Shairi: Walimwengu ndio wabaya

Shairi: Walimwengu ndio wabaya

Dr leader

JF-Expert Member
Joined
Jun 28, 2016
Posts
1,067
Reaction score
1,425
Walimwengu ndo wabaya

Jama nipo mahututi, tena ndani icuu
Mekurubia mauti, nahema kwa juu juu
Siwezi swali kunuti, Mola anipe nafuu
Dunia haina baya, walimwengu ndo wabaya

Wamenipiga ulozi, ule wa chuo kikuu
Kwa uchanga kimalezi, sijafikia wakuu
Nipo mbali na wazazi, kwa mamita elfuu
Dunia haina baya, walimwengu ndo wabaya

Mniombee na dua, ili iwe asibabu
Haya ninayo ugua, yeye ndo wa kunitibu
Msidhani ni mafua, nikaenda kama dubu
Dunia haina baya, walimwengu ndo wabaya

Abuuabdillah ✍️
0744 883 353
 
Back
Top Bottom