Rekebisha kidogo,
Sio misikiti bali Musallah ( Chumba cha kusalia) yaani 5m x 5m chumba kidogo tu kinatosha kabisa.. Wakati abiria wanasubiri kuondoka na muda wa Swala umefika.
Hiyo Subaru ilitengenezwa kwa soko la Japan, nchi yenye baridi kali ndio maana ilitakiwa itumie oil ya 0W20 , kama upo Dar, tumia oil yenye grade 10W30 synthetic..
Grade ya oil inategemea hali ya hewa gari inapotumika sio aina ya gari.
0W20 ni nyepesi sana kwa hali hewa ya kwetu. Fanya utafiti...
Kwa hiyo hao wengine waliondaa hayo mashindano ya AFCON sijui Cote de Ivoire, Cameroon, Gabon, Equtorial Guinea wana maendeleo gani ya kimiundo mbinu ya ajabu kutushinda sisi? Mbona ni mafukara tu pangu pakavu na wamefanya?
Huo uweusi jiulize sababu ni nini, weka madawa ya kupaka pembeni.
Fuatilia na ufanye utafiti dalili ya kiafya inayoitwa Insulin resistance,
Ni sawa na gari itoe moshi mzito mweupe halafu unaipeleka car wash waisafishe labda itaacha kutoa moshi. Insulin Resistance is real.
Sikiliza wewe usiejua kitu, kama kitu hujui uliza..
Uislam umempa haki baba mtu agawe mali yake apendavyo wakati yuko hai, anatakiwa awagawie wote watoto anaodhani ni wakwake walio nje ya ndoa madhali yuko hai.. Isitoshe bado pia kapewa nafasi tena kuandika wasia / wosia ya mali yake sio zaidi...
Kwahiyo hiyo sheria ya mtoto wa nje ya ndoa ili arithi sharti iwe lazima mtoto afanane na babayake, asipofanana na babayake harithi.. Basi itakuwa sheria ya ajabu sana hiyo hahahahhaa
Mtoto atarithi mali za baba yupi?. Maana Mama yake katembeza kitumbua kwa wengi, baba ni yupi? Au kwa sababu Marehemu alikuwa na vijisenti ndio aangushiwe nyumba bovu? We vipi bana!
Sheria ya mirathi ni kama sheria ya uraia wa nchi, kuzaliwa nchini bila kutimiza masharti mengine ya uraia hakukupi haki za uraia hata kama ulizaliwa hapahapa na unaongea kiswahili fasaha kuliko Shabaan Robert na umeishi nchini miaka 50.
Wewe unamjua Trump au unamsikia ?yeye na mambo ya pesa hataki mchezo kabisa, huyo ni mfanya biashara bahili kwelikweli, pesa ya hazina ya Marekani anahisi kama za kwake binafsi.. Usiku na mchana anawaza akapore wapi pesa, wewe unazungumza eti ataijenga Israel, acha mzaha Mzee..!
Mtu na akili zake timamu anamsikiliza na kumuamini Trump.
Vipi Canada na Greenland zimeshajiunga na Marekani? Na ile Riviera ya Gaza inaendeleaje? Bila kusahau ile siku ya kwanza akiingia madarakani atampigia simu moja tu Putin na vita ya Ukraine vitasimama hahaha ngoja tumuulize Elon Musk !
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.