Wao wa magharibi wafanye biashara na Russia ya matrilioni ya madola kupitia chini ya kapet, ila nyinyi hamruhusiwi kufanya biashara yoyote ili muendelee kuwa ombaomba kwao.
Mkuu hiki tunachokiona kinachoendelea ni kweli au tuko kwenye ndoto? Marekani kufikia kudhalilika kiasi hiki? Mbona mporomoko wa kasi namna hii? Hii ndio Marekani ya kina George W Bush au nyingine? Hapana aisee!
Hahaaa Iran kajichokea? Wakati huohuo Marekani kapaki tumeli twake twa mwaka 1962 kuleeee karibia na Srilanka anavizia meli za mizigo kaungana na maharamia ya Somalia kuteka dadeki, sijui angekuwa Iran hajachoka ingekuwaje hahahhaa
Marekani mzee wa propaganda za kuitisha dunia imuogope ..Hazalishi kiwango hicho cha mafuta, mafuta yaliyomo kwenye reserve yake underground ni ghali sana kuyatoa, ndio maana kununua ya nje kwake ni rahisi zaidi, sio kila cha kuambiwa tunaamini. Inawezekana ni siku moja tu alitoa hayo mapipa...
Rekebisha kidogo,
Sio misikiti bali Musallah ( Chumba cha kusalia) yaani 5m x 5m chumba kidogo tu kinatosha kabisa.. Wakati abiria wanasubiri kuondoka na muda wa Swala umefika.
Hiyo Subaru ilitengenezwa kwa soko la Japan, nchi yenye baridi kali ndio maana ilitakiwa itumie oil ya 0W20 , kama upo Dar, tumia oil yenye grade 10W30 synthetic..
Grade ya oil inategemea hali ya hewa gari inapotumika sio aina ya gari.
0W20 ni nyepesi sana kwa hali hewa ya kwetu. Fanya utafiti...
Kwa hiyo hao wengine waliondaa hayo mashindano ya AFCON sijui Cote de Ivoire, Cameroon, Gabon, Equtorial Guinea wana maendeleo gani ya kimiundo mbinu ya ajabu kutushinda sisi? Mbona ni mafukara tu pangu pakavu na wamefanya?
Huo uweusi jiulize sababu ni nini, weka madawa ya kupaka pembeni.
Fuatilia na ufanye utafiti dalili ya kiafya inayoitwa Insulin resistance,
Ni sawa na gari itoe moshi mzito mweupe halafu unaipeleka car wash waisafishe labda itaacha kutoa moshi. Insulin Resistance is real.
Sikiliza wewe usiejua kitu, kama kitu hujui uliza..
Uislam umempa haki baba mtu agawe mali yake apendavyo wakati yuko hai, anatakiwa awagawie wote watoto anaodhani ni wakwake walio nje ya ndoa madhali yuko hai.. Isitoshe bado pia kapewa nafasi tena kuandika wasia / wosia ya mali yake sio zaidi...
Kwahiyo hiyo sheria ya mtoto wa nje ya ndoa ili arithi sharti iwe lazima mtoto afanane na babayake, asipofanana na babayake harithi.. Basi itakuwa sheria ya ajabu sana hiyo hahahahhaa
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.