Recent content by lugamba2001

  1. L

    Kwa nini usomi wetu ugeuke kuwa laana kwa Watanzania?

    kwa hakika yapo mengi ayafanyayo, mwandamu lakini, kuiga kuna madhara makubwa zaidi! Mara zote tuwahusisha wasanii na mambo ya kuiga, lakini ukweli twawaonea tu, uigaji mbaya zaidi ni ule wa kukopi kitu cha kitaaluma na kuhamisha kitu kama kilivyo bila kujali mazingira na wakati!
  2. L

    Kwa nini usomi wetu ugeuke kuwa laana kwa Watanzania?

    Ukifanikiwa kuongea na wanafunzi wanaomaliza darasa la saba, kidato cha nne au hata cha kidato cha sita, wengi wao kama si wote, wana ndoto za kuendelea kusoma, hadi vyuo vikuu na ikiwezekana nje ya nchi. Hili la kujivunia kama nchi, ni swala linalotufananisha na wengine wote waishio ulimwenguni...
  3. L

    Kiboko ya Wanandoa na wapenzi wasio waaminifu

    Mmmmmh! Hiyo software yako, huku India tayari imeshaleta mizozo! Gazeti la The Hindu la leo lilikuwa na story yenye visa vya 'spyware' kama hiyo. Bahati mbaya sijaweza kupata link ukajisomea mwenyewe, wameiona ni story ya kawaida hivyo wameshaitoa online. Lakini ukweli ni kuwa hiyo 'investiment'...
  4. L

    Marrying a chagga

    huu ni utanii tuu... lakini wa kiukweli kweli vile!!!
  5. L

    Mayahudi Weusi

    Nadhani ni sahihi kujadili maswala ya dini kwa mtizamo 'positive', lakini kwa kuwa wengi wetu uvumilivu wetu kwa asiye wa upande wetu ni robo, na kwa kuwa swala la imani ni 'private matter' zaidi, hivyo unapojadili imani za watu kwa kweli inakupasa uwe makini. Mijadala mingi ya kidini...
  6. L

    So Violent people on earth?

    Ama kweli mbuzi wa maskini hazai na akizaa ni madume! Napendekeza jamii forums uanze utaratibu wa kuchambua mada zenye kufanana na jina lako! kama umeshanunuliwa kama wale wengine basi tujue, maana sasa tunashindwa, hatuoni cha kusoma, wala cha kuchangia, kila siku mizozo au mashindano...
  7. L

    Kikwete: Unprepared to lead

    Kila Mtanzania, hata mtoto mdogo, anelewa jinsi JMK alivyoshindwa kama Rais wa Tanzania na mwenyekiti wa chama chenye historia ya pekee africa (CCM)! Dalili ziko kila mahala, si serikali wa CCM wenye kujua wanakoelekea! Serikali haina mwelekeo, kila siku inaibuka na jipya wakati la awali...
  8. L

    Nini chanzo cha wizi bongo!?

    Kweli yaonyesha uchovu ni mwingi miongoni mwetu! Ukiwa uwezo wako ni kuona karibu sana, kioo kitafaa kukuonyesha uso wako! Utahisi siku zote we wang'ara, kumbe mwili wako si uso pekee! Na ukishaona umeng'ara sana usoni, ongeza kioo cha pili ili uone na kisogo pia! Je chan'gara pia? Maana...
  9. L

    UDOM kuajiri wahadhiri 50 toka India?

    Tanzania ni nchi ya ajabu kidogo, labda ndiyo uchanga wenyewe! Ina viongozi ambao mara wafikapo ofisini, hutafuta nini kiwape umaarufu wa haraka haraka, japo wa muda mfupi tu. Hawajali, wala kuzingatia mipango ya maendeleo iliyofanyiwa utafiti na vitengo vya mipango (Planning) vilivyojaza wasomi...
  10. L

    UDOM kuajiri wahadhiri 50 toka India?

    Habari za uhakika toka kwa raia wa India, aliyepata mkataba wa Kufundisha Sociology UDOM, zinasema kuwa raia wa India wapatao 50, wamepata mkataba wa kufundisha katika Chuo kikuu cha Dodoma, ambapo watalipwa dola za Kimarekani 3,000/ kwa mwezi. Mwandishi wa habari hii, alikutana na jamaa huyo...
  11. L

    Nini chanzo cha wizi bongo!?

    Ndugu wana jamii forums! hoja yangu, ni nyepesi kuisoma lakini ukiiangalia kwa undani ni nzito! najua kila mtu aweza kutoa jibu lake kwa haraka haraka, lakini mimi napenda tufikirie na tutafiti kwa umakini mkubwa na pengine waliokwishafanya utafiti watuambie, labda tunaweza kuioko jamii yetu...
Back
Top Bottom