Walimwengu ndo wabaya
Jama nipo mahututi, tena ndani icuu
Mekurubia mauti, nahema kwa juu juu
Siwezi swali kunuti, Mola anipe nafuu
Dunia haina baya, walimwengu ndo wabaya
Wamenipiga ulozi, ule wa chuo kikuu
Kwa uchanga kimalezi, sijafikia wakuu
Nipo mbali na wazazi, kwa mamita elfuu
Dunia...