): “Twaeni tabia tatu kutoka kwa kunguru; kujamiiana kwa siri, kwenda kutafuta riziki mwan- zoni mwa asubuhi, na akili na hadhari dhidi ya hatari zinazoweza kujitokeza.”
Maurice Bucaile,Mwanasayansi na mwandishi wa kitabu kiitwacho: The Bible,Qur-an and Science, ukimsoma unaweza kupata mengi kuhusu huyo Firaun alifariki katika maji. Huyo ndiye ambaye Qur-an ilimzungumzia kuwa atahifadhiwa ili iwe mazingatio kwa watu. Mtoa post namshauri apate wasaa wa kukipitia...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.